Mbunge Jacqueline Ngonyani (CCM): Ifungwe mitambo ya kukagua wabunge wa kiume ambao hawajatahiriwa

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Jan 27, 2018
747
3,059
Mbunge wa Viti Maalumu, Jacquline Ngonyani (CCM), ametaka ifungwe mashine maalumu bungeni ya kukagua wabunge wa kiume ambao hawajatahiriwa.

DyzTOJlX4AA6qto.jpg
February 7, 2019 Mbunge wa viti maalum CCM Jacqueline Ngonyani amemshauri Spika wa Bunge Job Ndugai kufunga mashine maalum Bungeni ambayo itakuwa na uwezo wa kuwakagua Wabunge wanaume ambao hawajatahiriwa ili kusaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Jacqueline Ngonyani ametoa ushauri kwa Wabunge ambao hawaja fanya tohara (hawajatahiriwa) watahiriwe haraka.

"Mh. Spika kuna suala la Mkono Sweta (Wanaume ambao hawajatahiriwa) , Mkono Sweta ni janga, mi nilikuwa nashauri tuanze na Wabunge wote humu ndani ambao pengine watabainika ambao hawajafanya hiyo tohara basi wa fanyiwe tohara mara moja," alisema Ngonyani leo Bungeni jijini Dodoma.

Aidha Mbunge huyo alisema kuwa mkono Sweta uaambukiza magonjwa mengi ukiwepo wa ukimwi amesema kuwa hiyo inaambukiza kwenye mwenye mkono sweta kwa mwanamke
 
Back
Top Bottom