Mbunge adaiwa kununua vitabu vya msemakweli na kuchoma moto

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Mbunge adaiwa kununua vitabu kuchoma moto

Mwandishi Wetu , Mwanza


KITABU cha ‘Mafisadi wa Elimu’ kimezidi kuwa lulu jijini Mwanza baada ya

nakala zake 25,000 ambazo zilitarajiwa kusambazwa kwa mauzo,

kununuliwa na mmoja wa wabunge na kuchomwa moto.


Habari zilizopatikana jijini Mwanza na kuthibitishwa na mmoja wa

mawakala waliopewa jukumu la kusambaza ili kuuza vitabu hivyo,

zilieleza kuwa mwanasiasa huyo kupitia kwa watu wake wa karibu aliomba

kununua nakala zote hizo za vitabu kwa nyakati tofauti kwa madai ya

kuvisambaza bure kwa watu.


Kitabu hicho ambacho kimeanza kusambazwa katika mikoa mbalimbali kwa

mauzo kimekuwa kikitafutwa na wananchi kwa ajili ya kusoma ili

kutambua kilichoandikwa hivyo kuwa gumzo kwa wananchi.


Imeelezwa kuwa mbunge huyo wa kanda ya ziwa kwa mara ya kwanza

alipata taarifa za kuingia kitabu hicho na kutuma watu kukusanya

nakala hizo katika meza za wauzaji na kwenda kuchoma moto.

“Baada ya nakala za kwanza ambazo zilikuwa kama 5,000 kununuliwa

kwa siku moja na kuisha, wakala aliwasiliana na mwenye kitabu ambaye

aliamua kutuma nakala nyingine kwa ajili ya kuuzwa, lakini pia

aliambiwa zimeisha baada ya siku mbili” alieleza mmoja wa wauza

magazeti wa mkoani Mwanza.


Kutokana na kukosekana kwa kitabu hicho baadhi ya wafanyabiashara kwa

kutumia moja ya nakala ambazo wamebahatika kuwa nazo wameanza kudurufu

kitabu hicho kwa kutoa nakala ambazo wanaziuza mitaani

kwa bei ya Sh3000.

“Mimi binafsi kila ninapokwenda kuuza magazeti watu wamekuwa

wakiniulizia kitabu hicho na wengine wameniomba kikifika tu

niwapelekee wakanunue, sasa nilipowaambia bado hakipatikani ila kuna

nakala walisema niwapelekee na waliweza kununua kwa bei

ile ya kitabu” alieleza muuza magazeti huyo.


Katika kitabu hicho wabunge ambao walidaiwa kuwa na shahada feki ni

Anthony Diallo, Deodarus Kamala pamoja na Raphael Chegeni ambao

walitajwa kuwa na shahada ya uzamili(masters) na uzamivu(PhD) feki
 
Sasa ni dhahiri hao waheshimiwa wana digrii feki,kwanini wanaogopa hicho kitabu kisomwe na watu kama kweli mtu ana digrii ya kweli,pia baado sijaridhika na digrii ya David Mathayo na inabidi sijui(bahati mbaya Takukuru nao hawaaminiki) wangelichunguza hilo swala,Prof Nkunya katuongopea anakuwa naye kama sio musomi kuhusu suala la kumsafisha David hata mimi ngumbaru nimeona kuna walakini mkubwa au ndio ufisadi wa elimu umemuingia huyo Professor,pia naona siasa zimeingilia kati sidhani kama hao wabunge wangekuwa wa upinzani serikali ingekaa kimya,aibu kwenu wabunge vihiyo nyie ndio mko tayari kuwaibia mitihani watoto wenu!aibu kwenu
 
Hii sredi inahusiana vp na MMU? Mods plz do ze nidful! Imekaa kipolitikali zaidi
 
Nasikia kuwa hata Dkt Mwakyembe alifeli Form IV akatumia cheti cha ndugu yake kuendelea na masomo ya A Level!
 
Nasikia kuwa hata Dkt Mwakyembe alifeli Form IV akatumia cheti cha ndugu yake kuendelea na masomo ya A Level!
Miaka ile ilikuwa vigumu sana kwenda secondary bila kurudia mitihani mara saba au nane hivi, Bonde la mto Lufilyo karibu wasomi wowte walirudia madarasa na shule baada ya kuhitimu kujaribu bahati zao tena.
 
Mwandishi Wetu , Mwanza
Chanzo: Gazeti la Mwanchi Jumapili

KITABU cha "Mafisadi wa Elimu" kimezidi kuwa lulu jijini Mwanza baada ya nakala zake 25,000 ambazo zilitarajiwa kusambazwa kwa mauzo, kununuliwa na mmoja wa wabunge na kuchomwa moto.

Habari zilizopatikana jijini Mwanza na kuthibitishwa na mmoja wa
mawakala waliopewa jukumu la kusambaza ili kuuza vitabu hivyo, zilieleza kuwa mwanasiasa huyo kupitia kwa watu wake wa karibu aliomba kununua nakala zote hizo za vitabu kwa nyakati tofauti kwa madai ya kuvisambaza bure kwa watu.

Kitabu hicho ambacho kimeanza kusambazwa katika mikoa mbalimbali kwa
mauzo kimekuwa kikitafutwa na wananchi kwa ajili ya kusoma ili kutambua kilichoandikwa hivyo kuwa gumzo kwa wananchi.

Imeelezwa kuwa mbunge huyo wa kanda ya ziwa kwa mara ya kwanza
alipata taarifa za kuingia kitabu hicho na kutuma watu kukusanya nakala hizo katika meza za wauzaji na kwenda kuchoma moto.

"Baada ya nakala za kwanza ambazo zilikuwa kama 5,000 kununuliwa kwa siku moja na kuisha, wakala aliwasiliana na mwenye kitabu ambaye aliamua kutuma nakala nyingine kwa ajili ya kuuzwa, lakini pia aliambiwa zimeisha baada ya siku mbili" alieleza mmoja wa wauza magazeti wa mkoani Mwanza.

Kutokana na kukosekana kwa kitabu hicho baadhi ya wafanyabiashara kwa
kutumia moja ya nakala ambazo wamebahatika kuwa nazo wameanza kudurufu kitabu hicho kwa kutoa nakala ambazo wanaziuza mitaani kwa bei ya Sh3,000.

"Mimi binafsi kila ninapokwenda kuuza magazeti watu wamekuwa wakiniulizia kitabu hicho na wengine wameniomba kikifika tu niwapelekee wakanunue, sasa nilipowaambia bado hakipatikani ila kuna nakala walisema niwapelekee na waliweza kununua kwa bei ile ya kitabu" alieleza muuza magazeti huyo.

Katika kitabu hicho wabunge ambao walidaiwa kuwa na shahada feki ni
Anthony Diallo, Deodarus Kamala pamoja na Raphael Chegeni ambao walitajwa kuwa na shahada ya uzamili (masters) na uzamivu (PhD) feki.

MY Comments: .
Kama hawahusiki na vyeti feki , vijitabu wanachoma moto vya nini? Nadhani kuna kila sababu ya wananchi kuhoji na kuomba TCU iwaite watu hao kwa lazima wapeleke vyeti vyao.
 
Sasa huyu mbunge atanunua hizo kopi mpaka lini?Na huyo mchapaji wa hicho kitabu si ataendelea kutajirika?Huyo mbunge kweli ana upungufu wa elimu
 
Sasa huyu mbunge atanunua hizo kopi mpaka lini?Na huyo mchapaji wa hicho kitabu si ataendelea kutajirika?Huyo mbunge kweli ana upungufu wa elimu


Mkuu Ben,

Kweli aliyesema ukiona Elimu ghali, jaribu Ujinga..kweli hakukosea.
 
Kama kweli Dialo kanunua na kuchoma moto vitabu ni upungufu wa maarifa ni sawa na mwanafuzi kushindwa somo la hesabu na kuamua kuchoma moto kitabu cha hesabu kitu ambacho hakitasaidia kitu
 
Mbona habari aina chanzo?

Umeanza kuisoma habari paragraph gani . Kwenye mitihani ya shule primary na sekondary tuliambiwa kabla ya kujibu mawasli soma maelekezo unaweza kukuta maelekezo ni usijibu swali. kama hujaona source rudia kusoma kwa makini.

Hawa jamaa wamezoea kununua magazeti sasa wamenza na kwenye vitabu.
 
.

MY Comments: .
Kama hawahusiki na vyeti feki , vijitabu wanachoma moto vya nini? Nadhani kuna kila sababu ya wananchi kuhoji na kuomba TCU iwaite watu hao kwa lazima wapeleke vyeti vyao.

Tunawahukumu wenyewe! TCU ni hao hao. kama cheti chako ni cha halali why bother?

na mkoa wa mwanza ina wengi kwenye hako kajitabu, so kuna uwezekano hata hizo hela walichanga! huwezi ukapambana na wananchi, hivi sasa wameongeza kasi ya kitabu kununuliwa.

Hatuna viongozi tuna wahuni wahuni tu, huyo mbunge alichofanya si ujinga wala umbumbumbu, ni uhuni!
 
Biashara nzuri sana hii,ngoja niwasiliane na wachapishaji ili ninunue kwao vitabu kisha nawauzia "mafisadi wa Elimu" wanavichoma kisha naagiza vingine hivyo hivyo mpaka na mie nitoke. Hii itakuwa biashara halali maana lazima kodi ntalipa.
 
Sasa huyu mbunge atanunua hizo kopi mpaka lini?Na huyo mchapaji wa hicho kitabu si ataendelea kutajirika?Huyo mbunge kweli ana upungufu wa elimu[/QUOTE]

Kweli tupu kwenye bold. Kwa mtu ambaye ana akili na utashi huwezi kununua hivyo vitabu wakati printer yupo kazini, labda umnunue Printer asiprint tena. Du kweli ukihiyo una kazi.

Halafu wamekaa kimya, kama wamenyeshewa mvua.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom