Mbunge adai kufanyiwa vitendo vya kishirikina jimboni

Nyambala

JF-Expert Member
Oct 10, 2007
4,465
1,169
Du! huyu naye ni kiongozi by 2010???? Kweli Tanzania ni zaidi ya uijuavyo! Wakuu are we really serious?

Mbunge adai kufanyiwa vitendo vya kishirikina jimboni

Hussein Semdoe, Kilindi

MBUNGE wa Jimbo la Kilindi katika Mkoa wa Tanga, Beatrice Shelukindo amesema amekuwa akifanyiwa vituko mbalimbali vya kishirikiana wakati wa ziara za kutembelea wananchi na hivyo kushindwa kutekeleza shughuli zake kwa ufanisi.

Shelukindo alidai kila anapoanza ziara ya kuwatembelea wananchi wake vijijini, hukumbana na vikwazo mbalimbali ikiwa ni pamoja na gari yake kuharibika mara kwa mara katika mazingira ya kutatanisha na wakati mwingine kunusurika kupata ajali baada ya gari lake kuparamia miti

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika mikutano ya hadhara, wakati akihutubia wananchi katika vijiji vya kata za Saunyi na Mswaki wilayani Kilindi juzi Shelukindo, aliwataka wachawi hao, kufanya dawa ili akubaliwe kila jambo analoliomba serikalini kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo hilo kama kuboreshea miundombinu mbalimbali katika eneo hilo.

"Kuna jambo linalonishangaza kila ninapotaka kufanya ziara hapa jimboni, yanaibuka mambo ya ajabu, hivi karibuni nilikuwa nikiwahi kikao mjini Songe, lakini gari yangu ikazimika ghafla, lakini likawaka na nilipofika jirani na mji huo, gari likaharibika tena, nikapanda basi la kwanza nalo likaharibika, nikapanda la pili nalo pia liliharibika na nilichelewa kikao kile.

Jamani ndugu zangu uchawi hauna faida yoyote tubadilike ki fikra ili tuelekeze nguvu zetu katika kufanya kazi zetu za maendeleo pamoja na kusomesha watoto wetu, lakini kuendekeza ushirikina ni kupotoka kimaendeleo," alisema Shelukindo.

Mbunge huyo aliwaomba wazee na waganga wilayani hapa kumsaidia kufanya dawa ili aweze kuwahi vikao mbalimbali vya kusaidia maendeleo ya wilaya hiyo, badala ya kufanya dawa ili achelewe, kama wanavyomfanyia.


Alisema ni aibu kwa baadhi ya wakazi wa Jimbo hilo la Kilindi kuendekeza vitendo hivyo vya kishirikina ambavyo vimekithiri na kudai kuwa sasa vimepitwa na wakati.

"Ndugu zangu niwaeleze hali halisi ilivyo, mimi nimepata majaribu mengi yanayohusiana na ushirikina, niliyowaeleza ni baadhi tu. Kama isingekuwa kumuomba Mungu sasa hivi tayari ningeshafukiwa kaburini na ingebaki mifupa,"alisema huku akionyesha kusikitishwa na hali hiyo.


Source: Mwananchi
 
I hope alikuwa anatania tu kujaribu kujikosha na tabia yake ya kuchelewa!
 
Du! huyu naye ni kiongozi by 2010???? Kweli Tanzania ni zaidi ya uijuavyo! Wakuu are we really serious?
Ukitaka kumjua mtu aljiyechuja ni aina hii ya viongozi. Kwani huyu mama huko ni kwao mila na tamaduni za kwao anazifahamu na hao wanaotaka kugombea jimbo hilo ni wa kwao na yeye yuko kwenye seat hivi sasa. Wasiwasi wa nini kama anakubalika???

Unajua kuna aina ya wabunge ambao ni wapiga kelele sana bungeni Hivyo kuwafanya wajulikane sana kitaifa lakini kwenye majimbo yao hakuna kitu cha maana wanachokifanya na mara nyingi huwa wanatumia miaka 4 kutumbua dar na dodoma na nje ya nchi na mwaka 1 hutumia jimboni na inapofikaribia kipindi cha uchaguzi hulialia kama fisi.

Hivi kama wewe ni mbunge na jimboni kwako unakubalika wasiwasi wa nini??? Wananchi hivi sasa wameelimika sana na hawadanganyiki na fix za kisiasa hivyo kama hufikii vigezo vyao watakutimua tuu.
 
Aende kwa marehemu Mandondo kule atapata ujinga wote anaoutaka,ila pepo hatokuwa nayo iwapo umauti utamkuta kabla ya kutubu!
 
Si ameokoka huyu? Mbona sasa asitumie nguvu za wokovu kuushinda uchawi. Dada Beatrice umenisikitisha kwa hili maana nilijua wewe uu mlokole wa kikweli. Hutakiwi kuogopa kama una Yesu wako. Kemea kwa jina la Yesu na utashinda.

Ukweli ni kwamba Tanga ni mkoa unaojulikana kwa aina zote za uchawi na nguvu za jiza ila pia Wilaya ya Kilindi ndiyo yenyewe.
 
Kajuaje karogwa kama na yeye si mchawi...

Kaziii kwei kwei.. CCM na Sheikh Yahya Hussein
 
Magazeti hayaaminiki tena, ingekuwa si hivyo ningeona inconsistencies katika kauli za mbunge kuomba kufundwa halafu hapo hapo kujitia mtu wa dini.
 
Kama ni mtu wa mungu ataamini vipi ushirikina? kwa upande mwingine anawaomba wachawi wamsaidie... nae anahusika kwa njia fulani. Kuamini ni kushiriki!!
 
Magazeti hayaaminiki tena, ingekuwa si hivyo ningeona inconsistencies katika kauli za mbunge kuomba kufundwa halafu hapo hapo kujitia mtu wa dini.
Waswahili wenzangu ninaomba tafsiri ya nene UNAFIKI
 
Ushirikina ni mojawapo ya sera za chama cha cha mafisadi, hatuwashangai ,kwani hata ofisi kuuubwa kuliko zote nchini imeingia kwenye upuuzi huu wa kutumia wachawi kutisha watu wasigombee nafasi hiyo. Hivi hamkumbuki kilichotokea kwa mgombea wa chama hicho kule mwanza mwaka 2005? Hakika tutayasikia mengi.
 
Hii ndiyo level ya imani za giza ilipofika, sasa maalbino wetu watapona? watoto wetu watapona? kwa imani hii unadhani wakazi wa kilindi ni watu wa namna gani? Na huyu mama ana dini?

Mungu ibariki tanzania
 
Wabwanga ya kweli haya??



Kwa lipi moja haya anayosema Mbunge au hiyo imani yake ya kishirikina?
Kwa mie sioni ukweli wa hilo lakwanza na nashangazwa na hili la pili, Hata Shelukindo nae? Hata hivyo huyo si CCM au la kwani CCM kule Ikulu si mnajuwa ya Sheikh Yahya na maombi kwa timu ya Ivory Coast.
 
Mwaka huu, we acha tuuu! tutaskia mengi sana. Mbunge Beatrice anajiandaa kupambana na Aisha kigoda katika jimbo la kilindi, wawili hao hawaivi sasa hivi nasikia kila mmoja anamtuhumu mwenzake ni mchawi, ama kweli ukistaajabu ya tanga...!
 
Kwa nnavyoijua Tanzania, sishindwi kushangaa, kwamba hiyo kitu ina ukweli!

Huyu mama keshafulia kwa lugha ya siku hizi ya mjini, kwahiyo hayo yote anayosema hayanaukweli maji yamezidi unga huko jimboni kwake na sasa anatafuta sababu za kupata sympathy ya wapigakura!!
Mbunge anaeamini ushirikina hawezi kuwaletea watu maendeleo afadhali wananchi wa Kilindi wamtose aende akaimbe ngonjela!!
 
Huyu mama keshafulia kwa lugha ya siku hizi ya mjini, kwahiyo hayo yote anayosema hayanaukweli maji yamezidi unga huko jimboni kwake na sasa anatafuta sababu za kupata sympathy ya wapigakura!!
Mbunge anaeamini ushirikina hawezi kuwaletea watu maendeleo afadhali wananchi wa Kilindi wamtose aende akaimbe ngonjela!!



Quote:
SMU


I hope alikuwa anatania tu kujaribu kujikosha na tabia yake ya kuchelewa!






Mkuu ukweli naomaanisha ni kuwa "haya maneno yalisemwa na huyu mama" na hii ni baada yah SMU kuweka benefit of doubt kwamba huenda ni
spinning ya mwandishi.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom