Mbunge Ester Matiko apata ajali mbaya akitoka kumjulia hali Mhere Mwita, mmoja afariki

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,395
SIMIYU: Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko apata ajali mbaya usiku wa kuamkia leo wakati akitoka Kumjulia hali Mwenyekiti wa BAVICHA Wilaya ya Geita, Kamanda Mhere Mwita. Katika ajali hiyo mtu mmoja ameripotiwa kupoteza maisha.

=======
Napenda kuwashukuru kwa kuniombea kutokana na ajali mbaya niliyoipata leo katika eneo la kitambaa kilometa chache tu toka mto Simiyu. Namshukuru sana Mungu kwa upendeleo wa pekee wa kuniokoa katika ajali hii mbaya.

Nawashukuru watanzania wote bila kujali itikadi walivyo jitahidi kutoa misaada mbali mbali mara tu baada ya ajali kutokea. Wananchi wa eneo husika, wasafiri watumiao ile barabara, Jeshi la Polisi, Wabunge, Viongozi wa wangu wa chama wa Taifa, Mkoa wa Simiyu na Mwanza, marafiki , kipekee kabisa kaka yangu mbunge wa Magu amejitolea sana kuhakikisha tunapata huduma za dharula hadi usiku wa manane. Mungu akubariki sana na akurudishie ulipojitoa.

Nimeletwa Mwanza nina maumivu makali kwenye mgongo, kiuno na mbavu ila najua Mwenyezi Mungu atatenda miujiza. Niwafariji wafiwa wa ndg yetu alipoteza maisha katika tukio hili.

Marehemu alikuwa akitokea Busega ila akawa anatembea upande wa gari za kutoka Magu. Na ndio chanzo cha ajali hawa madereva wa pikipiki tuwaombee kwa Mungu.

Ahsanteni sana Ndg zangu.

d64d77d8-1715-4ce6-b035-31c72d58cdff.jpg


190c27d9-01dc-4edf-a108-0d7e5e9bb040.jpg
190c27d9-01dc-4edf-a108-0d7e5e9bb040.jpg
 
SIMUYU: Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko apata ajali mbaya usiku wa kuamkia leo wakati akitoka Kumjulia hali Mwenyekiti wa BAVICHA Wilaya ya Geita, Kamanda Mhere Mwita. Katika ajali hiyo mtu mmoja ameripotiwa kupoteza maisha.

=======
Napenda kuwashukuru kwa kuniombea kutokana na ajali mbaya niliyoipata leo katika eneo la kitambaa kilometa chache tu toka mto Simiyu. Namshukuru sana Mungu kwa upendeleo wa pekee wa kuniokoa katika ajali hii mbaya.

Nawashukuru watanzania wote bila kujali itikadi walivyo jitahidi kutoa misaada mbali mbali mara tu baada ya ajali kutokea. Wananchi wa eneo husika, wasafiri watumiao ile barabara, Jeshi la Polisi, Wabunge, Viongozi wa wangu wa chama wa Taifa, Mkoa wa Simiyu na Mwanza, marafiki , kipekee kabisa kaka yangu mbunge wa Magu amejitolea sana kuhakikisha tunapata huduma za dharula hadi usiku wa manane. Mungu akubariki sana na akurudishie ulipojitoa.

Nimeletwa Mwanza nina maumivu makali kwenye mgongo, kiuno na mbavu ila najua Mwenyezi Mungu atatenda miujiza. Niwafariji wafiwa wa ndg yetu alipoteza maisha katika tukio hili.

Marehemu alikuwa akitokea Busega ila akawa anatembea upande wa gari za kutoka Magu. Na ndio chanzo cha ajali hawa madereva wa pikipiki tuwaombee kwa Mungu.

Ahsanteni sana Ndg zangu.

View attachment 474313

View attachment 474314 View attachment 474314
Chanzo CHa ajali hapo ni mwendo kasi zingine blabla
 
Hivi tochi za mapolisi huwa hazipo usiku??? maana hakuna jibu zaidi ya mwendo kasi ....baada ya ujio wa tochi mchana ajali zimepungua sana na madereva wanaendesha kwa adabu lakini usiku ni "fungulia dog" matokeo yake ndio haya
 
Pole Mbunge. Kwa maana hiyo dereva ametoka akiwa hana hata tatizo? Au Mbunge alikuwa peke yake manake sijasikia akitajwa mwingine zaidi ya Mbunge na Mwendesha pikipiki ambaye amepoteza maisha.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom