Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Mods, tafadhali iachane hii walau hadi itakapopata jibu la uhakika na ndipo muichanganye na nyingine.....
Wajuvi wa Sheria,
Mie swali langu ni fupi sana. Tumesoma kuwa kama Mbunge akifariki au kujiondoa, basi CHAMA kilichoshinda ubunge kwa jimbo hilo, kitatoa mtu wa PILI aliyekuwa kwenye list. Jambo hili mie ninaona lina ulakini fulani.
Kama kweli huko tuendako kutakuwa na Wagombea wasio na vyama, sasa huyo asiye na chama ikitokea ameacha kuwa Mbunge kwa sababu yoyote ile, nani atarithishwa Ubunge wake?
Mie nafikiri Eliminations kwenye vyama ife na waache walau kila chama kiwe na Wagombea walau tuseme wanne na hao wote wapigiwe kura ukichanganya na wale wasio na vyama. Atakayepata kura nyingi katika hao ndiyo mshindi na ikitokea Mbunge au Diwani kaacha kuwa Mbunge au Diwani basi wanachukua mtu aliyekuwa wa pili kwenye LISTI nzima bila kuangalia ametoka chama gani.
Sijui kama nayo itakuwa njia nzuri sana ila walau itasaidia kama kweli tunataka kuokowa hela za walipa kodi. Uchaguzi ujao kama hii hali itaruhusiwa, wanaweza kutokea wagombea wengi sana wasiofungamana na chama chochote na hao mwisho wa siku wakawa wanaleta uchaguzi wa mara kwa mara.
Wajuvi wa Sheria,
Mie swali langu ni fupi sana. Tumesoma kuwa kama Mbunge akifariki au kujiondoa, basi CHAMA kilichoshinda ubunge kwa jimbo hilo, kitatoa mtu wa PILI aliyekuwa kwenye list. Jambo hili mie ninaona lina ulakini fulani.
Kama kweli huko tuendako kutakuwa na Wagombea wasio na vyama, sasa huyo asiye na chama ikitokea ameacha kuwa Mbunge kwa sababu yoyote ile, nani atarithishwa Ubunge wake?
Mie nafikiri Eliminations kwenye vyama ife na waache walau kila chama kiwe na Wagombea walau tuseme wanne na hao wote wapigiwe kura ukichanganya na wale wasio na vyama. Atakayepata kura nyingi katika hao ndiyo mshindi na ikitokea Mbunge au Diwani kaacha kuwa Mbunge au Diwani basi wanachukua mtu aliyekuwa wa pili kwenye LISTI nzima bila kuangalia ametoka chama gani.
Sijui kama nayo itakuwa njia nzuri sana ila walau itasaidia kama kweli tunataka kuokowa hela za walipa kodi. Uchaguzi ujao kama hii hali itaruhusiwa, wanaweza kutokea wagombea wengi sana wasiofungamana na chama chochote na hao mwisho wa siku wakawa wanaleta uchaguzi wa mara kwa mara.