Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mbunge wa Simanjiro, na kada wa chama cha Mapinduzi ccm,James ole Milly amewataka viongozi wasitaafu serikalini na Chama kuacha kuingilia na kukosoa jitihada zinazofanywa na serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi badala yake waunge mkono jitihada hizo zinazofanywa na rais John Magufuli katika kuliletea maendeleo taifa.
Milly ametoa Kauli hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Arusha, kufuatia kuibuka kwa baadhi ya viongozi wasitaafu nchini kuanza kukosoa na kubeza jitihada zinazofanywa na Rais Magufuli ambaye ameonyesha uzalendo mkubwa katika kulitumikia taifa na wananchi wake.
Mbunge huyo amewataja baadhi ya wasitaafu wa CCM Mzee Yusuf Makamba na Mzee Abdulrahman Kinana ambao hivi karibuni waliibuka na kuandika waraka wakitumia kivuli cha chama cha Mapinduzi alidai viongozi hao wastaafu hawana mamlaka ya kufanya hivyo.
Alisema wasitaafu hao Mzee Makamba na Kinana hawana uhalali wowotte wa kukosoa na kuhoji mwelekeo wa ccm na serikali yake.
"Ukisoma kwa kina taarifa ya viongozi hawa wasitaafu wa CCM utagundua kuwa walikuwa na nia ovu ya kuhujumu na kutokuwa na imani na uongozi wa rais Magufuli" Alisema Milly
Amesema taarifa hiyo ni Kuendeleza siasa za kudhalilisha na kuponda juhudi za mabadiliko chanya ya kisiasa ,Kijamii,kiuchumi na kiusalama yaliyoanzishwa na mwenyekiti wa CCM ,Rais Magufuli.
Milly alisema pamoja na kutounga Mkono kauli mbalimbali zinazoibuliwa na wanaharakati ,ila aliwataka Makamba na Kinana iwapo wanabaini shutuma zinazoelekezwa kwao si za msingi ,kukimbilia mahakamani na si kutumia kivuli cha CCM kufidha madhambi yao.
Aliwataka wananchi kuepuka kauli za kichochezi zinazoenezwa na wasitaafu hao kwa kuwa zinalenga kuigawa CCM na serikali yake na kuwataka wananchi wamuunge mkono rais Magufuli kwa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR),mradi wa Umeme wa maji ya mto Rufiji (Stickers Gorge ,Ununuzi wa ndege 8 na ufufuaji wa shirika la Ndege nchini (ATCL).
Aliwataka viongozi wasitaafu kumwacha huru rais Magufuli ili atekeleze ahadi alizozitoa kwa wananchi na kuepuka kumwingiza kwenye misukosuko na migogoro ya kisiasa .
Milly ametoa Kauli hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Arusha, kufuatia kuibuka kwa baadhi ya viongozi wasitaafu nchini kuanza kukosoa na kubeza jitihada zinazofanywa na Rais Magufuli ambaye ameonyesha uzalendo mkubwa katika kulitumikia taifa na wananchi wake.
Mbunge huyo amewataja baadhi ya wasitaafu wa CCM Mzee Yusuf Makamba na Mzee Abdulrahman Kinana ambao hivi karibuni waliibuka na kuandika waraka wakitumia kivuli cha chama cha Mapinduzi alidai viongozi hao wastaafu hawana mamlaka ya kufanya hivyo.
Alisema wasitaafu hao Mzee Makamba na Kinana hawana uhalali wowotte wa kukosoa na kuhoji mwelekeo wa ccm na serikali yake.
"Ukisoma kwa kina taarifa ya viongozi hawa wasitaafu wa CCM utagundua kuwa walikuwa na nia ovu ya kuhujumu na kutokuwa na imani na uongozi wa rais Magufuli" Alisema Milly
Amesema taarifa hiyo ni Kuendeleza siasa za kudhalilisha na kuponda juhudi za mabadiliko chanya ya kisiasa ,Kijamii,kiuchumi na kiusalama yaliyoanzishwa na mwenyekiti wa CCM ,Rais Magufuli.
Milly alisema pamoja na kutounga Mkono kauli mbalimbali zinazoibuliwa na wanaharakati ,ila aliwataka Makamba na Kinana iwapo wanabaini shutuma zinazoelekezwa kwao si za msingi ,kukimbilia mahakamani na si kutumia kivuli cha CCM kufidha madhambi yao.
Aliwataka wananchi kuepuka kauli za kichochezi zinazoenezwa na wasitaafu hao kwa kuwa zinalenga kuigawa CCM na serikali yake na kuwataka wananchi wamuunge mkono rais Magufuli kwa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR),mradi wa Umeme wa maji ya mto Rufiji (Stickers Gorge ,Ununuzi wa ndege 8 na ufufuaji wa shirika la Ndege nchini (ATCL).
Aliwataka viongozi wasitaafu kumwacha huru rais Magufuli ili atekeleze ahadi alizozitoa kwa wananchi na kuepuka kumwingiza kwenye misukosuko na migogoro ya kisiasa .