Hakuna mtu muelewa na mpenda haki asiyetambua kwamba Serikali imefanya ukatili wa Hali ya juu kwa kitendo cha kuondoa fao la kujitoa katika mifuko ya hifadhi ya jamii.
Ipo idadi kubwa sana ya Watanzania ambao wameajiriwa katika sekta binafsi, na kama tunavyofahamu, mara nyingi sekta binafsi hazina mikataba ya kudumu kama ilivyo kwa Serikali, hivyo basi mtu anaweza kufanya kazi miezi kadhaa, mwaka, miaka kadhaa na mkataba wake ukafika kikomo.
Lakini kwa sheria mpya ya fao la kujitoa, mtu huyo huyo mkataba wake ukimalizika hataweza kupata pesa yake yote ya pensheni bali sheria inamlazimisha asubiri kufikisha umri wa miaka 60 hata kama mkataba umeisha akiwa na miaka 20 au 30😀😀😀 (what a joke)
Tunatambua kwamba lengo la Serikali ni kupora pesa hizi ili zitumike kwenye miradi ya Serikali.
Huu ni unyanyasaji mkubwa. Sheria kandamizi kama hii zinapaswa kufutiliwa mbali na wapenda haki wote bila kujali itikadi za kisiasa.
Wabunge wengi pamoja na kwamba wengi wao wana umri mkubwa hii sheria ingekuwa inawahusu kwenye mafao yao, sidhani kama wangekubaliana na upuuzi huu.
Ifike hatua wabunge mpiganie kile mnachokiamini huku mkiacha unafiki pembeni, na hapa ndipo nitakapomuona Mbunge mzalendo na mwenye nia ya dhati.
Ipo idadi kubwa sana ya Watanzania ambao wameajiriwa katika sekta binafsi, na kama tunavyofahamu, mara nyingi sekta binafsi hazina mikataba ya kudumu kama ilivyo kwa Serikali, hivyo basi mtu anaweza kufanya kazi miezi kadhaa, mwaka, miaka kadhaa na mkataba wake ukafika kikomo.
Lakini kwa sheria mpya ya fao la kujitoa, mtu huyo huyo mkataba wake ukimalizika hataweza kupata pesa yake yote ya pensheni bali sheria inamlazimisha asubiri kufikisha umri wa miaka 60 hata kama mkataba umeisha akiwa na miaka 20 au 30😀😀😀 (what a joke)
Tunatambua kwamba lengo la Serikali ni kupora pesa hizi ili zitumike kwenye miradi ya Serikali.
Huu ni unyanyasaji mkubwa. Sheria kandamizi kama hii zinapaswa kufutiliwa mbali na wapenda haki wote bila kujali itikadi za kisiasa.
Wabunge wengi pamoja na kwamba wengi wao wana umri mkubwa hii sheria ingekuwa inawahusu kwenye mafao yao, sidhani kama wangekubaliana na upuuzi huu.
Ifike hatua wabunge mpiganie kile mnachokiamini huku mkiacha unafiki pembeni, na hapa ndipo nitakapomuona Mbunge mzalendo na mwenye nia ya dhati.