Mbunge na diwani CHADEMA, walalamikiwa na wananchi kwa kukwamisha maendeleo kwa miaka 4

Ndakilawe Lissu alisimamia haki, aliwaeleza wabunge haoni sababu ya wananchi wake kuchangishwa pesa za ujenzi wa madarasa iwapo kila mwaka hela iliyotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo inarudishwa hazina kana kwamba kazi za kufanya hazipo. Huo ni uzembe mkubwa na hakuna sababu ya kuwaongezea wananchi mzigo wakati hela inarudishwa na kuliwa na wachache. Ipelekwe kwa wananchi ijenge shule, zahanati barabara na kununua madawa, madawati na kadhalika.
Mbunge makini huwajali watu wake na si kuwabebesha mizigo watu wake wakati kuna njia ya kuwapunguzia mizigo.
Hakuna michango isiyo na ulazima iwapo kila mmoja atatimiza wajibu wake ipasavyo. Unadhani serikali inashindwa kujenga shule? Lakini pia hali ni mbaya zaidi kwa yale majimbo tiifu kwa CCM. Watu wakiamua kukuletea picha za shule, zahanati, barabara na jinsi wananchi wanavyopata shida utashangaa kama hii ni tanzania ambayo wabunge wake wanaunga mkono hoja 100%. Miaka zaidi ya 50 watu mmnaunga mkono hoja!!!!!!! Lakini jambo la kujiuliza je watoto wao wanasoma katika shule hizo.
Kama umechomwa na mwiba na umevunjikia mguuni, huna sababu ya kunywa panadol ili kupunguza maumivu. Suluhisho kukabiliana na maumivu na kuutoa mwiba mguuni. Lissu anawaambia wananchi wake hakuna sababu ya kujiadhibu eti mnachangia shule wakati pesa za kufanya hivyo kila mwaka zinarudishwa hazina kana kwamba hakuna vitu vya kufanya, ni kuieleza serikali ijenge shule maana yenyewe ndo inakusanya kodi toka kwa hao wananchi. Wananchi waachwe wafikirie kuleta maendeleo yao na huku serikali ikitimiza wajibu wake. Wangechangia iwapo kweli serikali imeshindwa na haina jinsi ya kufanya hivyo. Hata wananchi hilo wamgeliona na wangejihamasisha bila kuhamasishwa.
 
Last edited by a moderator:
Kama mnataka Tundu Lissu alipaishe jimbo mpeni na UWEZO wa kukusanya KODI!Mtuachie KODI na sisi MUONE KAZI.
 
Tunawaonea wabunge bure kabisa,wanaotakiwa kuulizwa maswali haya ni wale wanaokusanya kodi na kupanga mipango ya maendeleo,kama pesa zinaishia kwenye mifuko ya wajanja wachache,kwanini walaumiwe wabunge?Hapa haijalishi mbunge wa chama tawala au upinzani.
 
kwa sasa mmemwancha DR.Slaa na Mbowe sasa adui yenu mpya ni Lissu baada ya kuwaambia ukweli !! Kweli Lumumba inaporomoka!!
 
Hivi mnadhani Lisu ni mtu wa maana kwenye hii nchi hana kitu ni mtu fulani mleta shida na kelele tu.

watu wengine wana ubongo wa kuku, hivi hajui kuwa ccm wameitawala nchi hii kwa miaka mingapi na shule za dizaini hiyo zipo ngapi tz? kote huko anaongoza lissu?
 
Hapa napata tabu kwa hiyo kabla ya hiyo miaka 4 maendeleo yalikuwepo au baada ya Tundu lissu ndio yakasimama?ila swali lingine kwani shule za dizaini hii zipo tuu kwa Tindu Lissu au kwa mwigulu,Sita,Chalinze wao madarasa yana Tiles Kabisa?
 
Nilishtushwa sana na kauli ya mwenyekiti wa halmashauri ya Singida kuwa mbunge wa Singida mashariki anazuia wananchi kujitolea shughuli za maendeleo.

Akiwa kwenye mkutano wa hadhara wa katibu mkuu wa "chama dume" CCM mwenyekiti huyo aliongea kauli hiyo akihutubia umati wa watu huku katibu wa CCM mkoa wa Singida akipigia chapuo kuwa mbunge huyo hatoshi.

Cha ajabu wazungumzaji wote waliomtaja mbunge huyo wa Singida mashariki hawakumtaja kwa jina, kuanzia mwenyekiti wa halmashauri, katibu wa CCM mkoa, Nnauye hata mzee Kinana.

Kweli siasa za CCM ndo zimeishia wapi? kumkejeli "mbunge wa taifa" mh. Lissu?

Kutoa visingizio vya kushindwa kwenu na "kaserikali corrupt na weak" na kumpakazia mbunge kwa kuwa tu ni wa upinzani na mwiba kwenu?

Kwa hili nimewadharau, kamuulizeni "vasco da gama" kwa nini hotuba zake za kisiasa siku hizi jina la Lissu lazima liwepo?

Ulizeni vicha vitunguu kama Werema, watakuambia jamaa alivyo safi.

Kuwa CCM rahaaaaaaa, maana hutumii akili, mdomo tu tosha.
 
8Pjk6roF7VMesAAAAASUVORK5CYII=
 
Hivi mnadhani Lisu ni mtu wa maana kwenye hii nchi hana kitu ni mtu fulani mleta shida na kelele tu.

jamaa anawatesa sana, ivi kuna jina baya ambalo hamjamuita kweli? pointi aliyosema Lissu ni kuwa kila mwaka pesa mkoani singida inarudishwa hazina kwa kukosa matumizi, alitoa mpaka takwimu, je wananchi wanachangiaje wakati kila mwaka serikali inarudishiwa chenji kuwa imekosa matumizi? ingefaa mtoe majibu kwa uyo mtu mliyemuita majina yote duniani!!
 
Tunawaonea wabunge bure kabisa,wanaotakiwa kuulizwa maswali haya ni wale wanaokusanya kodi na kupanga mipango ya maendeleo,kama pesa zinaishia kwenye mifuko ya wajanja wachache,kwanini walaumiwe wabunge?Hapa haijalishi mbunge wa chama tawala au upinzani.

Kama walijua kuwepo kwao bungeni hakuleti tofauti kwanini wanagombania?
 
Lakini tuwe fair kidogo matatizo hayo yapo kwenye kila jimbo Tanzania hata kwa Pinda ukienda utayakuta.
 
Back
Top Bottom