MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,734
Ni kweli nakubali kuwa kusoma ( kuelimika ) sana siyo Kutusua ( Kufanikiwa ) Kimaisha kwani kama ingekuwa hivyo basi Mimi Generalist nisingekuwa na Maisha haya Duni ( ya Dhiki ) niliyonayo sasa kwa Elimu yangu hii ya haka ' tudigrii ' kangu Kamoja tu ninakokamiliki huu mwaka wa 12 sasa.
Lakini pia haimaanishi kuwa basi kwakuwa hukubahatika kuwa na Elimu za Wastani ( Degree ) aliyonayo Generalist, ya Kati ( Masters ) aliyonayo Sky Eclat na Mmawia na ya Juu kabisa ( Doctorate ) aliyonayo Mtani wangu Mwigulu Nchemba basi kila mara Uwadhihaki waliyobahatika kuwa nayo.
Generalist naheshimu sana Michango ya Mbunge wa Geita Msukuma na huwa ninavutiwa ( napenda ) mno Ujengaji wake wa Hoja hasa juu ya Masuala ( Issues ) ya Mambo Mtambuka ( Current Affairs ) yanayoendelea nchini.
Ila sijapendezwa na Kitendo cha Mbunge huyu Msukuma cha kutaka Kutumia Elimu yake haba ( ya Darasa la Saba ) kama Tiketi ya Kuwadharau wenye Elimu Kubwa ( Wanataaluma ) hapa nchini Tanzania na kama Kichaka chake cha Kuuficha Udhaifu wake kama Mbunge na Maendeleo Haba ya Jimboni Kwake.
Vile vile Generalist pia sipendi Vitendo vya Wasomi ( Intellectuals ) hapa Tanzania cha Kujiona na Kuwadharau wale wasiosoma sana kama Wao kwani Jukumu lao kubwa siyo Kuwadharau bali ni Kuwaelimisha na Kuwasaidia katika Kufikiri ili basi mwisho wa Siku Mawazo yao yote ( Fikra zao zote ) yawe ( ziwe ) na Tija kwa Maendeleo Mtambuka ya Taifa la Tanzania na Watanzania kwa ujumla.
Nimshauri tu Mbunge wa Geita Msukuma kuwa huu muda anaoutumia kila Siku Kuchukizwa na Kuwananga vibaya Wasomi wa Tanzania ( hasa Wanasiasa na Wabunge ) Wenzake angeutumia katika Kujielimisha zaidi kwa kwenda Shule na ikibidi nae afike hadi Chuo Kikuu ili basi baadae nae abadilike Kifikra na Kimtazamo ajue kuwa kumbe huenda haya Makelele yake na Chuki zake kwa wenye Elimu Kubwa ( Wasomi ) ni Matokeo ya kutopata Elimu Kubwa ambayo inasaidia kumfanya Msomi kuwaza Makubwa zaidi.
Msukuma akasome bado muda anao tu.
Lakini pia haimaanishi kuwa basi kwakuwa hukubahatika kuwa na Elimu za Wastani ( Degree ) aliyonayo Generalist, ya Kati ( Masters ) aliyonayo Sky Eclat na Mmawia na ya Juu kabisa ( Doctorate ) aliyonayo Mtani wangu Mwigulu Nchemba basi kila mara Uwadhihaki waliyobahatika kuwa nayo.
Generalist naheshimu sana Michango ya Mbunge wa Geita Msukuma na huwa ninavutiwa ( napenda ) mno Ujengaji wake wa Hoja hasa juu ya Masuala ( Issues ) ya Mambo Mtambuka ( Current Affairs ) yanayoendelea nchini.
Ila sijapendezwa na Kitendo cha Mbunge huyu Msukuma cha kutaka Kutumia Elimu yake haba ( ya Darasa la Saba ) kama Tiketi ya Kuwadharau wenye Elimu Kubwa ( Wanataaluma ) hapa nchini Tanzania na kama Kichaka chake cha Kuuficha Udhaifu wake kama Mbunge na Maendeleo Haba ya Jimboni Kwake.
Vile vile Generalist pia sipendi Vitendo vya Wasomi ( Intellectuals ) hapa Tanzania cha Kujiona na Kuwadharau wale wasiosoma sana kama Wao kwani Jukumu lao kubwa siyo Kuwadharau bali ni Kuwaelimisha na Kuwasaidia katika Kufikiri ili basi mwisho wa Siku Mawazo yao yote ( Fikra zao zote ) yawe ( ziwe ) na Tija kwa Maendeleo Mtambuka ya Taifa la Tanzania na Watanzania kwa ujumla.
Nimshauri tu Mbunge wa Geita Msukuma kuwa huu muda anaoutumia kila Siku Kuchukizwa na Kuwananga vibaya Wasomi wa Tanzania ( hasa Wanasiasa na Wabunge ) Wenzake angeutumia katika Kujielimisha zaidi kwa kwenda Shule na ikibidi nae afike hadi Chuo Kikuu ili basi baadae nae abadilike Kifikra na Kimtazamo ajue kuwa kumbe huenda haya Makelele yake na Chuki zake kwa wenye Elimu Kubwa ( Wasomi ) ni Matokeo ya kutopata Elimu Kubwa ambayo inasaidia kumfanya Msomi kuwaza Makubwa zaidi.
Msukuma akasome bado muda anao tu.