Mbunge Haonga: Miradi na maendeleo majimbo ya Upinzani ni lazima sio Hisani

Evans-Arsenal

JF-Expert Member
Jan 10, 2016
868
1,385
Mbunge wa jimbo la Mbozi Mbeya, mheshimiwa Pascal Haonga (CHADEMA-Chama cha Demokrasia na Maendeleo) amesema kwamba miradi inayopangwa kwa ajili ya maendeleo katika majimbo yote nchini hasa ya upinzani sio jambo la Hisani ni jambo la lazima na hivyo serikali inapaswa kupeleka maendeleo katika kila jimbo na sio miradi kutolewa kama Hisani kwa baadhi ya majimbo nchini.

Mbunge wa mbozi alichangia mchango wake bungeni na kupinga kauli aliyotoa Mheshimiwa spika wa bunge la Tanzania Mh Jobu Ndugai ambaye aliwauliza mawaziri kuhusu kupeleka miradi ya maendeleo kwa wapinzani majimboni na hili hali wamekataa kupitisha bajeti ya fedha kwa mwaka 2017/18.
 
Back
Top Bottom