Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,891
- 939
MBUNGE MHE. FURAHA N. MATONDO AKABIDHI VITI MWENDO 70 KWA WALEMAVU KWA WILAYA ZOTE, MWANZA
Mbunge wa Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Mwanza Mhe. Furaha N. Matondo katika ziara yake aliyoifanya Wilaya zote za Mkoa wa Mwanza amekabidhi Viti Mwendo 70 kwa watu wenye ulemavu Mkoa wa Mwanza.
Hafla ya ugawaji wa Viti Mwendo hivyo ilifanyika katika Ukumbi wa Gandhi Hall uliopo Wilaya ya Nyamagana ikihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Kighoma Malima, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana na baadhi ya Viongozi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa na Wilaya, Viongozi wa UWT Mkoa na Wilaya, Madiwani, Wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Jiji la Mwanza.
"Nimefarijika sana kukutana na ndugu zangu ikiwa ni pamoja na kugawana kile nikipatacho nimepata Amani Kubwa sana na nitafanya hivi kwa wilaya zote za mkoa wa Mwanza" - Mhe. Furaha Matondo
"Nimepata wasaa wa kuendelea kujumuika na ndugu zangu wenye mahitaji maalum Wilaya ya Ilemela, ninamshukuru MUNGU sana kwa ajili ya Madaktari pia ambao wapo pamoja Nami kwa ajili ya huduma hii. Niwashukuru sana viongozi wa Chama pamoja na jumuiya ya UWT, UVCCM na Jumuiya ya Wazazi na wananchi wote wa Wilaya ya Ilemela, nasisitiza wahitaji ni watoto wetu ni Baba na mama zetu na ndugu zetu na Jamaa zetu tuwalinde tuwapende tuwajali" - Mhe. Furaha Matondo
"Viti Mwendo hivyo vitagaiwa kwa Wilaya zote saba za Mkoa wa Mwanza ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum" - Mhe. Furaha Matondo
Aidha, Mhe. Furaha Matondo amempongeza Rais wa JMT Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza Miaka Miwili Madarakani kwa kishindo huku akianisha mambo ambayo yamefanyika katika Mkoa wa Mwanza.
#UWTImara
#JeshiLaMama
#KaziIendelee