Mbunge CHADEMA atishiwa maisha, kisa fomu dhidi ya Mbowe

Hii ni aibu yetu sote

Yanayoendelea ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), yanasikitisha.

Pamoja na wabunge kadhaa wa Chama hicho kuparurana na kutukanana hadharani kisa suala la Mbowe kugombea tena Uenyekiti, sasa hali ya Mbunge wa Chama hicho Cecil Mwambe aliyetangaza kuchukua fomu dhidi ya Mbowe ni mbaya.

"Amelazimika kuishi kwa tahadhari kubwa. Amepanikisha wakubwa zake," kinasema chanzo cha kuaminika.

Mbunge huyo amelaumiwa hadharani na Peter Msigwa Mbunge wa Iringa Mjini kwa kuchukua fomu. Inaelezwa kuwa sasa pia amepokea vitisho kadhaa dhidi ya maisha yake.

"Ndio maana tunasema hiki chama na kwa ujumla upinzani mzima hapa nchini haujajiandaa kuishi katika zama za demokrasia. Amin nawaambieni ni heri CCM inayojibadilisha kila siku kuliko wapinzani wanaodhalilika kila siku kwa kutokiwa tayari kwa mabadiliko," anasema Mchungaji Munga Keason wa Kanisa la Peace and Gospel Fellowship.

Wakati Mwambe akiwa anaishi uhamishoni, mwenzake anayedaiwa pia kwamba atachukua fomu ya Uenyekiti, Mzee Sumaye, amekipata kinachomstahili.

Ameshindwa na kivuli chake. Yani kagombea uenyekiti Kanda ya Pwani akiwa yeye tu lakini wapigakura wamekichagua kivuli chake kwa kura 48 halafu yeye halisi kapata kura 28. Kivuli kimeshinda!

"Na kivuli hicho ni Meya wa Ubungo Chadema ambaye aliongoza fitna ya kumwangusha Sumaye kisa anataka Mtu wake yaani Mbowe apite bila kupingwa Uenyekiti licha ya kuwa ameishi zaidi ya mida wa kikatiba."
Nadhani ni dhahiri wako sahihi kabisa, ikibidi wafe kwa hofu na pressure zao hakuna wa kuwatisha.
Ccm mmewahujumu sana wabunge wa chadema kwa kuwanunua na wengine wana ushahidi wa kuwanunua tena kwa kuwatishia maisha wasipokubaliana.
Sasa hawataki watu wa kupewa dhamana kisha mkawanunua tulieni, waacheni wafanye chaguzi zao.
Sidhani kama kwenye chaguzi za Jafo waliwaingilia
 
Nilipofika tu hapa anasema Mchunganyi Munga Keason wa Kanisa la Fellowship nikaacha kusoma nikaendelea na shughuli zangu
Safari hii kuna wachungaji kadhaa, na makasisi wamesajiliwa kwenye kundinla wasiojulikana. Wengi ni hawa wanaoitwa makanisa ya kiroho.

Siongee kwa kufurahisha jukwaa, ninkwa uhakika japo siwezi kuweka vielelezo hapa. Na wanatoa taarifa kila siku kwa wakubwa zao. Na hao wachunguzeni, wenye akili mtawajua hao wasiojulikana wanaotumia makanisa na misikiti. Na waumini muwe makini katika kuyaweka wazi mambo yenu kwa viongozi wa dini, hasa wale mlio na mashaka nao.

Siku moja, kiongozi mmojawapo wa wasiojulikana, aliweka loudspeaker ya simu yake wakati akipokea taarifa toka kwa mtu anayejiita kiongozi wa kiroho, na akaniambia kuwa hakuna wakati ambao wasiojulikana wamekuwa na mtandao mpana kama awamu hii.
 
Kama ni kweli na inawezekana kabisa kuwa hivyo, basi hawa nao wanastahili kupelekwa huko SHENZISTAN. Mimi sioni ubaya wa Mbowe kuendelea lakini si kwa njia ya kutisha wanaotaka wagombee kiti hicho kikatiba. Haya ndio yanayotufanya tusiwe na vyama.
Katika maelezo yake, ulivyosoma, umeona mahali popote ambapo ameeleza ni vitisho gani vimetolewa? Vimetolewa na nani? Vimetolewa kwa njia gani?

Usipoteze muda kuziamini hizi hadithi za kijinga ambazo zipo kwaajili ya wajinga.

Ni vizuri kuwa na mabadiliko ya viongozi kila inapobidi na inapowezekana lakini siyo kwa propaganda za kiwendawazimu kama hizi.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom