Mbunge Msigwa wasaidie wafanyabiashara wa nyanya wa Ilula wanasema ni heri kujinyonga!!

tramadol

JF-Expert Member
Oct 10, 2015
5,383
4,317
Nimewasikia wafanyabiashara wa nyanya wa Ilula wanalalamika kuwa biashara ya nyanya imekuwa ngumu na heri hata kujinyonga kuliko Kuna nyanya zinaharibika.

Mbunge Mch Msigwa wasaidie hao wafanyabiashara ili biashara hiyo iwape mafanikio kama zamani.
 
Msigwa 2.jpg
Mbunge Mch Msigwa
 
Nyanya nyingi zinaharibika tu nadhani tukipata wazo la kuanzisha Hata usindikaji wa nyanya za kopo na Hata mambo ya tomato sauce muhimu kwa bidhaa hiyo.
 
msigwa anahusikaje kwenye jimbo lisilo lake?kwani mbunge wa huko kazi yake nini?
nonsense!
 
msigwa anahusikaje kwenye jimbo lisilo lake?kwani mbunge wa huko kazi yake nini?
nonsense!
mbunge wa kilolo ndo jukumu lake ya msigwa ni kihesa,ir mjini, mlandege,kihesa kilolo,kibwabwa na kitwiru+zizi la ngombe
 
msigwa anahusikaje kwenye jimbo lisilo lake?kwani mbunge wa huko kazi yake nini?
nonsense!
Wanaweza kuwa msaada mkubwa kwa wana Iringa wote huwa Kuna umoja wa wabunge ktk mkoa husika na kwa Iringa Msingwa very Potential
 
mbunge wa kilolo ndo jukumu lake ya msigwa ni kihesa,ir mjini, mlandege,kihesa kilolo,kibwabwa na kitwiru+zizi la ngombe
Anaweza kusaidia kutoa wazo kwa wana Ilula Kuna watu Mungu amewapa kipaji cha ushawishi
 
Anaweza kusaidia kutoa wazo kwa wana Ilula Kuna watu Mungu amewapa kipaji cha ushawishi
lakin niliona kiwanda kipya cha kusindika nyanya maeneo ya mseke ama awajaanza uzalishaj nafikili ni tawi lao maana wakingine Arusha
 
Hapo ilula tokea siku nyingi sana wanasema kutaanzishwa kiwanda cha kusindika nyanya lakini hola. Serikali imekuwa ikipiga danadana. Wabunge wake wenyewe Akina Msolla kapita hajafanya chcohote, na mwenzake Mwamoto Hakuna anachokifanya
 
Msigwa ni IRINGA mjini na Mwamoto Kilolo ndio yote na ILULA,Ila usi kariri Nyanya zina limwa ILULA tu kwa Iringa Bro.
 
Soko la nyanya kuwa hivyo ni kawaida ingawa sasa limezidi, mwezi wa 4 kurudi nyuma nyanya ilikuwa na bei kubwa mno waliolima walitajirika, hii iliotokana na mvua Dec hazikuwa nzuri.
 
Mkuu wa mkoa aweke askari hapo kila gari lisimame kwa dakika 3 watu dar tunahitaji nyanya hatupati kwa bei nzuri.
Basi zote zisimame abiria wanunue.
Kila roli linunue matenga mawili
 
Mkuu wa mkoa aweke askari hapo kila gari lisimame kwa dakika 3 watu dar tunahitaji nyanya hatupati kwa bei nzuri.
Basi zote zisimame abiria wanunue.
Kila roli linunue matenga mawili
Kwa kawaida kwenye biashara kuna suala la demand and supply na kwa staili yetu ya kuigana kwa hivi sasa soko limejaa [glut] kuliko mahitaji. Suluhisho zuri ni kuwa na viwanda vidogo vya kusindika nyanya ili ziweze kukaa muda mrefu sokoni.
Mbunge kwa hili mtamuonea tuu.
 
Back
Top Bottom