Mbunge Jerry Silaa hajui kitu kuhusu ATCL, asijifanye mjuaji

Wasalaam wapenzi wa jukwaa hili!

Ndugu zangu huwa napata ukakasi sana ninapoona mtu ambaye anaonekana anajiita msomi lakini anyoongea hayana reflection na usomi wake. Tena kijana ambaye nafikiri kesho angeweza kua Key figure kwenye ujenzi wa taifa. Ndugu yangu bwanamdogo Jery Slaa ni mpotoshaji mkubwa sana kuhusu ATCL, Sijui ni kujikakamua aonekane kwamba anajua au anatafuta sifa za kitoto.

Kwa haraka haraka nimshauri ndugu yangu Jerry Silaa kama hana uelewa na masuala ya biashara na uchumi akae kimya hata kama baba yake alikua rubani, kua rubani hakukufanyi wewe kua mtaalamu wa biashara za ndege.

ANAVYOPOTOSHA BUNGE
Msomi mzima huwezi kusema kuwa hakuna tatizo kusikia shirika miaka 10 mfululizo linapata hasara ya mabilioni ya shilingi ukafurahia ati kwa sababu ni kawaida kwa mashirika ya ndege kupata hasara, kwahiyo wananchi waendelee kukosa miradi ya maji na madawa kwa sababu kuna shirika limegeuka kua mchwa wa kumaliza pesa?

Jery anapotosha kua hasara ya ndege zetu ni kwa sababu ya COVID-19, haelewi na wala hakumbuki kwamba kua ugonjwa huu ulianza mwaka 2019 mwishoni, inahusiana vipi na hasara ya miaka ya nyuma? Huyu mtu wa aina hii tumpe jina gani?

USHAURI UNAWEZA KUMSAIDIA NDUGU HUYU NA WATU WENGINE WA AINA YAKE
Kanuni zote za kibiashara duniani hua zinataka mradi wowote katika taifa lolote lile ufunguliwe ikiwa kuna economic stability katika taifa. Una bajeti yako ndogo katika taifa halafu unachukua sehemu yake unaaanzisha mradi ambao utakuingizia hasara tena irudi kuendelea kufidia hasara ile ile kwa bajeti ile ile ndogo, hivi hii ni kitu gani kama siyo kuumiza wananchi ambao ndio walipa kodi?

Huwezi kufurahia hasara miaka mitano mfululizo ati inafufua shirika wakati unajua kabisa kua shirika lina madeni kibao, yaani unataka upae angani unapata hasara halafu bado una madeni yanazidi hata hiyo hasara unayopata, ni lini utapata faida kama utaendekeza mawazo haya ya kina Jerry Slaa?

Kama tulikua tunajua kua shirika lina madeni megi, basi tungeweza kumalizana nayo kwanza na kuweka sawa mikataba ya kimataifa lady ndio tuje tuanze kufanya maboresho ya shirika letu ili hata tunapopata hasara lakini wakati wa kuifidia kusiwe na maumivu makubwa. Au tungesibiri uchumi wetu utengamae ili tuweze kulisafisha shirika halafu tuanze na mtaji wetu wa hizo ndege huku kwenye anga la kimataifa hatuna tatizo.

Huwezi kufananisha hasara ya Shirika la ndege la Ethiopia, Kenya, Qatar au South Afrika wakati uchumi wao una ahueni wanaweza kufidia hasara hiyo.

Ifike mahali tuwe wakweli tuache kujipendekeza pendekeza ili kulisaidia taifa, unafki haujengi na hauna msaada wowote kwenye ustawi wa taifa pia. Tuwe wazalendo kama kuna hasara tukubali kua ni tatizo na ni lazima litatuliwe.
Hivi huko nyuma kabla ya 2016 mlikua na ndege ngapi na watumishi wangapi? Ukijibu hilo utajua slaa alichokua anatetea,kuwa msomi ni pamoja na kuwa na mawazo tofauti na yako.utalipaje Deni bila kua na biashara? Biashara inatakiwa ilipe Deni,ndo maana mabenki yanaweza kuikopesha biashara yako iloyumba ili upate uwezo wa kulipa Deni.
 
Wasalaam wapenzi wa jukwaa hili!

Ndugu zangu huwa napata ukakasi sana ninapoona mtu ambaye anaonekana anajiita msomi lakini anyoongea hayana reflection na usomi wake. Tena kijana ambaye nafikiri kesho angeweza kua Key figure kwenye ujenzi wa taifa. Ndugu yangu bwanamdogo Jery Slaa ni mpotoshaji mkubwa sana kuhusu ATCL, Sijui ni kujikakamua aonekane kwamba anajua au anatafuta sifa za kitoto.

Kwa haraka haraka nimshauri ndugu yangu Jerry Silaa kama hana uelewa na masuala ya biashara na uchumi akae kimya hata kama baba yake alikua rubani, kua rubani hakukufanyi wewe kua mtaalamu wa biashara za ndege.

ANAVYOPOTOSHA BUNGE
Msomi mzima huwezi kusema kuwa hakuna tatizo kusikia shirika miaka 10 mfululizo linapata hasara ya mabilioni ya shilingi ukafurahia ati kwa sababu ni kawaida kwa mashirika ya ndege kupata hasara, kwahiyo wananchi waendelee kukosa miradi ya maji na madawa kwa sababu kuna shirika limegeuka kua mchwa wa kumaliza pesa?

Jery anapotosha kua hasara ya ndege zetu ni kwa sababu ya COVID-19, haelewi na wala hakumbuki kwamba kua ugonjwa huu ulianza mwaka 2019 mwishoni, inahusiana vipi na hasara ya miaka ya nyuma? Huyu mtu wa aina hii tumpe jina gani?

USHAURI UNAWEZA KUMSAIDIA NDUGU HUYU NA WATU WENGINE WA AINA YAKE
Kanuni zote za kibiashara duniani hua zinataka mradi wowote katika taifa lolote lile ufunguliwe ikiwa kuna economic stability katika taifa. Una bajeti yako ndogo katika taifa halafu unachukua sehemu yake unaaanzisha mradi ambao utakuingizia hasara tena irudi kuendelea kufidia hasara ile ile kwa bajeti ile ile ndogo, hivi hii ni kitu gani kama siyo kuumiza wananchi ambao ndio walipa kodi?

Huwezi kufurahia hasara miaka mitano mfululizo ati inafufua shirika wakati unajua kabisa kua shirika lina madeni kibao, yaani unataka upae angani unapata hasara halafu bado una madeni yanazidi hata hiyo hasara unayopata, ni lini utapata faida kama utaendekeza mawazo haya ya kina Jerry Slaa?

Kama tulikua tunajua kua shirika lina madeni megi, basi tungeweza kumalizana nayo kwanza na kuweka sawa mikataba ya kimataifa lady ndio tuje tuanze kufanya maboresho ya shirika letu ili hata tunapopata hasara lakini wakati wa kuifidia kusiwe na maumivu makubwa. Au tungesibiri uchumi wetu utengamae ili tuweze kulisafisha shirika halafu tuanze na mtaji wetu wa hizo ndege huku kwenye anga la kimataifa hatuna tatizo.

Huwezi kufananisha hasara ya Shirika la ndege la Ethiopia, Kenya, Qatar au South Afrika wakati uchumi wao una ahueni wanaweza kufidia hasara hiyo.

Ifike mahali tuwe wakweli tuache kujipendekeza pendekeza ili kulisaidia taifa, unafki haujengi na hauna msaada wowote kwenye ustawi wa taifa pia. Tuwe wazalendo kama kuna hasara tukubali kua ni tatizo na ni lazima litatuliwe.
Naona wewe ndio mpotoshaji mkuu na nina wasiwasi na kujifanya unajua hadi kukosoa wakati inaonekana unaleta siasa kwenye mambo ya uchumi, tatizo sio kufidia sijui uchumi uko juu ,uchumi kuwa juu hauji kama njugu na ni iradi ya kimkakati ndio inainua uchumi na sio madawa au maji safi mkuu, rudi haraka darasani,tatizo Watanzania tunadhani maendeleo au kuwa taifa lenye uchumi mkubwa nikitu cha papo kwa papo nchi zilizoendelea zilianza na mapinduzi ya viwanda na kujenga miundo mbinu karibu karne 2 zilizopita sasa sisi tunajiangalia wenyewe badala ya vizazi vijavyo,halafu unaposema uchumi wa Kenya upo juu je unajua maisha wanayoishi Wakenya ,kweli unaweza kulinganisha na maisha wanayoishi Watanzania? au unasikia tu ngonjera kwenye magazeti,kwanza robo tatu ya uchumi wa Kenya unamilikiwa na mabeberu mabwenyenye wanachi hawana ardhi utakuta familia zinaishi kama manamba kwenye vibanda vya mabati, tembea uone na sio kuwa mfalme tu wa kubofya vitufe. Halafu hao Waethiopia huo uchumi unaosema uko juu kivipi sijui wakati wananchi wake wanafia kwenye makontena wakisafirishwa kama mbuzi,umasikini wa Waethiopia huwezi kulinganisha na umasikini wetu. Narudia tena muwe mnatembea kwanza kwenye nchi za watu mtaona tofauti zilizopo, tena basi na msiishie kwenye majiji makubwa nendeni hadi uswekeni.
 
Umeonesha kumpinga bila ku challenge chochote alichosema zaidi ya kutaja hasara...

Wasalaam wapenzi wa jukwaa hili!

Ndugu zangu huwa napata ukakasi sana ninapoona mtu ambaye anaonekana anajiita msomi lakini anyoongea hayana reflection na usomi wake. Tena kijana ambaye nafikiri kesho angeweza kua Key figure kwenye ujenzi wa taifa. Ndugu yangu bwanamdogo Jery Slaa ni mpotoshaji mkubwa sana kuhusu ATCL, Sijui ni kujikakamua aonekane kwamba anajua au anatafuta sifa za kitoto.

Kwa haraka haraka nimshauri ndugu yangu Jerry Silaa kama hana uelewa na masuala ya biashara na uchumi akae kimya hata kama baba yake alikua rubani, kua rubani hakukufanyi wewe kua mtaalamu wa biashara za ndege.

ANAVYOPOTOSHA BUNGE
Msomi mzima huwezi kusema kuwa hakuna tatizo kusikia shirika miaka 10 mfululizo linapata hasara ya mabilioni ya shilingi ukafurahia ati kwa sababu ni kawaida kwa mashirika ya ndege kupata hasara, kwahiyo wananchi waendelee kukosa miradi ya maji na madawa kwa sababu kuna shirika limegeuka kua mchwa wa kumaliza pesa?

Jery anapotosha kua hasara ya ndege zetu ni kwa sababu ya COVID-19, haelewi na wala hakumbuki kwamba kua ugonjwa huu ulianza mwaka 2019 mwishoni, inahusiana vipi na hasara ya miaka ya nyuma? Huyu mtu wa aina hii tumpe jina gani?

USHAURI UNAWEZA KUMSAIDIA NDUGU HUYU NA WATU WENGINE WA AINA YAKE
Kanuni zote za kibiashara duniani hua zinataka mradi wowote katika taifa lolote lile ufunguliwe ikiwa kuna economic stability katika taifa. Una bajeti yako ndogo katika taifa halafu unachukua sehemu yake unaaanzisha mradi ambao utakuingizia hasara tena irudi kuendelea kufidia hasara ile ile kwa bajeti ile ile ndogo, hivi hii ni kitu gani kama siyo kuumiza wananchi ambao ndio walipa kodi?

Huwezi kufurahia hasara miaka mitano mfululizo ati inafufua shirika wakati unajua kabisa kua shirika lina madeni kibao, yaani unataka upae angani unapata hasara halafu bado una madeni yanazidi hata hiyo hasara unayopata, ni lini utapata faida kama utaendekeza mawazo haya ya kina Jerry Slaa?

Kama tulikua tunajua kua shirika lina madeni megi, basi tungeweza kumalizana nayo kwanza na kuweka sawa mikataba ya kimataifa lady ndio tuje tuanze kufanya maboresho ya shirika letu ili hata tunapopata hasara lakini wakati wa kuifidia kusiwe na maumivu makubwa. Au tungesibiri uchumi wetu utengamae ili tuweze kulisafisha shirika halafu tuanze na mtaji wetu wa hizo ndege huku kwenye anga la kimataifa hatuna tatizo.

Huwezi kufananisha hasara ya Shirika la ndege la Ethiopia, Kenya, Qatar au South Afrika wakati uchumi wao una ahueni wanaweza kufidia hasara hiyo.

Ifike mahali tuwe wakweli tuache kujipendekeza pendekeza ili kulisaidia taifa, unafki haujengi na hauna msaada wowote kwenye ustawi wa taifa pia. Tuwe wazalendo kama kuna hasara tukubali kua ni tatizo na ni lazima litatuliwe.
 
Marekani wamejenga vingi vingine ndo wakaja kwenye hizo NASA za anasa unazozungumzia! Yaana Mtu hana kodi ya nyumba unamwambia anunue hummer, kisa NASA, NASA pori!
Unahisi Marekani hamna masikini au changamoto zozote za kihuduma za kijamii?

Kwaiyo kuwa na national carrier ni anasa? Duh!
 
Lakini hawa wakaguzi wetu wawe wanatujulisha pia hiyo Loss inavyokuwa calculated. siku zote financial statements usipojua kuzifafanua huwezi elewa.Kuna wakati statements zinaonyesha shirika linapata faida na bado linafirisika.

Wewe hujiulizi kwa nini mashirika yote makubwa duniani ya ndege yana declare loss lakini bado yapo sokoni na ndege zao zinaendelea kuruka wala hujasikia hata siku moja wameshindwa kulipa mishahara ya uendeshaji.

Finacial statements ni "fictious" zinatumia standards ambazo zimejaa estimates na judgements.

Unajua pia,kuna kitu kinaitwa uchakvu,nazo huwa ni gharama ,ijapo hakuna cashoutflow

Nadhani mijadala kama hii inahitaji watalaamu wa mambo ya uhasibu,siyo kuwaachia wanasiasa.tukiwaachia wanasiasa watatupotosha kwa maslahi yao binafsi.

Kwa upande wangu siwezi ku-hemka kwa taarifa kama hiyo iliyo ya upande mmoja.mpaka nipate taarifa zote mhimu,1) faida na hasara 2)mizania 3)mtiririko wa fedha taslimu,4)taarifa ya madiliko ya mtaji. Uhai wa shirika unaangaliwa kwa vigezo zaid ya faida tuu. pia sera za shirika katika katika uhasibu na utoaji taarifa za fedha.

Huwezi kuanza biashara kubwa kama hiyo ukapata faida ndani ya muda mfupi
Facts

Pongezi sana mkuu.
 
Hebu tutajie hizo spin off effects ambazo tunapata kutoka ATCL? Hao NASA wenyewe wanatumia rockets za Space X kupeleka Astronauts wake angani.

Kinachogomba hapa kwetu ni hiyo haja ya kuwa na midege yetu wenyewe ambayo inatutoza nauli kubwa wakati yalikuwepo mashirika yakitoa huduma hiyo hiyo kwa bei nafuu. Hao watalii walioongezeka waliletwa na mashirika ya ndege ya kimataifa bila sisi kuingia gharama yeyote isipokuwa kuvuta ada wanazotulipa kutumia anga na facilities zetu. Na kama tunadhani hao watalii watakimbilia ATCL na kuacha KLM, Emirates, Turkish Airlines n.k. tunajidanganya.
Wamarekani pamoja na mihela yao hawana shirika la taifa la ndege. British Airways inamilikiwa na IAG, kampuni ambayo imekuwa registered Spain na inamiliki Iberia na Aer Lingus.

Sisi tungewaachia wenye uzoefu watoe hiyo huduma ya usafiri wa anga na hivyo vihela vyetu tungevitumia kuboresha maisha ya wananchi wetu. Usafirishaji wowote ni biashara, sio huduma.

Amandla....
British Airways, United Airlines ni mashirika yanayoserve interests za mataifa ya Uingereza na Marekani, kama ulikuwa hujui ndio hivyo umejua sasa. Usipotezwe na majina la wamiliki yaliyoorodheshwa kwenye official websites za hayo mashirika (kumbuka US na UK ni nchi sophisticated, what you see is not always what it is), we elewa tu kwamba linapokuja suala la interests za mataifa hayo, mfano kutangaza utalii wa nchi hizo kupitia airspaces, au ikitokea emergency evacuations katika nchi zisizofikika, na mambo mengine yasiyoweza kuwekwa wazi na nchi hizo, basi elewa kwamba mashirika haya hutumika kikamilifu.

Spin-off benefits ninazoweza kuziweka wazi kwa sasa kupitia ATCL ni ya kuitangaza nchi kupitia airspaces. Jina tu lenyewe "Air Tanzania" ndege ikiwa imepaki Heathrow au Oliver Tambo airports tayari inafanya maelfu ya watu duniani wajue kuwa kuna nchi inaitwa Tanzania. Au we hujui kwanini Kenya inajulikana sana kuliko Tanzania katika domains za kimataifa?

"Sisi tungewaachia wenye uzoefu watoe hiyo huduma ya usafiri wa anga na hivyo vihela vyetu tungevitumia kuboresha maisha ya wananchi wetu."

Unaona sasa ninachokiita akili za kimaskini? Humu duniani kama tungefuata fikra zako basi tungekuwa mafukara kupita kiasi. Ubora wa maisha hautokani na kujikunyata, hao walio wazoefu wa usafiri wa anga walipataje uzoefu huo? Walizaliwa na huo uzoefu? We hujui kwamba kuna watanzania wengi wameajiriwa na ATCL, kwani hao ubora wao wa maisha hautokani na ATCL?
 
Mkuu muulize huyu mbumbumbu Precision imetusaidia nini kwa miaka yote iliyokuwapo? KLM na Ethiopia wsna agenda zao kibiashara sio agenda ya nchi yetu kama utalii na Export.



British Airways, United Airlines ni mashirika yanayoserve interests za mataifa ya Uingereza na Marekani, kama ulikuwa hujui ndio hivyo umejua sasa. Usipotezwe na majina la wamiliki yaliyoorodheshwa kwenye official websites za hayo mashirika (kumbuka US na UK ni nchi sophisticated, what you see is not always what it is), we elewa tu kwamba linapokuja suala la interests za mataifa hayo, mfano kutangaza utalii wa nchi hizo kupitia airspaces, au ikitokea emergency evacuations katika nchi zisizofikika, na mambo mengine yasiyoweza kuwekwa wazi na nchi hizo, basi elewa kwamba mashirika haya hutumika kikamilifu.

Spin-off benefits ninazoweza kuziweka wazi kwa sasa kupitia ATCL ni ya kuitangaza nchi kupitia airspaces. Jina tu lenyewe "Air Tanzania" ndege ikiwa imepaki Heathrow au Oliver Tambo airports tayari inafanya maelfu ya watu duniani wajue kuwa kuna nchi inaitwa Tanzania. Au we hujui kwanini Kenya inajulikana sana kuliko Tanzania katika domains za kimataifa?

"Sisi tungewaachia wenye uzoefu watoe hiyo huduma ya usafiri wa anga na hivyo vihela vyetu tungevitumia kuboresha maisha ya wananchi wetu."

Unaona sasa ninachokiita akili za kimaskini? Humu duniani kama tungefuata fikra zako basi tungekuwa mafukara kupita kiasi. Ubora wa maisha hautokani na kujikunyata, hao walio wazoefu wa usafiri wa anga walipataje uzoefu huo? Walizaliwa na huo uzoefu? We hujui kwamba kuna watanzania wengi wameajiriwa na ATCL, kwani hao ubora wao wa maisha hautokani na ATCL?
 
British Airways, United Airlines ni mashirika yanayoserve interests za mataifa ya Uingereza na Marekani, kama ulikuwa hujui ndio hivyo umejua sasa. Usipotezwe na majina la wamiliki yaliyoorodheshwa kwenye official websites za hayo mashirika (kumbuka US na UK ni nchi sophisticated, what you see is not always what it is), we elewa tu kwamba linapokuja suala la interests za mataifa hayo, mfano kutangaza utalii wa nchi hizo kupitia airspaces, au ikitokea emergency evacuations katika nchi zisizofikika, na mambo mengine yasiyoweza kuwekwa wazi na nchi hizo, basi elewa kwamba mashirika haya hutumika kikamilifu.

Spin-off benefits ninazoweza kuziweka wazi kwa sasa kupitia ATCL ni ya kuitangaza nchi kupitia airspaces. Jina tu lenyewe "Air Tanzania" ndege ikiwa imepaki Heathrow au Oliver Tambo airports tayari inafanya maelfu ya watu duniani wajue kuwa kuna nchi inaitwa Tanzania. Au we hujui kwanini Kenya inajulikana sana kuliko Tanzania katika domains za kimataifa?

"Sisi tungewaachia wenye uzoefu watoe hiyo huduma ya usafiri wa anga na hivyo vihela vyetu tungevitumia kuboresha maisha ya wananchi wetu."

Unaona sasa ninachokiita akili za kimaskini? Humu duniani kama tungefuata fikra zako basi tungekuwa mafukara kupita kiasi. Ubora wa maisha hautokani na kujikunyata, hao walio wazoefu wa usafiri wa anga walipataje uzoefu huo? Walizaliwa na huo uzoefu? We hujui kwamba kuna watanzania wengi wameajiriwa na ATCL, kwani hao ubora wao wa maisha hautokani na ATCL?
Stupid as stupid goes. Zile ni private entities na zina serve interests za shareholders wake kwanza.
Kama nia ni kutangaza jina la Tanzania si bora wangekodisha mabango makubwa katika nchi hizo? Hivi kweli, wih a straight face, unasema Kenya inajulikana kwa sababu wazungu wanaona Kenya Airways imepaki ndege zake Schipol Airport! Seriously!
Akili ya kimasikini ni kuchukua akiba yako yote kumcheza binti yako kwa wiki nzima ili majirani wakuone. Kama suala ni ajira, bora hizo pesa wangenunulia korosho ili watu wake waweze kuendesha maisha yao badala ya kununua mavitu ambayo haijaajiri hata watu 1000. Tunajisifu kununua ndege kwa pesa taslimu wakati tunasubiri mabeberu kuwajengea vyoo watoto wetu mashuleni mwao!

Amandla...
 
Stupid as stupid goes. Zile ni private entities na zina serve interests za shareholders wake kwanza.
Kama nia ni kutangaza jina la Tanzania si bora wangekodisha mabango makubwa katika nchi hizo? Hivi kweli, wih a straight face, unasema Kenya inajulikana kwa sababu wazungu wanaona Kenya Airways imepaki ndege zake Schipol Airport! Seriously!
Akili ya kimasikini ni kuchukua akiba yako yote kumcheza binti yako kwa wiki nzima ili majirani wakuone. Kama suala ni ajira, bora hizo pesa wangenunulia korosho ili watu wake waweze kuendesha maisha yao badala ya kununua mavitu ambayo haijaajiri hata watu 1000. Tunajisifu kununua ndege kwa pesa taslimu wakati tunasubiri mabeberu kuwajengea vyoo watoto wetu mashuleni mwao!

Amandla...
Kazi kweli kweli. Ngoja twende taratibu, utaelewa kidogo kidogo.

"British Airways (BA) is the flag carrier airline of the United Kingdom."

Hiyo sentensi ndiyo sentensi ya kwanza kwenye wikipedia page ya British Aiways. Nini maana ya flag carrier? Maana yake nini kuitwa flag carrier? "A flag carrier is a transportation company, such as an airline or shipping company, that, being locally registered in a given sovereign state, enjoys preferential rights or privileges accorded by the government for international operations."

Kwa tafsiri isiyo rasmi ni shirika la usafiri linalotambulisha nchi husika, na serikali za nchi hizo hulitumia shirika hilo kwa ajili ya "operations" za kimataifa. Neno operations nimeliweka kwenye mabano makusudi ili kama una akili basi ujiongeze. Ninaamini unazo akili so jiongeze.

Mmezoeshwa kujikataa hadi mnatia kinyaa. Mnaingizwa chaka sana na siasa za ushabiki kiasi kwamba hamuwezi kuchambua ni kipi ni maslahi ya umma, na ni kipi ni maslahi ya wanasiasa au maslahi binafsi. ATCL ni shirika la kimkakati la taifa la Tanzania, period. Kama ilivyo Tanesco, kama ilivyo TBC, hayo ni mashirika yanayotambulisha taifa la Tanzania, na kutetea maslahi ya taifa letu. Kama hiyo kazi hawaifanyi vyema hilo ni suala jingine, lakini kama una akili timamu hauwezi kusimama hapa na kutwambia kwamba kama hawafanyi vyema basi tuvunje hayo mataasisi. Huko ni kufeli, ni kutengeneza a failed state, na viongozi wanaotetea ujinga wa kuvunja ATCL ni viongozi failure takataka kabisa.
 
Hawana jipya kabisa yaani wanalipana posho kwa miezi 3 kwenye kinachoitwa Bunge la Bajeti imagine 120,000 kwa siku mara miezi 3 = 10,800,000 jumlisha na mazagazaga mengine na mshahara wao wa kila mwezi zaidi ya Mil 3 balaa sana. Wakati watumishi nwa umma wana miaka 6 hawana hata buku la nyongeza, halafu hawahawa mbulula wanajiita wabunge hawajawahi kusema lolote wanakula wanavimbiwa wanajamba tu hawajui shida za wananchi, hawawezi kuwa na akili yoyote wala mchango wowote wa maana
 
Kazi kweli kweli. Ngoja twende taratibu, utaelewa kidogo kidogo.

"British Airways (BA) is the flag carrier airline of the United Kingdom."

Hiyo sentensi ndiyo sentensi ya kwanza kwenye wikipedia page ya British Aiways. Nini maana ya flag carrier? Maana yake nini kuitwa flag carrier? "A flag carrier is a transportation company, such as an airline or shipping company, that, being locally registered in a given sovereign state, enjoys preferential rights or privileges accorded by the government for international operations."

Kwa tafsiri isiyo rasmi ni shirika la usafiri linalotambulisha nchi husika, na serikali za nchi hizo hulitumia shirika hilo kwa ajili ya "operations" za kimataifa. Neno operations nimeliweka kwenye mabano makusudi ili kama una akili basi ujiongeze. Ninaamini unazo akili so jiongeze.

Mmezoeshwa kujikataa hadi mnatia kinyaa. Mnaingizwa chaka sana na siasa za ushabiki kiasi kwamba hamuwezi kuchambua ni kipi ni maslahi ya umma, na ni kipi ni maslahi ya wanasiasa au maslahi binafsi. ATCL ni shirika la kimkakati la taifa la Tanzania, period. Kama ilivyo Tanesco, kama ilivyo TBC, hayo ni mashirika yanayotambulisha taifa la Tanzania, na kutetea maslahi ya taifa letu. Kama hiyo kazi hawaifanyi vyema hilo ni suala jingine, lakini kama una akili timamu hauwezi kusimama hapa na kutwambia kwamba kama hawafanyi vyema basi tuvunje hayo mataasisi. Huko ni kufeli, ni kutengeneza a failed state, na viongozi wanaotetea ujinga wa kuvunja ATCL ni viongozi failure takataka kabisa.
Kizungu kweli kigumu. Wapi wamesema flag carrier inatumbulisha nchi husika? Wapi wamesema kuwa nchi husika inaweza kuitumia kwa operations zake? Au ulipoona international operations ndio ukaelewa hivyo? Hapa wanazungumzia upendeleo katika international operations za shirika hilo. Kwa mfano, watapewa slots zaidi katika kusafiri kati ya Heathrow na JFK. Serikali hata siku moja haitumii ndege za shirika binafsi kwa operations nje ya utaratibu wa wao kuwa wateja kama watu wengine. Serikali kutumia commercial airlines kwa "operations" zake kutazifanya ziwe target halali kama serikali itaingia kwenye vita na nchi nyingine.

