Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,494
- 19,327
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetabiriwa mabaya ikiwemo kung'oka madarakani katika miaka 10 ijayo, au kusababisha mapambano na wananchi wanaodai haki na uhuru.
Aidha, viongozi walio madarakani wametakiwa kutochukulia nafasi walizonazo kama ni dhamana na si zao binafsi.
Kauli hizo zimetolewa na Mbunge wa Jimbo la Maputo nchini Msumbiji, Dk Eduardo Namburete katika mahojiano maalum na Mwananchi jijini Nairobi nchini Kenya hivi karibuni.
"Tanzania sio kisiwa mambo yake yanafahamika, yanasikika na matatizo yake kama Msumbiji. Kama chama tawala (CCM) hakitabadilika, miaka 10 ijayo kinaweza kuanguka madarakani, kama si hivyo kinaweza kusababisha machafuko kutokana na wananchi kudai haki zao na uhuru," alisema Dk Namburete.
Hayo yamekuja huku ndani ya CCM kukiwa na vuguvugu, kuwepo kwa makundi kupingana waziwazi kimsimamo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo mapambano dhidi ya ufisadi.
Dk Namburete ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Eduardo Mondlane cha mjini Maputo Msumbiji alisema, CCM na vyama vingine vilivyopigania uhuru barani Afrika na kuendelea kuongoz hadi sasa vimeanza kusahau malengo ya uhuru na ahadi zao kwa wananchi hivyo kugeuka na kuwa sawa na wakoloni.
"..Tangu walipochukua madaraka viongozi wamejishikiza zaidi na vyama na familia zao na kusahau wananchi, wamesahau malengo ya uhuru, wamesahau ahadi zao kwa wananchi na kuendeleza ubinafsi," alisema mwanasiasa huyo kijana.
Alifafanua kuwa viongozi wengi wa Afrika ikiwemo Tanzania wamemezwa na ubinafsi huku wakikumbuka na kuwakumbatia marafiki zao na familia zao pekee, wakiwa na taswira ya kujilinda zaidi kutokana na kuogopa kubanwa na sheria watokapo madarakani.
Dk Namburete ambaye ni Mbunge kwa tiketi ya chama cha Renamo kinachoongozwa na Afonso Dhakama alisema kutokana na hali hiyo wananchi wameanza sasa wanatambua zaidi haki zao na kuanza kuhoji matukio yanayoendelea katika nchi zao na kutaka mabadiliko.
"Vyama tawala sasa vina hali ngumu katika utawala, wananchi wanajua haki zao wanaona uovu, wamechoka ndiyo maana kelele za kudai mabadiliko zipo kila mahali Afrika," alisema Dk Namburete na kuongeza:
Matukio yanayotokea kwenye baadhi ya nchi za Afrika hivi sasa kudai mabadiliko kama Afrikakusini ni ishara tosha kuwa watawala wa kiafrika wamegeuka wakoloni na kuwa wananchi wameanza harakati mpya kuwaondoa wakoloni hao. Hali isipobadilika zitaenea barani Afrika ndani ya miaka 10."
Chanzo: Mwananchi
Mbunge huyu anasema ukweli usiobishika kabisa. Kwanza yeye ni mtu wa nje, kwa hiyo hana anachopata binafsi kutokana na maneno haya
Aidha, viongozi walio madarakani wametakiwa kutochukulia nafasi walizonazo kama ni dhamana na si zao binafsi.
Kauli hizo zimetolewa na Mbunge wa Jimbo la Maputo nchini Msumbiji, Dk Eduardo Namburete katika mahojiano maalum na Mwananchi jijini Nairobi nchini Kenya hivi karibuni.
"Tanzania sio kisiwa mambo yake yanafahamika, yanasikika na matatizo yake kama Msumbiji. Kama chama tawala (CCM) hakitabadilika, miaka 10 ijayo kinaweza kuanguka madarakani, kama si hivyo kinaweza kusababisha machafuko kutokana na wananchi kudai haki zao na uhuru," alisema Dk Namburete.
Hayo yamekuja huku ndani ya CCM kukiwa na vuguvugu, kuwepo kwa makundi kupingana waziwazi kimsimamo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo mapambano dhidi ya ufisadi.
Dk Namburete ambaye pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Eduardo Mondlane cha mjini Maputo Msumbiji alisema, CCM na vyama vingine vilivyopigania uhuru barani Afrika na kuendelea kuongoz hadi sasa vimeanza kusahau malengo ya uhuru na ahadi zao kwa wananchi hivyo kugeuka na kuwa sawa na wakoloni.
"..Tangu walipochukua madaraka viongozi wamejishikiza zaidi na vyama na familia zao na kusahau wananchi, wamesahau malengo ya uhuru, wamesahau ahadi zao kwa wananchi na kuendeleza ubinafsi," alisema mwanasiasa huyo kijana.
Alifafanua kuwa viongozi wengi wa Afrika ikiwemo Tanzania wamemezwa na ubinafsi huku wakikumbuka na kuwakumbatia marafiki zao na familia zao pekee, wakiwa na taswira ya kujilinda zaidi kutokana na kuogopa kubanwa na sheria watokapo madarakani.
Dk Namburete ambaye ni Mbunge kwa tiketi ya chama cha Renamo kinachoongozwa na Afonso Dhakama alisema kutokana na hali hiyo wananchi wameanza sasa wanatambua zaidi haki zao na kuanza kuhoji matukio yanayoendelea katika nchi zao na kutaka mabadiliko.
"Vyama tawala sasa vina hali ngumu katika utawala, wananchi wanajua haki zao wanaona uovu, wamechoka ndiyo maana kelele za kudai mabadiliko zipo kila mahali Afrika," alisema Dk Namburete na kuongeza:
Matukio yanayotokea kwenye baadhi ya nchi za Afrika hivi sasa kudai mabadiliko kama Afrikakusini ni ishara tosha kuwa watawala wa kiafrika wamegeuka wakoloni na kuwa wananchi wameanza harakati mpya kuwaondoa wakoloni hao. Hali isipobadilika zitaenea barani Afrika ndani ya miaka 10."
Chanzo: Mwananchi
Mbunge huyu anasema ukweli usiobishika kabisa. Kwanza yeye ni mtu wa nje, kwa hiyo hana anachopata binafsi kutokana na maneno haya