Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,890
- 939
MBUNGE NICODEMUS MAGANGA AITAKA SERIKALI KUWA NA MFUMO MZURI WA KUWATAMBUA WASTAAFU
Mbunge wa Mbogwe (CCM), Nicodemus Maganga amehoji Serikali kuwapiga chenga wastaafu pindi wanapoanza kudai mafao yao.
Akiuliza swali la msingi, Maganga amehoji Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha pesheni za wastaafu zinalipwa kwa wakati?.
Akijibu swali hilo Ijumaa Mei 26, 2023 Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi amesema kuwa mifuko inaendelea kuimarisha namna ya ulipaji wa mafao ili kuhakikisha maombi ya wastaafu wapya yanafanyiwa kazi kwa haraka.