Mbunge Ole Milya amtuhumu RC Mnyeti kwa rushwa, ahoji ukaribu wake na kampuni ya Tz One, Mnyeti Ajibu mapigo

buswelu moja

JF-Expert Member
Aug 24, 2014
226
147
Mbunge Ole Milya amtuhumu Rc Mnyeti kuhusu rushwa,ahoji ukaribu wake na kampuni ya Tz One , Rc Mnyeti Ajibu mapigo

Mwandishi Wetu,Mirerani

Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya amemtuhumu mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti kwamba anapokea rushwa ili kuwakandamiza wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite walioko eneo la Mirerani mkoani Manyara.

Ole Milya ametoa kauli hiyo Leo Julai 28 mwaka huu katika mji mdogo wa Mirerani mbele ya kamati ya kuchunguza na kutatua mipaka baina ya wachimbaji wadogo na kampuni ya Tanzanite One.

Hatahivyo, Ole Milya alienda mbali zaidi na kuhoji ukaribu baina ya kiongozi huyo wa serikali na kampuni hiyo huku akisema kwamba hatakubali kuona haki za wanyonge zinakandamizwa pindi akiwa madarakani.

"Nimwombe Mheshimiwa mkuu wa mkoa urafiki wake na Tanzanite One ufikie mwisho, usiliingize taifa hili kwenye migogoro isiyostahili "alisema Ole Milya

Alisisistiza kwamba kampuni hiyo inapaswa kutoa ajira kwa wachimbaji wadogo waliopo katika eneo hilo bila upendeleo na kukemea tabia inayofanywa na viongozi wa kampuni hiyo kuwabughudhi wachimbaji wadogo wasitafute riziki katika eneo hilo.

Alimtaka Rc Mnyeti kutekeleza majukumu yake kwa haki na kumkemea kwamba asiwasumbue wachimbaji wadogo kwa kuwa anapokea rushwa kutoka kwa kampuni hiyo.

Akajibu mapigo Rc Mnyeti alisema kwamba kitendo cha yeye kusimamia maslahi ya wachimbaji wadogo kama kuwa na mikataba kimemponza lakini haki itasimama pale pale.


Mnyeti alisema kwamba ataendelea kuwabana wamiliki wa migodi mbalimbali ili waweze kuwapatia mikataba ya ajira Watumishi wao kwa kuwa ndio matakwa ya kisheria.

Naye Waziri wa madini, Dotto Biteko aliwataka viongozi hao kumaliza tofauti zao kwa kuwa kazi ya wizara yake ni kuona wachimbaji wadogo nchini wanainuka kimapato ikiwa ni pamoja na kukuza mitaji yao hususani katika uchimbaji wa madini.

Mwisho
IMG-20190728-WA0025.jpeg
IMG-20190728-WA0026.jpeg
 
Mbunge Ole Milya amtuhumu Rc Mnyeti kuhusu rushwa,ahoji ukaribu wake na kampuni ya Tz One , Rc Mnyeti Ajibu mapigo

Mwandishi Wetu,Mirerani

Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya amemtuhumu mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti kwamba anapokea rushwa ili kuwakandamiza wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite walioko eneo la Mirerani mkoani Manyara.

Ole Milya ametoa kauli hiyo Leo Julai 28 mwaka huu katika mji mdogo wa Mirerani mbele ya kamati ya kuchunguza na kutatua mipaka baina ya wachimbaji wadogo na kampuni ya Tanzanite One.

Hatahivyo, Ole Milya alienda mbali zaidi na kuhoji ukaribu baina ya kiongozi huyo wa serikali na kampuni hiyo huku akisema kwamba hatakubali kuona haki za wanyonge zinakandamizwa pindi akiwa madarakani.

"Nimwombe Mheshimiwa mkuu wa mkoa urafiki wake na Tanzanite One ufikie mwisho, usiliingize taifa hili kwenye migogoro isiyostahili "alisema Ole Milya

Alisisistiza kwamba kampuni hiyo inapaswa kutoa ajira kwa wachimbaji wadogo waliopo katika eneo hilo bila upendeleo na kukemea tabia inayofanywa na viongozi wa kampuni hiyo kuwabughudhi wachimbaji wadogo wasitafute riziki katika eneo hilo.

Alimtaka Rc Mnyeti kutekeleza majukumu yake kwa haki na kumkemea kwamba asiwasumbue wachimbaji wadogo kwa kuwa anapokea rushwa kutoka kwa kampuni hiyo.

Akajibu mapigo Rc Mnyeti alisema kwamba kitendo cha yeye kusimamia maslahi ya wachimbaji wadogo kama kuwa na mikataba kimemponza lakini haki itasimama pale pale.


Mnyeti alisema kwamba ataendelea kuwabana wamiliki wa migodi mbalimbali ili waweze kuwapatia mikataba ya ajira Watumishi wao kwa kuwa ndio matakwa ya kisheria.

