Mbunge akerwa Zanzibar kufananishwa na wilaya

zanzibar ni nchi. hata kama ni ndogo kieneo na watu, zipo nchi nyingine ni ndogo kuliko znb. mf. Vatican ni ndogo kuliko kata ya manzese ambayo ina wakazi 120000, wakati vaticani ina wakazi wasiozidi 3000. ufumbuzi ni serikali 3.
 
Muungano umetuweka salama sana dhidi ya magaidi, otherwise Zanzibar/Pemba zingekuwa kama Somalia/Somaliland! Tuendelee kuuenzi Muungano huu wa kipekee duniani! Mungu uwaangamize wote wanaouonea kijicho Muungano wetu! Wote semeni Amen!

Na hii ndio falsafa inayotumika kuwa brainwash WADANGANYIKA then tunaendelea kutetea tusichokijua.
 
wakubwa lazima tukubali kuwa hapa kuna tatizo,kama mbunge anaitolea zanzibar mfano kwa ukubwa wa eneo tu,mzanzibar anaomba mwongozo....hatari!!!..hivi anayejua aniambie hivi sababu kubwa ya tanganyika na zanzibar kuungana ni nini???..mara nyingi watu wanaungana ili wafaidi rasilimali kwa pamoja...lakini katika muungano huu utasikia..mafuta yasiyo ya muungano...hivi mnaweza kuoana halaf kila mtu akabaki na shuka lake???..samahani sikuwepo mwaka 1964..mtanisamehe

hebu tuongelee mifano hai...tuliambiwa mafuta na gas asilia ni rasilimali za muungano, fair enough. Lakini zanzibar wanauliza kwamba gas asilia imekua ikivunwa kwa karibuni miaka 7 hivi sasa...kwanini hakua mgao au share yeyote waliopelekewa zanzibar iliyotokana na gas asilia. Sasa kuna kosa gani zanzibar wakidai mafuta yasiwe ya muunganano?
 
Na hii ndio falsafa inayotumika kuwa brainwash WADANGANYIKA then tunaendelea kutetea tusichokijua.
Acha hizo, huu Muungano maridadi sana na ni wa kujivunia! Mzanzibari ana uraia wa nchi mbili, yaani Mzanzibari na pia Mtanzania! Ndio maana Mzanzibari mwenye akili ataupigania Muungano huu usifariki hata kidogo! Mtanganyika (Mtanzania Bara kama ukipenda) anafaidika na hali ya utulivu iliyopo chini ya Muungano huu!
 
hebu tuongelee mifano hai...tuliambiwa mafuta na gas asilia ni rasilimali za muungano, fair enough. Lakini zanzibar wanauliza kwamba gas asilia imekua ikivunwa kwa karibuni miaka 7 hivi sasa...kwanini hakua mgao ua share yeyote waliopelekewa zanzibar iliyotokana na gas asilia. Sasa kuna kosa gani zanzibar wakidai mafuta yasiwe ya muunganano?
Tatizo la Wazanzibari wamekuwa na jazba kuliko maelezo! Kwani wakiongea bila jazba hawawezi kusikilizwa? Ushauri wangu ni kwamba Wazanzibari waombe mgao wa gesi asilia na mafuta toka Serikali ya Muungano kuliko kutaka kumiliki mafuta ambayo kimsingi yana uwezekano mdogo sana wa kupatikana!
 
Matumizi mabaya ya muda wa bunge. Hata mimi nishawahi kusema Zanzibar kwa size na resource za kiuchumi ni ndogo kuliko Kahama.

Ukisoma magazeti ya Kimarekani, Mmarekani akitaka kukuambia nchi ni ndogo anakwambia "It is smaller than Rhode Island" their smallest state, au Jana nilikuwa naangalia some PBS documentary kuna Mmarekani mmoja kaenda Iran, anarekodi watu wa Iran katika juhudi za kuonyesha the positive side of Iran, kaiita Iran "This Alaska size country". Kama mtu anasema kwa nia ya kuonyesha proportionality, sioni tatizo liko wapi.

Wazanzibari wengine wana inferiority complex kama alivyosema mkuu hapo juu. Zanzibar ni ndogo kuliko Geita, this is a fact, the MP cannot change this.
 
zanzibar ni nchi. hata kama ni ndogo kieneo na watu, zipo nchi nyingine ni ndogo kuliko znb. mf. Vatican ni ndogo kuliko kata ya manzese ambayo ina wakazi 120000, wakati vaticani ina wakazi wasiozidi 3000. ufumbuzi ni serikali 3.
Zanzibar ni "nchi" lakini eneo lake ni dogo kuliko Wilaya ya Geita!
 
hebu tuongelee mifano hai...tuliambiwa mafuta na gas asilia ni rasilimali za muungano, fair enough. Lakini zanzibar wanauliza kwamba gas asilia imekua ikivunwa kwa karibuni miaka 7 hivi sasa...kwanini hakua mgao ua share yeyote waliopelekewa zanzibar iliyotokana na gas asilia. Sasa kuna kosa gani zanzibar wakidai mafuta yasiwe ya muunganano?

Hapa naona kuna kujichanganya....kama gesi asilia ni ya muungano (Zanzibar included!) na inatumiwa na serikali ya muungano kwa faida ya serikali ya muungano, Zanzibar wanataka mgawo wa nini na wao ni sehemu ya muungano huo? Gesi imekuwa ikizalisha umeme (ingawa bado hautoshi) na umeme huo kutumiwa pia na wazanzibari (tena kwa bei ya chini kuliko ya wenzao wa bara) tena wanataka mgawo wa nini?
 
Bw. Max alisema kuwa wilaya ya Geita ina ofisa kilimo mmoja, wakati wilaya hiyo ni kubwa kuliko Kilwa na Zanzibar.

Huyu mbunge wa CUF nae ana vituko. Ni wapi hapa Mh. Max kasema Zanzibar ni wilaya??? Hapa Max kaongelea ukubwa wa eneo na hata haja taja Zanzibar kama mkoa.
 
Muungano umetuweka salama sana dhidi ya magaidi, otherwise Zanzibar/Pemba zingekuwa kama Somalia/Somaliland! Tuendelee kuuenzi Muungano huu wa kipekee duniani! Mungu uwaangamize wote wanaouonea kijicho Muungano wetu! Wote semeni Amen!

Mhh hivi kweli? mbona tumeshambuliwa na magaidi katika ubalozi wa Marekani na watanzania wengi walikufa wakati tupo kwenye muungano.
 
Tatizo la Wazanzibari wamekuwa na jazba kuliko maelezo! Kwani wakiongea bila jazba hawawezi kusikilizwa? Ushauri wangu ni kwamba Wazanzibari waombe mgao wa gesi asilia na mafuta toka Serikali ya Muungano kuliko kutaka kumiliki mafuta ambayo kimsingi yana uwezekano mdogo sana wa kupatikana!

Kwanini waombe wakati hiyo katiba kama kweli ndio emesema hivyo...Kila anaehisi anadhulumiwa hawezi kutokuwa na jazba...it's a natural human instinct
 
Huyu mbunge wa CUF nae ana vituko. Ni wapi hapa Mh. Max kasema Zanzibar ni wilaya??? Hapa Max kaongelea ukubwa wa eneo na hata haja taja Zanzibar kama mkoa.

still bado ameonesha dharau! nadhani lengo lake lilikuwa wilaya yake ipate mgao mkubwa kushinda nchi ya znz.. znz ni inchi inafaa sisi watanganyika tuheshimu! ...

kuna siku nilikuwa na dada kutoka znz .. alikuwa mgeni huku ughaibuni ilibidi nimepele madukani ... tukakutana na mtu kutoka Uganda akatuuliza mnatokea nchi gani . yule dada akasema " aim from zanzibar" dah! mim ilibidi nibaki kimya sababu hakuna nchi inayotwa tanganyika!

inabidi tudai tanganyika yetu kwa nguvu!!
 
Hapa naona kuna kujichanganya....kama gesi asilia ni ya muungano (Zanzibar included!) na inatumiwa na serikali ya muungano kwa faida ya serikali ya muungano, Zanzibar wanataka mgawo wa nini na wao ni sehemu ya muungano huo? Gesi imekuwa ikizalisha umeme (ingawa bado hautoshi) na umeme huo kutumiwa pia na wazanzibari (tena kwa bei ya chini kuliko ya wenzao wa bara) tena wanataka mgawo wa nini?

Kwahiyo tumerudi pale pale , kama huu muungano ni ubabaishaji tuu. Nia na madhumuni si muungano bali kuitawala Zanzibar. Iweje kama zanzibar ni partner wa muungano isielezwe kinachoingia na kutoka cha muungano? You want to be both a partner and a master wa muungano at the same time? Kila kitu waamuzi Bara...It's amazing ...
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Kwahiyo tumerudi pale pale , kama huu muungano ni ubabaishaji tuu. Nia na madhumuni si muungano bali kuitawala Zanziar. Iweje kama zanzibar ni partner wa muungano isielezwe kinachoingia na kutoka cha muungano? You want to be both a partner and a master wa muungano at the same time? Kila kitu waamuzi Bara...It's amazing ...

Kutawaliwa na nani? Tanganyika haipo! Kuna muungano ambao na Zanzibar yumo na kuna Zanzibar pekee......sasa hapa suala la kuitawala Zanzibar linatokea wapi? Sana sana unaweza kusema Zanzibar ndio inaitawala Tanganyika (mfano, hebu angalia kipindi cha Rais Mwinyi....basically nchi nzima (bara na Zanz) ilikuwa chini ya wazanzibari!). Angalia bungeni....wabunge wa Zanzibar wanapigia kura (wanafanya maamuzi) hata masuala yasiyohusu Znz. Au kuna kitu nakimiss hapa?
 
still bado ameonesha dharau! nadhani lengo lake lilikuwa wilaya yake ipate mgao mkubwa kushinda nchi ya znz.. znz ni inchi inafaa sisi watanganyika tuheshimu! ...

kuna siku nilikuwa na dada kutoka znz .. alikuwa mgeni huku ughaibuni ilibidi nimepele madukani ... tukakutana na mtu kutoka Uganda akatuuliza mnatokea nchi gani . yule dada akasema " aim from zanzibar" dah! mim ilibidi nibaki kimya sababu hakuna nchi inayotwa tanganyika!

inabidi tudai tanganyika yetu kwa nguvu!!

Kwa nini ukae kimya? Kwani passport yako inaonyesha unatoka wapi???
 
Wabunge Wengine wa Bara lazima waende kwenye Darasa la Siasa, kama kweli tunataka Muungano wa hiari na sio kulazimishwa.Hauwezi kulinganisha Nchi na Wilaya PERIOD.
Ni dhambi gani kuilinganisha Zanzibar na Geita kigeografia? Mnajidai mnamachungu lakini hayana mashiko. Kwani mtu akilinganisha uswisi na mkoa wa Tabora kwa maana ya ukubwa wa kijografia ni dhambi? Mda wote wabunge toka Zanzibar hawana jipya zaidi ya kulalamika tu na kukosoa tu Zanzibar inapotajwa.
 
Kutawaliwa na nani? Tanganyika haipo! Kuna muungano ambao na Zanzibar yumo na kuna Zanzibar pekee......sasa hapa suala la kuitawala Zanzibar linatokea wapi? Sana sana unaweza kusema Zanzibar ndio inaitawala Tanganyika (mfano, hebu angalia kipindi cha Rais Mwinyi....basically nchi nzima (bara na Zanz) ilikuwa chini ya wazanzibari!). Angalia bungeni....wabunge wa Zanzibar wanapigia kura (wanafanya maamuzi) hata masuala yasiyohusu Znz. Au kuna kitu nakimiss hapa?

haha haha !!! ni mfano wa kumkabidhi funguo za nyumba mtoto wako wa kiume...Documents za umiliki wa nyumba bado unazo wewe (baba) . Tanganyika imevaa koti la Tanzania...Inaitumia "Tanzania" kwa manufaa ya Tanganyika na hiki ndicho wanachokiogopa wa tanganyika "kulivua koti la Tanzania .
 
Kwa nini ukae kimya? Kwani passport yako inaonyesha unatoka wapi???

mwenzangu aliyeulizwa mwanzo kasema anatokea zanzbar ... sasa mimi niseme Tanzania ..? ambayo ni muungano wa tangayika + Zanzibar. kwanza ningemchanganya yule muuliza swali nianze zanzibar ni muungano wa nchi mbili tanganyika na zanzbar,

kama ningeulizwa mimi wa kwanza mnatokea nchi gani ningemuwahi TZN.... then maswali magumu yangebaki kwa yule mzenji
 
Back
Top Bottom