Viper
JF-Expert Member
- Dec 21, 2007
- 3,667
- 1,400
Na Shakoor Jongo
jamani hawa ndio wabunge wetu! wanachi wake huko mvomero sidhani kama watakubaliana na mambo anayoyafanya DAR mbunge wao.......
source
MBUNGE wa Jimbo la Mvomero mkoani Marogoro kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM', Mhe. Amos Gabriel Makala (pichani) juzikati alifanya kufuru baada ya kugawa fedha kama njugu kwa kila mwanamuziki aliyekuwa anapanda jukwaani na kutaja jina lake.
Tukio hilo lilichukua nafasi juzikati ndani ya Maisha Club wakati Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta' ilipokuwa inatoa burudani ya ukweli.
Alipoulizwa na paparazi wetu sababu za kufanya hivyo Makala alisema: "Najisikia furaha kila jina langu linapotajwa, ndiyo maana nampa zawadi kila anayetoa kibwagizo cha kunisifia".
Bendi hiyo imekuwa ikitoa burudani ndani ya Maisha Club kila Alhamisi baada ya kuingia mkataba na uongozi wa ukumbi huo.
jamani hawa ndio wabunge wetu! wanachi wake huko mvomero sidhani kama watakubaliana na mambo anayoyafanya DAR mbunge wao.......
source