Mbunge aswekwa ndani

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Mbunge aswekwa ndani
Waandishi Wetu
Daily News; Tuesday,February 26, 2008 @20:01



MBUNGE wa Magu Mjini ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha, Festus Limbu, jana alishikiliwa kwa saa kadhaa katika kituo cha Polisi cha Oysterbay Dar es Salaam baada ya kusababisha ajali barabarani.

Chanzo chetu cha habari kilidai kuwa sambamba na Mbunge huyo kugonga gari lililokuwa mbele yake pia ‘alimkunja’ askari wa Usalama Barabarani aliyefika eneo la ajali hadi ikabidi mgambo wa Jiji waingilie kati na kumpeleka kituo cha Polisi.

Tukio hilo lilitokea saa mbili asubuhi katika barabara ya Bagamoyo eneo la kituo cha mabasi cha Mbuyuni ambako Mbunge huyo inasemekana alishindwa kulizuia gari lake karibu na taa za kuongozea magari na kuligonga gari lililokuwa mbele yake ambalo nalo lililigonga gari jingine.

Baada ya kutokea ajali hiyo askari wa Usalama Barabarani (jina tunalo) aliyekuwa eneo hilo alikwenda kuangalia tukio hilo kujua chanzo na kuchukua taarifa muhimu za tukio zima. “Askari huyo alipofika hapo, Mbunge huyo ‘alimkunja’ akitaka kumpiga hali iliyowashtusha askari wa Jiji waliokuwa kwenye gari lao katika eneo hilo ambao walishuka kwenda kutoa msaada.

“Walipofika pale kuona raia kamkwida na kumkunja trafiki, walimkamata Limbu, wakamwingiza kwenye gari lao na kumfikisha katika kituo cha Polisi,” kilisema chanzo cha habari. Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha alikwenda kituoni hapo kufuatilia tukio hilo na baadaye Limbu aliachiwa kwa dhamana yake mwenyewe.

Limbu alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alikiri kutokea ajali hiyo na kudai kuwa gari lililokuwa mbele yake lilifunga breki ghafla hali iliyomfanya yeye ashindwe kufunga breki na kusababisha ajali.

Alikanusha kumkaba askari wa Usalama Barabarani wala kufungwa pingu na kuongeza; “Baada ya ajali ilikuja break down na kuyachukua magari yaliyopata ajali ambako la mwenzangu liliumia… sikufungwa pingu wala Masha hakuja kituoni, lile ni suala la trafiki.”

Kwa upande wake Waziri Masha licha ya kukiri kutokea kwa ajali hiyo alisema akiwa karibu na eneo hilo akielekea ofisini kwake, alipigiwa simu na Mbunge wa Geita, Ernest Mabina kuhusu ajali hiyo na ndipo alipokwenda kituoni hapo.

“Nilikwenda kituoni kumwangalia Mbunge mwenzangu lakini sikwenda kumuwekea dhamana. Nilipofika pale nilikuta RTO (Mkuu wa Usalama barabarani wa Mkoa) akizungumza na Limbu na kweli niliona kuna hali ya ajali ingawa sijaliona gari lenyewe. “RTO aliniambia analishughulikia vizuri suala hilo. Basi nami nikamwambia alishughulikie vizuri kwa mujibu wa taratibu na nikaondoka,” alisema Waziri Masha.
 
Mbunge aswekwa ndani
Waandishi Wetu
Daily News; Tuesday,February 26, 2008 @20:01



MBUNGE wa Magu Mjini ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha, Festus Limbu, jana alishikiliwa kwa saa kadhaa katika kituo cha Polisi cha Oysterbay Dar es Salaam baada ya kusababisha ajali barabarani.

Chanzo chetu cha habari kilidai kuwa sambamba na Mbunge huyo kugonga gari lililokuwa mbele yake pia ‘alimkunja’ askari wa Usalama Barabarani aliyefika eneo la ajali hadi ikabidi mgambo wa Jiji waingilie kati na kumpeleka kituo cha Polisi.

Tukio hilo lilitokea saa mbili asubuhi katika barabara ya Bagamoyo eneo la kituo cha mabasi cha Mbuyuni ambako Mbunge huyo inasemekana alishindwa kulizuia gari lake karibu na taa za kuongozea magari na kuligonga gari lililokuwa mbele yake ambalo nalo lililigonga gari jingine.

Baada ya kutokea ajali hiyo askari wa Usalama Barabarani (jina tunalo) aliyekuwa eneo hilo alikwenda kuangalia tukio hilo kujua chanzo na kuchukua taarifa muhimu za tukio zima. “Askari huyo alipofika hapo, Mbunge huyo ‘alimkunja’ akitaka kumpiga hali iliyowashtusha askari wa Jiji waliokuwa kwenye gari lao katika eneo hilo ambao walishuka kwenda kutoa msaada.

“Walipofika pale kuona raia kamkwida na kumkunja trafiki, walimkamata Limbu, wakamwingiza kwenye gari lao na kumfikisha katika kituo cha Polisi,” kilisema chanzo cha habari. Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha alikwenda kituoni hapo kufuatilia tukio hilo na baadaye Limbu aliachiwa kwa dhamana yake mwenyewe.

Limbu alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alikiri kutokea ajali hiyo na kudai kuwa gari lililokuwa mbele yake lilifunga breki ghafla hali iliyomfanya yeye ashindwe kufunga breki na kusababisha ajali.

Alikanusha kumkaba askari wa Usalama Barabarani wala kufungwa pingu na kuongeza; “Baada ya ajali ilikuja break down na kuyachukua magari yaliyopata ajali ambako la mwenzangu liliumia… sikufungwa pingu wala Masha hakuja kituoni, lile ni suala la trafiki.”

Kwa upande wake Waziri Masha licha ya kukiri kutokea kwa ajali hiyo alisema akiwa karibu na eneo hilo akielekea ofisini kwake, alipigiwa simu na Mbunge wa Geita, Ernest Mabina kuhusu ajali hiyo na ndipo alipokwenda kituoni hapo.

“Nilikwenda kituoni kumwangalia Mbunge mwenzangu lakini sikwenda kumuwekea dhamana. Nilipofika pale nilikuta RTO (Mkuu wa Usalama barabarani wa Mkoa) akizungumza na Limbu na kweli niliona kuna hali ya ajali ingawa sijaliona gari lenyewe. “RTO aliniambia analishughulikia vizuri suala hilo. Basi nami nikamwambia alishughulikie vizuri kwa mujibu wa taratibu na nikaondoka,” alisema Waziri Masha.


Chama Cha Mapinduzi mwaka huu ni wao wa kufanya vibweka bwana .Hawa Wabunge nadhani walisha jua kwamba ukisha kuwa Mbunge wa CCM basi uko juu ya sheria .Neno kuswekwa ndani sijui linatoka maana hakukaa ndani ila anaweza kuwa alikuwa polisi tu .
 
Chama Cha Mapinduzi mwaka huu ni wao wa kufanya vibweka bwana .Hawa Wabunge nadhani walisha jua kwamba ukisha kuwa Mbunge wa CCM basi uko juu ya sheria .Neno kuswekwa ndani sijui linatoka maana hakukaa ndani ila anaweza kuwa alikuwa polisi tu .


hii habari ina picha kubwa ningependa kuijadili bila ya ushabiki. kuna vitu vimo tukiipitia kwa utulivu
 
"Limbu alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alikiri kutokea ajali hiyo na kudai kuwa gari lililokuwa mbele yake lilifunga breki ghafla hali iliyomfanya yeye ashindwe kufunga breki na kusababisha ajali."

Kwa hiyo Limbu akiwa anaendesha motakaa nyuma yako, ukimwona asiyejiweza anavuka barabara kwa kutambaa, usisimame, mgonge tu, maana Limbu atakugonga na kukulaumu ulisimama ghafla, maana dereva hutakiwi kuweka umbali wowote wa kutosha kati ya motakaa yako na ile unayoikaribia. Huyu ni kiongozi na anatoa sababu za namna hii.
 
hii habari ina picha kubwa ningependa kuijadili bila ya ushabiki. kuna vitu vimo tukiipitia kwa utulivu


Hata bila kumwelekeza RTO afanye nini, kule kuwepo kwa Masha tu pale kulitosha ku influence maamuzi ya RTO. Anngiza taratibu zifuatwe yeye kama nani? atatoa maagizo ya namna hiyo kwa kesi za ajali zote kila siku na kila ajali?

Hata kama nia mbaya haikuwepo, Kulikuwa na umuhimu gani yeye kwenda, akijua wazi kuwa ni bosi wao?
 
hii habari ina picha kubwa ningependa kuijadili bila ya ushabiki. kuna vitu vimo tukiipitia kwa utulivu

Mbunge wa Magu
Mbunge wa Geita
Sikumbuki Masha ni mbunge wa wapi!!......still asking myself

.....the bottom line they are all CCM MPs........
 
"Limbu alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alikiri kutokea ajali hiyo na kudai kuwa gari lililokuwa mbele yake lilifunga breki ghafla hali iliyomfanya yeye ashindwe kufunga breki na kusababisha ajali."

Kwa hiyo Limbu akiwa anaendesha motakaa nyuma yako, ukimwona asiyejiweza anavuka barabara kwa kutambaa, usisimame, mgonge tu, maana Limbu atakugonga na kukulaumu ulisimama ghafla, maana dereva hutakiwi kuweka umbali wowote wa kutosha kati ya motakaa yako na ile unayoikaribia. Huyu ni kiongozi na anatoa sababu za namna hii.

.......kweli kabisa..........huyu Limbu inabidi driver's license yake ifungiwe for a period.......very poor respond from Limbu.................tena eneo lenyewe ni karibu na taa za kuongozea magari
 
..hiyo ni ajali tu. it can happen to anybody.

..katika hiyo scenario, sheria za trafik zinaelekeza kwamba mwenye makosa ni Dr.Limbu. Lakini pamoja na ukweli hao, maelezo yake yananiridhisha. mara kadhaa nimenusurika ktk ajali katika mazingira kama ya Dr.Limbu.

..Laurian Masha ni mbunge wa nyamagana-mwanza.
 
Masha naye alifuata nini pale? ndio yale yale hawa watu wanajiona wako above the law..mtu kawekwa ndani eti waziri naye bila aibu kakimbilia kituoni,sasa sijui alikwenda kumtoa au kuwaambia yale ya mwandosya wakubwa ni kioo cha nchi kwa hiyo wasilipe/wasidaiwe bill za maji ,huyu masha na kusoma na kukaa US na kujua vizuri sheria zinavyofanya kazi lakini lenyewe ndio la kwanza kuvunja na kuonyesha mifano mibaya kama hii ya kutumia nafasi....tuendelee kuwaandika tuu labda wataacha.
 
Masha naye alifuata nini pale? ndio yale yale hawa watu wanajiona wako above the law..mtu kawekwa ndani eti waziri naye bila aibu kakimbilia kituoni,sasa sijui alikwenda kumtoa au kuwaambia yale ya mwandosya wakubwa ni kioo cha nchi kwa hiyo wasilipe/wasidaiwe bill za maji ,huyu masha na kusoma na kukaa US na kujua vizuri sheria zinavyofanya kazi lakini lenyewe ndio la kwanza kuvunja na kuonyesha mifano mibaya kama hii ya kutumia nafasi....tuendelee kuwaandika tuu labda wataacha.


Ukisha kuwa mkuu na hasa kwa tikiti ya CCM shule yako huwa haina maana ila kuendeleza utamaduni wa kuona wewe ni Mungu hadi yakufike kama ya Lowasa ndipo utamuona kavaa kawaida lakini siku zote hata msibani na shambani alilamba suti.
 
Ajali yaweza kutokea kwa mtu yeyote,sawa.Hila hili la kumkwinda trafik japo amerikanusha na kama kweli lilitendeka basi huu ni uvujanji mkubwa wa sheria unaostahili adhabu kali.Kama nakumbuka vizuri sheria za bongo,hili ni kosa la kumzuia askari kufanya kazi yake na unatakiwa kufikishwa mahamakani. Angekuwa huku tuliko wengine angeipata fresh na asingethubutu kurudia tena kosa la kumkwinda trafik. Hii ni yale yale tunayosema kila siku,mbunge au kiongozi akitoka chama tawala basi yeye anajua yuko juu ya sheria,juzi tu tumeyasikia ya Komba kule kiteto.
Swali:Hivi angekuwa raia wa kawaida ndiyo kamkwinda trafik,hao mgambo wa jiji wangemuacha tu na angefikishwa kituo cha polisi angekuwa na hali gani wakati huu? nahisi angekuwa MOI-muhimbili
 
Mbunge wa Magu
Mbunge wa Geita
Sikumbuki Masha ni mbunge wa wapi!!......still asking myself

.....the bottom line they are all CCM MPs........

Masha ni Mbunge wa Nyamagana, Mwanza.
 
Mbunge aswekwa ndani
Waandishi Wetu
Daily News; Tuesday,February 26, 2008 @20:01



MBUNGE wa Magu Mjini ambaye aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Fedha, Festus Limbu, jana alishikiliwa kwa saa kadhaa katika kituo cha Polisi cha Oysterbay Dar es Salaam baada ya kusababisha ajali barabarani.

Chanzo chetu cha habari kilidai kuwa sambamba na Mbunge huyo kugonga gari lililokuwa mbele yake pia ‘alimkunja’ askari wa Usalama Barabarani aliyefika eneo la ajali hadi ikabidi mgambo wa Jiji waingilie kati na kumpeleka kituo cha Polisi.

Tukio hilo lilitokea saa mbili asubuhi katika barabara ya Bagamoyo eneo la kituo cha mabasi cha Mbuyuni ambako Mbunge huyo inasemekana alishindwa kulizuia gari lake karibu na taa za kuongozea magari na kuligonga gari lililokuwa mbele yake ambalo nalo lililigonga gari jingine.

Baada ya kutokea ajali hiyo askari wa Usalama Barabarani (jina tunalo) aliyekuwa eneo hilo alikwenda kuangalia tukio hilo kujua chanzo na kuchukua taarifa muhimu za tukio zima. “Askari huyo alipofika hapo, Mbunge huyo ‘alimkunja’ akitaka kumpiga hali iliyowashtusha askari wa Jiji waliokuwa kwenye gari lao katika eneo hilo ambao walishuka kwenda kutoa msaada.

“Walipofika pale kuona raia kamkwida na kumkunja trafiki, walimkamata Limbu, wakamwingiza kwenye gari lao na kumfikisha katika kituo cha Polisi,” kilisema chanzo cha habari. Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha alikwenda kituoni hapo kufuatilia tukio hilo na baadaye Limbu aliachiwa kwa dhamana yake mwenyewe.

Limbu alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alikiri kutokea ajali hiyo na kudai kuwa gari lililokuwa mbele yake lilifunga breki ghafla hali iliyomfanya yeye ashindwe kufunga breki na kusababisha ajali.

Alikanusha kumkaba askari wa Usalama Barabarani wala kufungwa pingu na kuongeza; “Baada ya ajali ilikuja break down na kuyachukua magari yaliyopata ajali ambako la mwenzangu liliumia… sikufungwa pingu wala Masha hakuja kituoni, lile ni suala la trafiki.”

Kwa upande wake Waziri Masha licha ya kukiri kutokea kwa ajali hiyo alisema akiwa karibu na eneo hilo akielekea ofisini kwake, alipigiwa simu na Mbunge wa Geita, Ernest Mabina kuhusu ajali hiyo na ndipo alipokwenda kituoni hapo.

“Nilikwenda kituoni kumwangalia Mbunge mwenzangu lakini sikwenda kumuwekea dhamana. Nilipofika pale nilikuta RTO (Mkuu wa Usalama barabarani wa Mkoa) akizungumza na Limbu na kweli niliona kuna hali ya ajali ingawa sijaliona gari lenyewe. “RTO aliniambia analishughulikia vizuri suala hilo. Basi nami nikamwambia alishughulikie vizuri kwa mujibu wa taratibu na nikaondoka,” alisema Waziri Masha.

Hivi lini utakuja na hoja endelevu na ukaachana na hivi vitukio vidogo vidogo ambavyo magazeti ya kiu na ijumaa yanaviripoti kila siku. Tunataka vitu mtu wa pwani najua uwezo unao ila ni mvivu tu. Sisiemi kuwa hivi si vitu muhimu ila nachotaka kusema ni kuwa muda ni mali hivyo kuupoteza kwenye vitu ambavyo unaweza kuvipata kwenye kiu na kwa kibunango kiurahisi hamna haja ya kudublicate hapa
 
Hivi lini utakuja na hoja endelevu na ukaachana na hivi vitukio vidogo vidogo ambavyo magazeti ya kiu na ijumaa yanaviripoti kila siku. Tunataka vitu mtu wa pwani najua uwezo unao ila ni mvivu tu. Sisiemi kuwa hivi si vitu muhimu ila nachotaka kusema ni kuwa muda ni mali hivyo kuupoteza kwenye vitu ambavyo unaweza kuvipata kwenye kiu na kwa kibunango kiurahisi hamna haja ya kudublicate hapa

sawa mkuuu nimefahamu ulilokusudia ila....................
 
Back
Top Bottom