Asante kwa kuniita mjinga. Tangu lini Tanesco na ATCL zimekuwa mashirika ya kimkakati. Nchi nyingi tu hazina mashirika yake ya ndege ( Marekani, Uswisn.k.) na yanaenda vizuri tu. Nchi kama India pamoja na kiburi chake wanafanya kila jitihada kuuza Air India lakini kwa sababu wamechelewa sasa haliuziki. Nchi karibu zote za ulaya usambazaji wa nishati unafanywa na mashirika binafsi. Kazi ya serikali ni ku regulate tu.

Tofauti na unavyosema kuendelea kung'ang'ania mashirika kama ATCL ambayo hata huko kwenye watalii hawaendi kwa kuogopa ndege zao kukamatwa na wanaowadai ndio kutatugeuza kuwa failed state. Nchi haipimwi kwa ndege ngapi iliyokuwa nazo bali hali ya huduma kwa wananchi wake ( wangapi wana elimu ya kuwawezesha kumudu maisha yao, upatikanaji kwa urahisi kwa maji safi na salama, upatikanaji wa tiba bora, uhuru wa kujieleza na kuikosoa serikali yao, uhuru wa kuchagua viongozi wanaowataka n.k). Hizo ndege hata katika vipimo vya maendeleo ya nchi hazimo. Sana sana zinatufanya kuonekana vituko katika macho ya ulimwengu maana inathibitisha usemi kuwa waafrika ndivyo tulivyo.

Amandla..
 
Wasalaam wapenzi wa jukwaa hili!

Ndugu zangu huwa napata ukakasi sana ninapoona mtu ambaye anaonekana anajiita msomi lakini anyoongea hayana reflection na usomi wake. Tena kijana ambaye nafikiri kesho angeweza kua Key figure kwenye ujenzi wa taifa. Ndugu yangu bwanamdogo Jery Slaa ni mpotoshaji mkubwa sana kuhusu ATCL, Sijui ni kujikakamua aonekane kwamba anajua au anatafuta sifa za kitoto.

Kwa haraka haraka nimshauri ndugu yangu Jerry Silaa kama hana uelewa na masuala ya biashara na uchumi akae kimya hata kama baba yake alikua rubani, kua rubani hakukufanyi wewe kua mtaalamu wa biashara za ndege.

ANAVYOPOTOSHA BUNGE
Msomi mzima huwezi kusema kuwa hakuna tatizo kusikia shirika miaka 10 mfululizo linapata hasara ya mabilioni ya shilingi ukafurahia ati kwa sababu ni kawaida kwa mashirika ya ndege kupata hasara, kwahiyo wananchi waendelee kukosa miradi ya maji na madawa kwa sababu kuna shirika limegeuka kua mchwa wa kumaliza pesa?

Jery anapotosha kua hasara ya ndege zetu ni kwa sababu ya COVID-19, haelewi na wala hakumbuki kwamba kua ugonjwa huu ulianza mwaka 2019 mwishoni, inahusiana vipi na hasara ya miaka ya nyuma? Huyu mtu wa aina hii tumpe jina gani?

USHAURI UNAWEZA KUMSAIDIA NDUGU HUYU NA WATU WENGINE WA AINA YAKE
Kanuni zote za kibiashara duniani hua zinataka mradi wowote katika taifa lolote lile ufunguliwe ikiwa kuna economic stability katika taifa. Una bajeti yako ndogo katika taifa halafu unachukua sehemu yake unaaanzisha mradi ambao utakuingizia hasara tena irudi kuendelea kufidia hasara ile ile kwa bajeti ile ile ndogo, hivi hii ni kitu gani kama siyo kuumiza wananchi ambao ndio walipa kodi?

Huwezi kufurahia hasara miaka mitano mfululizo ati inafufua shirika wakati unajua kabisa kua shirika lina madeni kibao, yaani unataka upae angani unapata hasara halafu bado una madeni yanazidi hata hiyo hasara unayopata, ni lini utapata faida kama utaendekeza mawazo haya ya kina Jerry Slaa?

Kama tulikua tunajua kua shirika lina madeni megi, basi tungeweza kumalizana nayo kwanza na kuweka sawa mikataba ya kimataifa lady ndio tuje tuanze kufanya maboresho ya shirika letu ili hata tunapopata hasara lakini wakati wa kuifidia kusiwe na maumivu makubwa. Au tungesibiri uchumi wetu utengamae ili tuweze kulisafisha shirika halafu tuanze na mtaji wetu wa hizo ndege huku kwenye anga la kimataifa hatuna tatizo.

Huwezi kufananisha hasara ya Shirika la ndege la Ethiopia, Kenya, Qatar au South Afrika wakati uchumi wao una ahueni wanaweza kufidia hasara hiyo.

Ifike mahali tuwe wakweli tuache kujipendekeza pendekeza ili kulisaidia taifa, unafki haujengi na hauna msaada wowote kwenye ustawi wa taifa pia. Tuwe wazalendo kama kuna hasara tukubali kua ni tatizo na ni lazima litatuliwe.
unamshambulia bure Jerry, ana point kati hii hoja. wewe ndio umeandika pumba tupu
 
Kizungu kweli kigumu. Wapi wamesema flag carrier inatumbulisha nchi husika? Wapi wamesema kuwa nchi husika inaweza kuitumia kwa operations zake? Au ulipoona international operations ndio ukaelewa hivyo? Hapa wanazungumzia upendeleo katika international operations za shirika hilo. Kwa mfano, watapewa slots zaidi katika kusafiri kati ya Heathrow na JFK. Serikali hata siku moja haitumii ndege za shirika binafsi kwa operations nje ya utaratibu wa wao kuwa wateja kama watu wengine. Serikali kutumia commercial airlines kwa "operations" zake kutazifanya ziwe target halali kama serikali itaingia kwenye vita na nchi nyingine.

Asante kwa kuniita mjinga. Tangu lini Tanesco na ATCL zimekuwa mashirika ya kimkakati. Nchi nyingi tu hazina mashirika yake ya ndege ( Marekani, Uswisn.k.) na yanaenda vizuri tu. Nchi kama India pamoja na kiburi chake wanafanya kila jitihada kuuza Air India lakini kwa sababu wamechelewa sasa haliuziki. Nchi karibu zote za ulaya usambazaji wa nishati unafanywa na mashirika binafsi. Kazi ya serikali ni ku regulate tu.

Tofauti na unavyosema kuendelea kung'ang'ania mashirika kama ATCL ambayo hata huko kwenye watalii hawaendi kwa kuogopa ndege zao kukamatwa na wanaowadai ndio kutatugeuza kuwa failed state. Nchi haipimwi kwa ndege ngapi iliyokuwa nazo bali hali ya huduma kwa wananchi wake ( wangapi wana elimu ya kuwawezesha kumudu maisha yao, upatikanaji kwa urahisi kwa maji safi na salama, upatikanaji wa tiba bora, uhuru wa kujieleza na kuikosoa serikali yao, uhuru wa kuchagua viongozi wanaowataka n.k). Hizo ndege hata katika vipimo vya maendeleo ya nchi hazimo. Sana sana zinatufanya kuonekana vituko katika macho ya ulimwengu maana inathibitisha usemi kuwa waafrika ndivyo tulivyo.

Amandla..
Ninajitahidi sana nikujibu kistaarabu, lakini unanipa tabu sana. Lakini ngoja niendelee hivyo hivyo.

Umeandika mengi lakini nilipofika ulipoandika "uhuru wa kujieleza na kuikosoa serikali yao" ukanichefua. Yaani katika vipimo vya maendeleo kubwabwaja kinyume na taifa lako nayo unaita kipimo cha maendeleo? Na nieleweke, kwamba sitaki kusema unyimwe uhuru wa kujieleza au kukosoa.... lakini nimeshangaa sana namna gani nyie watu mnameza kila kitu mnacholishwa na systems za kibeberu kiasi cha kuweka uhuru wa kukosoa kwenye mizania sawa na huduma bora za afya.

"Nchi nyingi tu hazina mashirika yake ya ndege ( Marekani, Uswisn.k.) na yanaenda vizuri tu."

Soma United Airlines na Swiss International Airlines (zamani SwissAir). Nimekwambia nchi zote duniani zinazojielewa zipo inshu fulani hivi za kinchi ambazo hufanyika kwa wepesi zaidi au kwa maslahi mapana ya nchi yako iwapo una shirika la ndege imara ambalo serikali inaweza kulitumia kwa muktadha huo. Hakuna serikali functional isiyo na shirika lake la "kimkakati" kwa maslahi ya nchi husika. Ukiona mtu au kikundi cha watu kinatushauri tusiwe na shirika la ndege la serikali ujue huyo mtu au hicho kikundi kina ajenda zake. Nchi kama Marekani zipo sophisticated zaidi; na kutokana na nguvu za kiuchumi walizo nazo wana uwezo hata wa kuficha interests za kinchi kwenye private sector, au kujidisguise ionekane kama ni corporate private entity lakini kumbe inaserve interests za nchi ya Marekani.

"Tangu lini Tanesco na ATCL zimekuwa mashirika ya kimkakati"
"Nchi karibu zote za ulaya usambazaji wa nishati unafanywa na mashirika binafsi. Kazi ya serikali ni ku regulate tu."

Huelewi hata ninaposema kimkakati ninamaanisha nini. Unaposema kazi za serikali nchi za Ulaya ni "kuregulate tu" hata hujaeleza nini kilichomo kwenye kuregulate, wanaregulate nini, serikali imeingia mikataba ipi nao hao private generators and distributers? Hata sisi hapa TANESCO ina (ishawahi) kuwa na mikataba na private generators, refer Songas, IPTL, n.k. La muhimu ni to what extent serikali ina control energy sector. Kama level ya regulation haiziruhusu serikali za nchi hizo kuamua umeme uende wapi, ukatwe wapi, usiende wapi na kwa nini, then nchi hizo zitakuwa miongoni mwa nchi dhaifu sana kiusalama. Hata hivyo hii ni kukufumbua macho tu kwamba usidanganywe na neno "regulation". Hao energy suppliers na distributers wa Europe ni insiders wa European governments, wanaoperate kwa niaba ya serikali zao, kwa maslahi ya serikali zao. Nchini mwetu tulijaribu kuexperiment hiyo model na IPTL kilichotokea tukawa tunapigwa 120M kila siku mitambo iwe on au off.
 
Ninajitahidi sana nikujibu kistaarabu, lakini unanipa tabu sana. Lakini ngoja niendelee hivyo hivyo.

Umeandika mengi lakini nilipofika ulipoandika "uhuru wa kujieleza na kuikosoa serikali yao" ukanichefua. Yaani katika vipimo vya maendeleo kubwabwaja kinyume na taifa lako nayo unaita kipimo cha maendeleo? Na nieleweke, kwamba sitaki kusema unyimwe uhuru wa kujieleza au kukosoa.... lakini nimeshangaa sana namna gani nyie watu mnameza kila kitu mnacholishwa na systems za kibeberu kiasi cha kuweka uhuru wa kukosoa kwenye mizania sawa na huduma bora za afya.

"Nchi nyingi tu hazina mashirika yake ya ndege ( Marekani, Uswisn.k.) na yanaenda vizuri tu."

