Mbunge na Mwanamuziki, MwanaFA apinga sheria mpya ya BASATA ya kutaka kusikiliza nyimbo kabla ya Msanii kuipeleka redioni. Asema ni ya ‘kidwanzi’

Haya mambo yapo Tanzania tu mamaqe. Hivi aliyeturoga nani? Kabisaaaa eti ukitoa wimbo peleka BASATA!! Hahahahah mbona tumerudi kwenye Ujima na Ujamaa.
Kiongozi,ukiacha Pm,( ambayo haipatikani) njia gani nyingine naweza kukufikia.ahsante
 
MKIACHA MATUSI KWENYE MZIKI WENU Mtapungukiwa nini?

BaSATA nanyie hamtaki mistari ya kuwakosoa na serikali... Kwani nyie Mungu?
 
Mkuu tafadhali,umeielewa vyema hiyo post?
Mkuu tafadhali,umeielewa vyema hiyo post?
Mkuu nimeilewa sana, kwa muda mrefu serikali imekuwa ikitumia njia rafiki kuwashauri hawa wasanii wazingatie maadili kwenye kazi zao lakini wameshindwa. Sasa serikali imeamua iongeze mbinyo wa kisheria ambapo tangu may mosi mwaka huu utekelezaji wa sheria hii umeanza. Huyu msanii amekuwa akiimba nyimbo za matusi "refer wimbo wake wa mwanaume suruali" alioimba na Vanessa mdee. Analalamika kitu gani zaidi ya kulilia kuimba matusi.
 
Kwanini asiyaongelee bungeni?
Me nahisi wakati mwngine mbinu ya kusolve tatizo ni kuliwahi likiwa la moto. Kuongea bungeni ni rotation wako wabunge wengi so mpaka aje aongee ni unakuta muda umesogea. Kuanza kuandika mtandaoni nahisi ni hatua ya kwanza. pia naona kaongea hasahasa kutokana na msukumo uliotokana na nyimbo ya ney. Me naona kafanya vizuri na asiishie hapa aende akaliongelee bungeni.
 
Huu ni mwanya wa rushwa kwa watumishi wa BASATA, utoe hongo ndio nyimbo ipewe go ahead
Na hii iko hivyo hivyo katika taasisi na ofisi nyingi za serikali, hawana namna ya kujiendesha wamejazana ofisi cha maana wanachofanya hakuna na wanataka wajiendeshe kwa nguvu za wananchi kwa kulazimisha urasimu. Kuna taasisi nyingi sana za serikali zinazofanya kazi inayofanana, au taasisi kubwa ila inafanya kazi "ndogo" ambayo ingeweza kupelekwa kwenye taasisi nyingine iwe idara.
 
Mbunge wa Muheza, Hamis Mwinjuma ambaye pia ni mwanamuziki maarufu wa Bongofleva ‘MwanaFA’ ameipinga vikali sheria mpya iliyowekwa na BASATA. Sheria hiyo inamtaka msanii kupeleka kwanza nyimbo BASATA ikasikilizwe kabla ya kuipeleka kupigwa redioni.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika:


“Naomba niandike kuhusu hili la huu utaratibu mpya wa BASATA. Binafsi sikubaliani nalo na ntalipinga kwa nguvu nyingi. Sidhani kama Sheria hii inafaa hata kuwepo achia mbali kutumika. HAINA TIJA YEYOTE, HAIMSAIDII MSANII KWA NAMNA YEYOTE. Ni ya kidwanzi. Inatakiwa kurekebishwa kama sio kuondolewa kabisa.

Tutafute namna nyingine za ku’censor sanaa matusi yasisikike kwa kadri inavyowezekana na sio kwa utaratibu huu dhaifu na wa kikandamizaji. Siungi mkono nyimbo “chafu” lakini kutengeneza urasimu usio na msingi kwa kisingizio cha kuwepo kwa nyimbo zisizofaa ni jaribio la kuzorotesha tu sanaa.

Kama BASATA na COSOTA wanataka kutekeleza KILA Sheria inayowahusu wangeanza na Sheria namba 7 ya mwaka 1999 inayowapa Cosota haki ya kutoa leseni kwa maeneo ya hadhara yanayotumia kazi za sanaa, kukusanya MIRABAHA toka maeneo/leseni hizo na kuwalipa wasanii makusanyo hayo.

HIZI NDIO SHERIA ZITAKAZOMSAIDIA MSANII NA WAMEZIFUMBIA MACHO KWA MIAKA MINGI, wasanii wanaendelea kupoteza hela zao NYINGI stahiki na mnawaletea sheria zisizo na kichwa wala miguu kuja kuwakandamiza. BASATA kama mlezi wa wasanii lilitakiwa kusimama kidete mpaka hili la MIRABAHA lifanikiwe.

Bahati nzuri tuna Waziri na Katibu Mkuu wasikivu, tutalisemea kwa namna nyingi hili na tunaamini kero hii itaondolewa haraka.

Msifanye kutoa wimbo iwe kama kuomba passport au VIZA, mnaonea wasanii,tunakwamisha sanaa.

Kwa heshima nyingi nawaambia Basata, mambo ya namna hii ndio haswa yanayotupa kazi kubwa kuwaelezea wapenzi wa kawaida wa sanaa kuwa Baraza hili lina kazi nyingine zaidi ya kufungia na kufungulia tu nyimbo na wasanii.

Na kuweka kumbukumbu sawa, jambo liliwahi kuja kwa majadiliano kwenye Bodi ya Basata wakati nikiwa nahudumu kama MJUMBE wa Bodi,NA NILILIPINGA SANA kwa wakati ule kama nnavyoendelea kulipinga sasa.

Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”
Wangesema tu mtu apeleke shairi lake au tungo yake kabla ya kuanza kurecord na asahihishwe kama inabidi harafu akabithiwe kwenda kurecord

Lkn hii amesharecord ndo alete hahahaha wataua vipaji sana

Lkn pia wanapaswa kusimamia maadili ya kitanzania kwa nguvu zote
 
Sheria ni ya kijinga, inatengeneza mazingira ya rushwa hapo BASATA, inaua ubunifu, inaua sanaa.

Tulishatoa namna nzuri ya wao kuchuja maudhui ila wamekaza mafuvu.
 
Back
Top Bottom