Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,353
- 14,630
Mbunge Nicodemas Maganga wakati anachangia mpango wa taifa bungeni amewaonya mawaziri kuwa waache kuwa na mipango mingi isiyotekelezeka na sasa hivi wamemwachia rais Samia acheze peke yake na kila anapotoa pasi wanakutwa wamezubaa.
Mh Maganga ametolea mfano serikali iliwahakikishia wananchi kuwa vijiji vyote 2000 vilivyobaki vingekuwa vimepata umeme wa REA mpaka mwisho wa mwaka 2021 lakini mpaka sasa hakuna kinachofanyika zaidi ya kushuhudia makandarasi wa kichina wakipiga sarakasi za hapa na pale site!!.
Pia amesema tangu fedha za COVID 19 zifike majimboni hakuna kinachofanyika zaidi ya kushuhudia mabishano ya taratibu za manunuzi na kushuhudia upandaji wa bei wa kutisha wa vifaa vya ujenzi kwa sasa!.
Mh Maganga ametolea mfano serikali iliwahakikishia wananchi kuwa vijiji vyote 2000 vilivyobaki vingekuwa vimepata umeme wa REA mpaka mwisho wa mwaka 2021 lakini mpaka sasa hakuna kinachofanyika zaidi ya kushuhudia makandarasi wa kichina wakipiga sarakasi za hapa na pale site!!.
Pia amesema tangu fedha za COVID 19 zifike majimboni hakuna kinachofanyika zaidi ya kushuhudia mabishano ya taratibu za manunuzi na kushuhudia upandaji wa bei wa kutisha wa vifaa vya ujenzi kwa sasa!.