Mbunge ataka mawaziri wafanyiwe ‘interview’ kabla ya kuteuliwa, ahoji uhalali wa digrii zao

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,287
Dodoma. Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku maarufu kwa jina la Msukuma, ametaka mawaziri kufanyiwa usahili kabla ya kuteuliwa kushika nafasi hizo kutokana na baadhi yao kuwa na elimu ya juu, lakini wanashindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Akichangia katika hotuba ya Bajeti Kuu leo Alhamisi bungeni mjini hapa, Msukuma amesema walioaminiwa na kupewa nafasi hizo wamekuwa wakitajwa kwenye kashfa kubwa.

"Wengine wamegushi vyeti, tukiangalia wana madigrii huenda wengine wana uwezo mdogo wanazidiwa na makaratasi makubwa,"amesema.

Chanzo: Mwananchi
 
Je usaili unaweza kutambua UZALENDO na umakini wao??Je hii itaweza kuwa njia mbadala ya kutatua suala la mawaziri kutokuwa na umakini katika maeuala muhimu ya taifa??

ONLY GOD CAN
 
Msukuma ana mantiki sana msimpuuze achilia mbali uzalendo. Kuna maprof na PhD holders bungeni wanajibu utumbo hadi unajiuliza hivi kweli hii elimu niyaje?
 
Nikweli kabisaa. Je mngeishauri mamlaka ya uteuzi aanze na kina nani???
 
Chochote kinachofanyika chumbani kina siri nzito, lait watoto wangeshuhudia japo kwa nusu saa yafanyikayo chumbani kwa wazazi wao.
Shikamoo tusingezipata abadani.

Uhuru wa kufunga mikataba ya kitaifa ufichoni kunawapa mwanya viongozi wetu kuamua kama wendawazimu.

Dawa hapa rasilimali zote za taifa ziwekwe hadharani, tujue mbivu na mbichi kama ripoti za makinikia. Tutawajua tu wanafiki wetu. Muda ni mwl mzuri.
 
Walau kidogo naungana naye kwa vile kuna mbunge nimemsikia jana aisee sijui uelewa wake Ni butu mno
 
Kwa taratibu LIONchawe alipaswa kuachia Uwaziri wake ili kupisha uchunguzi alipokuwa Waziri wa Nishati na Madini
 
Huyu naye kuna wakati anajitambua na kuna wakati anarudi kule kule, ccm inawaharibu sana wanachama wake
 
Katiba ya Warioba ilipendekeza kuwa Mawaziri wasiwe Wabunge bali awe ameajiriwa na hivyo lazima atafanyiwa usajili. Sema Wabunge wa CCM walikiondoa kipengele hicho kwa maslahi yao binafsi.
 
Ukiwa CCM huwezi kuwa na akili hata siku moja.
Uwaziri iwe kazi ya kuomba na sio kuteuliwa.
 
C Mawaziri Tu Hata Wabunge Pia Haiwezekani Kuitikia Ndioooo Bila Kuhoji?
 
Na akome hii tabia ya kufuatilia degree za watu mwaana mwishowe ataanza kuhoji na PhD za wengine!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom