Mbunge pekee wa CHADEMA, Aida Khenan ahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Dkt. Magufuli jijini Dodoma

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,190
4,103
Mbunge pekee wa CHADEMA, Aida Khenan wa Jimbo la Nkasi Kaskazini ahudhuria sherehe za kuapishwa kwa Dk John Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Aida Khenan ametoa msimamo mwingine kuwa hawezi kuwasaliti wananchi waliomchagua kuwawakilisha hivyo anasubiri kuapishwa aingie bungeni. Awali Mbunge huyu alitoa msimamo kwamba watakachosema viongozi wa chama chake ndicho atakachofuata.

"Chama kiliniamini kikarudisha mamlaka kwa wananchi na wananchi wamenipa mamlaka. Kama niliapa Chadema siwezi isaliti hali kadhalika siwezi wasaliti wananchi wa Nkasi Kaskazini.

Naomba nitoe msimamo wangu, mimi Aida nimechaguliwa kwa mujibu wa sheria na ni mbunge halali wa Nkasi Kaskazini, ninasubiri kuapishwa na hakuna jambo jingine, sina mabadiliko mengine".

Aidha Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amesema kuwa kamati kuu itakaa na kutoa msimamo wa chama wa jumla kama kuendelea na msimamo wa awali uliotolewa na viongozi wakuu wa chama au vinginevyo.

Lakini pia ameongeza kuwa kama kamati kuu ya chama ikibariki maamuzi ya viongozi wakuu wa chama basi Aida kama atabaki na msimamo wake wa kwenda bungeni itabidi atafute namna nyingine ya kuwatumikia wananchi wa Nkasi.


1604687638076.png

1604687741834.png

 
Ana bonge la mwanya na dimpoz for pozi

Kawageuka wenzie kama Lamwai alivyofanya kule NCCR na Silver spoon yake.

Siasa sio uadui.
 
Inavyosemekana ataambiwa akae pembeni, akileta kiburi atafutwa uanachama, halafu kutatokea mgogoro mkubwa zaidi pale baadhi ya wabunge wazoefu waliokatwa watakapoanza kupewa mema ya nchi...
 
Kwakweli nampongeza sana huu uhuni wa Chadema kutaka kumdhulumu Dada wa watu haki yake ya kimsingi ya kuwawakilisha wananchi waliomchagua haukubaliki hata kidogo.

Uchaguzi umeisha sasa tuijenge nchi

CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Huyu mguu mmoja upo CCM, huhitaji hata elimu ya vidudu.

Watamfukuza, atahamia CCM na ubunge wake kwa maana hata itokee by election leo wapinzani hawana hata hamu na uchaguzi tena.
 
Huyu mwanamama mliomuamini na kumpa nafasi ya kugombea kupitia chama chenu na akafanikiwa kupenya, huenda sio mwezunu/mwenzetu bali ni mtu wa system aliekuwa na kazi maalumu ya kufanya ndani ya chama na ndio maana kapenya.

Hivyo, nawashauri muwe nae macho sana kwani anaweza kuwavuruga wakati wowote.

Huyo mwanamama hata watu wa chama cha mbogamboga nao nahisi watakiwa hawamjui.

Hajapita bure huyo!
 
Inavyosemekana ataambiwa akae pembeni, akileta kiburi atafutwa uanachama, halafu kutatokea mgogoro mkubwa zaidi pale baadhi ya wabunge wazoefu waliokatwa watakapoanza kupewa mema ya nchi...
Kwa hapa bongo somtyme Maisha bila unafiki hayaend
 
Back
Top Bottom