Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,441
- 7,778
Mheshimiwa spika, nitalisema kwa upole sana suala la machinga maana nikizungumza kwa ukali nitasemwa mimi sio mtanzania lakini nilivyolisea mwanzo nahisi watu hamkunielewa. Niliposema niliambiwa mimi ni mrundi sio Mtanzania.
Mimi natoka vijijini na ni mkulima wa mpunga, gunia la mpunga ndani ya mwezi mmoja limeshafika elfu 90 na wiki mbili tatu tulikuwa tunauza elfu 40/50, mchele umepanda hapahapa ndani kwetu.
Nimefanya karesearch kulingana na akili yangu, walazi wa mchele wameongezeka, wauza viazi vya chips wanalia vimeoza hamna walaji. Tulizoea manaansi wananunu machinga wanakatakata wanawauzia watu 200 linanunulika, sasa hivi hayanunuliki.
Watu wamerudi kwenye wali, tunakula unabakiza na kiporo cha chai. Mtoto anatoka Mbagala anasoma shule ya Uhuru, unampa kaelfu anakula kachips kake kwenye nailoni.
Sasa hivi wamachinga wote wamefurumushwa mnataka watu wote wakale kwenye restaurant, mimi nilielewa kabisa Rais alivyosema tukawaandalie mazingira mazuri.
Nina duka Kkoo siku ya 7 sijauza, fikiria mfanyakazi nilikuwa nampa posho ya chakula 3000 leo anatakiwa akale restaurant chai 2000, mchana 5000 nitatoa wapi? Kila anayefungua duka ana mfuko una hotpot, Watu wanakuja na makande na wali wa kiporo, haiwezekani kuhudumia kwasababu hatuuzi.
Waziri wa fedha jaribu kuliangalia na bahati nzuri umenitaja maana wewe ni waziri wa fedha inawezekana una takwimu vizuri kwamba mimi ni tajiri, mimi ni zao la machinga, machinga wapo aina tofauti, kuna machinga anashinda mlangoni kupiga debe anakaribisha anapata 2000, usifikiri watu wote wana mitaji na hao wenye mitaji ndio wanawezesha machinga, huwezi kutenganisha, ukiwatoa machinga Congo biashara imekufa.
Mbunge Musukuma
Pia Musukuma ameongelea ukamilishaji wa miradi kwani miradi ipo mingi ambayo huwa haifikishi mwisho akitolea mifano kwenye majengo kwenye halmashauri akitolea mfano vituo vya afya vilivyoishia kati huku wanaanzisha ujenzi wa vingine.
Mimi natoka vijijini na ni mkulima wa mpunga, gunia la mpunga ndani ya mwezi mmoja limeshafika elfu 90 na wiki mbili tatu tulikuwa tunauza elfu 40/50, mchele umepanda hapahapa ndani kwetu.
Nimefanya karesearch kulingana na akili yangu, walazi wa mchele wameongezeka, wauza viazi vya chips wanalia vimeoza hamna walaji. Tulizoea manaansi wananunu machinga wanakatakata wanawauzia watu 200 linanunulika, sasa hivi hayanunuliki.
Watu wamerudi kwenye wali, tunakula unabakiza na kiporo cha chai. Mtoto anatoka Mbagala anasoma shule ya Uhuru, unampa kaelfu anakula kachips kake kwenye nailoni.
Sasa hivi wamachinga wote wamefurumushwa mnataka watu wote wakale kwenye restaurant, mimi nilielewa kabisa Rais alivyosema tukawaandalie mazingira mazuri.
Nina duka Kkoo siku ya 7 sijauza, fikiria mfanyakazi nilikuwa nampa posho ya chakula 3000 leo anatakiwa akale restaurant chai 2000, mchana 5000 nitatoa wapi? Kila anayefungua duka ana mfuko una hotpot, Watu wanakuja na makande na wali wa kiporo, haiwezekani kuhudumia kwasababu hatuuzi.
Waziri wa fedha jaribu kuliangalia na bahati nzuri umenitaja maana wewe ni waziri wa fedha inawezekana una takwimu vizuri kwamba mimi ni tajiri, mimi ni zao la machinga, machinga wapo aina tofauti, kuna machinga anashinda mlangoni kupiga debe anakaribisha anapata 2000, usifikiri watu wote wana mitaji na hao wenye mitaji ndio wanawezesha machinga, huwezi kutenganisha, ukiwatoa machinga Congo biashara imekufa.
Mbunge Musukuma
Pia Musukuma ameongelea ukamilishaji wa miradi kwani miradi ipo mingi ambayo huwa haifikishi mwisho akitolea mifano kwenye majengo kwenye halmashauri akitolea mfano vituo vya afya vilivyoishia kati huku wanaanzisha ujenzi wa vingine.