Soma United Airlines na Swiss International Airlines (zamani SwissAir). Nimekwambia nchi zote duniani zinazojielewa zipo inshu fulani hivi za kinchi ambazo hufanyika kwa wepesi zaidi au kwa maslahi mapana ya nchi yako iwapo una shirika la ndege imara ambalo serikali inaweza kulitumia kwa muktadha huo. Hakuna serikali functional isiyo na shirika lake la "kimkakati" kwa maslahi ya nchi husika. Ukiona mtu au kikundi cha watu kinatushauri tusiwe na shirika la ndege la serikali ujue huyo mtu au hicho kikundi kina ajenda zake. Nchi kama Marekani zipo sophisticated zaidi; na kutokana na nguvu za kiuchumi walizo nazo wana uwezo hata wa kuficha interests za kinchi kwenye private sector, au kujidisguise ionekane kama ni corporate private entity lakini kumbe inaserve interests za nchi ya Marekani.

"Tangu lini Tanesco na ATCL zimekuwa mashirika ya kimkakati"
"Nchi karibu zote za ulaya usambazaji wa nishati unafanywa na mashirika binafsi. Kazi ya serikali ni ku regulate tu."

Huelewi hata ninaposema kimkakati ninamaanisha nini. Unaposema kazi za serikali nchi za Ulaya ni "kuregulate tu" hata hujaeleza nini kilichomo kwenye kuregulate, wanaregulate nini, serikali imeingia mikataba ipi nao hao private generators and distributers? Hata sisi hapa TANESCO ina (ishawahi) kuwa na mikataba na private generators, refer Songas, IPTL, n.k. La muhimu ni to what extent serikali ina control energy sector. Kama level ya regulation haiziruhusu serikali za nchi hizo kuamua umeme uende wapi, ukatwe wapi, usiende wapi na kwa nini, then nchi hizo zitakuwa miongoni mwa nchi dhaifu sana kiusalama. Hata hivyo hii ni kukufumbua macho tu kwamba usidanganywe na neno "regulation". Hao energy suppliers na distributers wa Europe ni insiders wa European governments, wanaoperate kwa niaba ya serikali zao, kwa maslahi ya serikali zao. Nchini mwetu tulijaribu kuexperiment hiyo model na IPTL kilichotokea tukawa tunapigwa 120M kila siku mitambo iwe on au off.
Ngoja nikujibu kwa mara ya mwisho. Kukataa kuwa uhuru wa kujieleza na kukosoa ni nguzo mojawapo ya maendeleo inaonyesha fikra zako zilivyo duni. Hivi unadhani bila uhuru wa kukosoa na kujieleza wananchi wanawezaje kuifahamisha serikali kuhusu utendaji mbovu wa wale waliopewa dhamana ya kuwasaidia ili wapate maendeleo? Tumeona utilities wa miradi ya maji isiyotoa maji, barabara zinazoharibika baada ya msimu mmoja ambapo wananchi inabidi wamsubiri Rais ndio watoe dukuduku zao. Uhuru ungekuwepo, matatizo yangemalizika katika ngazi ya DED. Tumeona madaktari wakiogopa kutoa takwimu kuhusu ugonjwa wa Covid kwa kuogopa kushughulikiwa.

United Airlines ni mali ya United Airlines Holdings Inc, kampuni ya kibiashara. Swiss Air ilifilisika na ikafutwa kabisa. Swiss International Airlines imetokana na Cross Air. Ni Crossfire ndio iliyobadilisha jina kuwa Swiss International Airlines. Hayo unayosema kuhusu unayoita mashirika mkakati ni upuuzi tu na zinatokana na kuangalia mno Netflix. Tunashauriwa tusiwe na shirika la ndege la serikali simply kwa sababu hatuna uwezo wa kulihudumia na kuliendesha ipasavyo. Tunajenga hoja kuwa tunanunua ndege ili tulete watalii halafu tunaogopa kwenda huko kwenye watalii kwa kuogopa kuwa zitakamwatwa. Kama tuna mihela mengi kiasi hicho kwa nini tusiwalipe tu wanaotudai? Au kwa nini tusifanye kama walivyofanya waswiss ( Na CAG wa zamani alivyoshauri) kwa kuiacha ATCL ifilisiwe na madeni yafe nayo. Baada ya hapo ndio tujipange kuanzisha shirika lingingine kama tutaona kuna haja ya kufanya hivyo. Nje ya hivyo tutaishia kupeleka Dreamliner Mwanza na Zanzibar.

Regulators kazi yao ni kuhakikisha kuwa umeme wa kutosha unapatikana na kwa bei inayoeleweka. Mambo ya uende wapi au usiende wapi ni mambo ya kibiashara na soko litaamua. Hayo Mambo ya serikali kutaka kuamua umeme ukatwe wapi na ukatwe lini ndio umechangia sana uharibikaji wa mitambo yetu. Hayo maamuzi yanapaswa kufanywa na wataalamu na sio wanasiasa.

Of course, energy distributors wanafanya kazi kwa maslahi ya serikali zao kwa kulipa kodi na kufuata matakwa ya kisera ( sio uendeshaji wa serikali). Kama malengo ya serikali ni kuondokana na fossil fuels nao watawekeza kwenye nishati safi zaidi maana serikali itawaadhibu kwa kuendelea kutoa nishati chafu. Kama hata hilo haulielewi basi hautakuja kuelewa kitu hata kama tukishinda humu siku nzima. Kwa sababu hiyo, sitakujibu tena maana itakuwa kujipotezea muda.

Amandla...
 
Sio wawakilishi wote wana maono sawa wengine ni wasifia matumbo yao kwa sasa tunaita CHAWA wa bossi.

Katika mradi wa hasara ni ndege bora hizo pesa wangejenga bwawa la nyerere na SGR kwenda Arusha toka DSM
 
Back
Top Bottom