Kididimo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 3,791
- 3,360
Nimemsikiliza Mbunge mmoja bungeni jana kama sijakosea ni Mbunge wa Maswa, akisema Wazungu wanabagua aina ya magonjwa na chanjo zake ili watufanyie biashara. Akatolea mfano wa Malaria kuwa hawajawahi kutafuta chanjo huku wakijua ndiyo inauwa watu wengi Afrika. Na, wanahangaika na chanjo ya magonjwa yasiyouwa sana kama Corona ili wafanye biashara.
Ukweli mimi binafsi sikubaliani naye. Bahati mbaya, sijafahamu taaluma yake, japo kwa nilivyomsikia maelezo yake, ni kama mwanasiasa asiye mtafiti mzuri.
Kama sijakosea hapa Tanzania tuna kituo maalamu cha utafiti wa ugonjwa wa malaria kiko Ifakara, Morogoro. Hiki kituo kwa kushirikiana na Taasisi nyingine kimekuwa kikijihusisha na utafiti wa tiba na chanjo ya malaria. Pia tayari shirika la afya Duniani WHO limeithinisha baadhi ya chanjo zilizogundiliwa sehemu mbalimbali duniani kutumika, mfano ni RTS,S. Hii chanjo imetumika Malawi, Ghana, Kenya na hata hapa Tanzania na kuonyesha mafanikio.
Lengo langu siyo kumbeza Waziri wetu mwenye dhamana ya Afya zetu, ila ni pale anapochelewa kureact kwa jambo lisilo sahihi.
Na miaka ya karibuni, Wasomi wetu wamekuwa wakikaa kimya bila kuchallenge hoja za wanasiasa pale inapolazimika au unapotokea upotoshaji.
Pia Mbunge kusema Corona haiuwi sana watu siyo sahihi. Hajatupa takwimu yoyote kuonyesha ni kiasi gani watu wamepimwa (kuwa screened) na kati ya hao, wangapi wamegundulika na wangapi wamepona au kufariki. Bunge letu linaporuhusu Mbunge kuongea jambo asilonauhakika nalo na Wasomi nao wakakaa kimya ni hatari sana.
Wiki hii tumepoteza Wazee maarufu na baadhi yao wasomi waliobobea kwa kitu kinaitwa "CHANGAMOTO YA UPUMUAJI". Kitaalamu, Waziri anatakiwa afafanue hili jambo kuwa je, hiyo changamoto ya upumuaji inaambukiza? Na kama inaambukiza, atupe angalau takwimu na jinsi ya kujikinga nayo!
Nimeona taarifa moja ya masikitiko ya kifo cha Prof. Mpangala,kuwa kilitokana na changamoto ya upumuaji. Na atasafirishwa kutoka Dodoma hadi Iringa na hatimaye hadi Dar kupumzishwa.
Bahati mbaya sijaona tamko lolote kuhusu tahadhari kwa wanaohudumia, kusafirisha, kuzika hawa ndugu zetu wansopoteza maisha kwa changamoto ya upumuaji.
Isijekuwa hili nalo ni janga la aina ile ile tuliloliwekea masharti ya namna ya kuzikana mwaka jana na leo Mbunge kasema tusihofu, na Wasomi wakakaa kimya huku hali ikizidi kuwa tete.
Ukweli mimi binafsi sikubaliani naye. Bahati mbaya, sijafahamu taaluma yake, japo kwa nilivyomsikia maelezo yake, ni kama mwanasiasa asiye mtafiti mzuri.
Kama sijakosea hapa Tanzania tuna kituo maalamu cha utafiti wa ugonjwa wa malaria kiko Ifakara, Morogoro. Hiki kituo kwa kushirikiana na Taasisi nyingine kimekuwa kikijihusisha na utafiti wa tiba na chanjo ya malaria. Pia tayari shirika la afya Duniani WHO limeithinisha baadhi ya chanjo zilizogundiliwa sehemu mbalimbali duniani kutumika, mfano ni RTS,S. Hii chanjo imetumika Malawi, Ghana, Kenya na hata hapa Tanzania na kuonyesha mafanikio.
Lengo langu siyo kumbeza Waziri wetu mwenye dhamana ya Afya zetu, ila ni pale anapochelewa kureact kwa jambo lisilo sahihi.
Na miaka ya karibuni, Wasomi wetu wamekuwa wakikaa kimya bila kuchallenge hoja za wanasiasa pale inapolazimika au unapotokea upotoshaji.
Pia Mbunge kusema Corona haiuwi sana watu siyo sahihi. Hajatupa takwimu yoyote kuonyesha ni kiasi gani watu wamepimwa (kuwa screened) na kati ya hao, wangapi wamegundulika na wangapi wamepona au kufariki. Bunge letu linaporuhusu Mbunge kuongea jambo asilonauhakika nalo na Wasomi nao wakakaa kimya ni hatari sana.
Wiki hii tumepoteza Wazee maarufu na baadhi yao wasomi waliobobea kwa kitu kinaitwa "CHANGAMOTO YA UPUMUAJI". Kitaalamu, Waziri anatakiwa afafanue hili jambo kuwa je, hiyo changamoto ya upumuaji inaambukiza? Na kama inaambukiza, atupe angalau takwimu na jinsi ya kujikinga nayo!
Nimeona taarifa moja ya masikitiko ya kifo cha Prof. Mpangala,kuwa kilitokana na changamoto ya upumuaji. Na atasafirishwa kutoka Dodoma hadi Iringa na hatimaye hadi Dar kupumzishwa.
Bahati mbaya sijaona tamko lolote kuhusu tahadhari kwa wanaohudumia, kusafirisha, kuzika hawa ndugu zetu wansopoteza maisha kwa changamoto ya upumuaji.
Isijekuwa hili nalo ni janga la aina ile ile tuliloliwekea masharti ya namna ya kuzikana mwaka jana na leo Mbunge kasema tusihofu, na Wasomi wakakaa kimya huku hali ikizidi kuwa tete.