Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,890
- 939
Mbunge wa Viti Maalum Vijana Mjini Magharibi Amina Ali Mzee alikuwa mgeni rasmi katika kufungua mafunzo ya vijana dhidi ya dawa za kulevya yaliyoandaliwa na taasisi ya vijana Mwembetanga Youth Organization (MYO)
Amina Mzee amewapongeza sana taasisi ya vijana ya Mwembetanga Youth Organization (MYO) kwa kuandaa mafunzo haya kwa vijana kwani wimbi kubwa wanaoathirika na dawa za kulevya ni vijana
"Niwaombe taasisi hii ya Mwembetanga Youth Organization (MYO) na taasisi nyingine waendeleee kutoa mafunzo na sisi viongozi wao wenye dhamana ya kusimamia vijana tutawaunga mkono ili kuhakikisha vijana katika jamii zetu wimbi la vijana wenye kutumia dawa za kulevya linapungua kwa asilimia kubwa" - Amina Mzee