Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,441
- 7,780
Mbunge wa Kigoma Mjini, Kilumbe Shabani Ng'enda wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 ameiomba Wizara kutazama upya nyimbo za hamasa zinazoimbwa jeshini wakati wa mazoezi kuwa ziwe za kuhamasisha uzalendo na kusifia Waasisi wa Taifa na kuachana na nyimbo ambazo anadai kuwa ukizisikia tu unajua mawazo yao yako kwenye ngono.