Naye Waziri wa madini, Dotto Biteko aliwataka viongozi hao kumaliza tofauti zao kwa kuwa kazi ya wizara yake ni kuona wachimbaji wadogo nchini wanainuka kimapato ikiwa ni pamoja na kukuza mitaji yao hususani katika uchimbaji wa madini.

Mwisho
IMG-20190728-WA0025.jpeg
IMG-20190728-WA0026.jpeg
Barnabas%20Lugwisha%20Dar%2020190722_002035.jpeg
 
Mbunge Ole Milya amtuhumu Rc Mnyeti kuhusu rushwa,ahoji ukaribu wake na kampuni ya Tz One , Rc Mnyeti Ajibu mapigo

Mwandishi Wetu,Mirerani

Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya amemtuhumu mkuu wa mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti kwamba anapokea rushwa ili kuwakandamiza wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite walioko eneo la Mirerani mkoani Manyara.

Ole Milya ametoa kauli hiyo Leo Julai 28 mwaka huu katika mji mdogo wa Mirerani mbele ya kamati ya kuchunguza na kutatua mipaka baina ya wachimbaji wadogo na kampuni ya Tanzanite One.

Hatahivyo, Ole Milya alienda mbali zaidi na kuhoji ukaribu baina ya kiongozi huyo wa serikali na kampuni hiyo huku akisema kwamba hatakubali kuona haki za wanyonge zinakandamizwa pindi akiwa madarakani.

"Nimwombe Mheshimiwa mkuu wa mkoa urafiki wake na Tanzanite One ufikie mwisho, usiliingize taifa hili kwenye migogoro isiyostahili "alisema Ole Milya

Alisisistiza kwamba kampuni hiyo inapaswa kutoa ajira kwa wachimbaji wadogo waliopo katika eneo hilo bila upendeleo na kukemea tabia inayofanywa na viongozi wa kampuni hiyo kuwabughudhi wachimbaji wadogo wasitafute riziki katika eneo hilo.

Alimtaka Rc Mnyeti kutekeleza majukumu yake kwa haki na kumkemea kwamba asiwasumbue wachimbaji wadogo kwa kuwa anapokea rushwa kutoka kwa kampuni hiyo.

Akajibu mapigo Rc Mnyeti alisema kwamba kitendo cha yeye kusimamia maslahi ya wachimbaji wadogo kama kuwa na mikataba kimemponza lakini haki itasimama pale pale.


Mnyeti alisema kwamba ataendelea kuwabana wamiliki wa migodi mbalimbali ili waweze kuwapatia mikataba ya ajira Watumishi wao kwa kuwa ndio matakwa ya kisheria.

Naye Waziri wa madini, Dotto Biteko aliwataka viongozi hao kumaliza tofauti zao kwa kuwa kazi ya wizara yake ni kuona wachimbaji wadogo nchini wanainuka kimapato ikiwa ni pamoja na kukuza mitaji yao hususani katika uchimbaji wa madini.

Mwisho View attachment 1165700View attachment 1165701View attachment 1165702
wanaendelea kulana wao kwa wao.

karma is a freaking bitch!
 
Tutajua tu zile za uchumi wa dharula kujenga hadi uwanja wa mpira kwa short term plan, usio wa kibiashara. Pia sina hakika lile fungu la ununuzi binadamu waheshimiwa lilikua na mkaguzi.
 
Msamiati wa uitwao Rushwa haumuhusu kiongozi aitwaye Mnyeti, Lugora na Ole Sabaya. Hivyo usitegemee unavyotamka Hilo neno wanaelewa Kama mtu mwenye Akili timamu anavyoelewa. Umeona anavyojibu Mnyeti kwamba kula rushwa kwake ndio kuwasaidia wachimbaji wadogo wawe na mikataba 😂😂😂😂
 
Hii ni video inayomwonyesha Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya akihoji ukaribu wa Mkuu wa mkoa wa Manyara na kampuni ya Tanzanite One iliyoko Manyara.
 
Hii ni video inayomwonyesha Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoani Manyara, James Ole Milya akihoji ukaribu wa Mkuu wa mkoa wa Manyara na kampuni ya Tanzanite One iliyoko Manyara. View attachment 1165730
Ni mwendo wa clip tu.

Huyu Ole mililya bado ana chembrchembe za upinzani watamshughlikia kama hajui.

Kumpinga Mnyeti ni kuhujumu Urais wa Magufuli kwa mujibu wa Wapiga vigelegele
 
Huyo Mnyeti MaCCM walimshangilia sana na akapindishwa cheo na kuwa RC baada ya kurekodiwa akitenda kosa la kutoa rushwa kwa madiwani wa upinzani,
sasa leo kale katabia cha rushwa kalichompandisha cheo anakaendeleza kwa Tz One haya WanaCCM endeleeni kumshangilia.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom