Mbunge asema migogoro ya ardhi inachangiwa na taasisi za Serikali

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,021
1,609
1653563401715.png

Akichangia bajeti ya Wizara ya Ardhi Bungeni leo Mei 26, Dkt Joseph Kizito amesema “sehemu kubwa ya migogoro katika maeneo yetu inachangiwa na taasisi zingine za serikali, inapotokea mwananchi ana matumizi na ardhi na Serikali kupitia idara zake wanaihitaji hiyo ardhi, wizara ya ardhi isimame kama hakimu, anayetenda haki kwa kila upande kwani wote wanamamlaka sawa ya umiliki ardhi”

Ameendelea “Madaba tuna mgogoro wa ardhi, kati ya wananchi wa Kipingo na watu wa hifadhi, lakini watu wa hifadhi wametumia ubabe kuchukua maeneo ya wananchi, utaratibu huu hauwezi kuleta afya” amemsihi Waziri wa Ardhi kuwapigania wananchi hao na kuhakikisha wanapata haki zao

Aidha amesema Migogoro ya ardhi haiwezi kutatuliwa na mahakama pekee, kwa kuwa mahakama ina utaratibu unaochelewesha mashauri sana, hivyo ameshauri Wizara husika ijifunze kwa mheshimiwa Lukuvi wakati ule anaenda mkoa hadi mkoa anakaa na wananchi na kutatua migogoro pamoja bila kusubiria mlolongo wa mahakama
 
Lukuvi alifiti sn kwenye hii Wizara, baada ya muda siyo mrefu Riziwani ndiyo atakuwa Waziri kamili kulinda maslahi ya mafisadi wenzake
 

Akichangia bajeti ya Wizara ya Ardhi Bungeni leo Mei 26, Dkt Joseph Kizito amesema “sehemu kubwa ya migogoro katika maeneo yetu inachangiwa na taasisi zingine za serikali, inapotokea mwananchi ana matumizi na ardhi na Serikali kupitia idara zake wanaihitaji hiyo ardhi, wizara ya ardhi isimame kama hakimu, anayetenda haki kwa kila upande kwani wote wanamamlaka sawa ya umiliki ardhi”

Ameendelea “Madaba tuna mgogoro wa ardhi, kati ya wananchi wa Kipingo na watu wa hifadhi, lakini watu wa hifadhi wametumia ubabe kuchukua maeneo ya wananchi, utaratibu huu hauwezi kuleta afya” amemsihi Waziri wa Ardhi kuwapigania wananchi hao na kuhakikisha wanapata haki zao

Aidha amesema Migogoro ya ardhi haiwezi kutatuliwa na mahakama pekee, kwa kuwa mahakama ina utaratibu unaochelewesha mashauri sana, hivyo ameshauri Wizara husika ijifunze kwa mheshimiwa Lukuvi wakati ule anaenda mkoa hadi mkoa anakaa na wananchi na kutatua migogoro pamoja bila kusubiria mlolongo wa mahakama
MIGOGORO ya ARDHI MANISPAA ya SUMBAWANGA INATENGENEZWA na WATENDAJI WA ARDHI MANISPAA na OFISI YA KAMISHNA

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Mimi ni mhanga wa hoja hii, serikali imehusika kwenye migogoro mingi ya ardhi. Mfano mtu kauziwa nyumba ya serikali, serikali inabariki sub-division ya kiwanja cha serikali kwa watu wasiohusika kabisa wala sio wanfanyakazi wa serikali kugawiwa kipande cha ardhi.
 
Eti mmejenga kwenye eneo la Jeshi!!!! Nchi ngumu hii, Mungu saidia.
ardhi inawadai au inamdai mtu kodi ya uwanja mil 8 deni halisi mil 2 adhabu mil 6 hii ni akili ya namna gani.kama mtu kashindwa kulipa hiyo mil 2 anawezaje kulipa mil 6?hawana tathimini hata ya uwezo wa wateja wao.na kwanini mtu huyo asilipe deni halisi bila adhabu tena kwa instalment kuliko kumwekea hizo adhabu ambazo kiuhalisia hataweza kulipa na serikali haitapata hizo pesa?hii ni mbinu ya kuwanyang'anya maskini ardhi yao/nyumba zao kwa kuwatishia kuzipiga mnada.
 
Back
Top Bottom