Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,720
- 155,327
WANASAYANSI wamegundua kuzuka kwa jamii nyingine ya mbu wanaoeneza malaria ambao wanatoa changamoto kwa wataalamu wa afya duniani, sasa kutakiwa kubuni mbinu mpya za kujikinga na ugonjwa huo unaoua watu wengi kuliko magonjwa mengine.
Mbu hao wana tabia tofauti na wale ambao wataalamu wamekuwa wakielezea mara kwa mara ndio wanaoeneza malaria.
Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya kuambukiza na Mzio (Niaid) ya Marekani, imesema kundi la wanasayansi nchini Uingereza wamegundua aina hiyo mpya ya mbu na kutoa ripoti hiyo hadharani mwezi uliopita.
Taarifa iliyotolewa na Niaid kwa gazeti hili ilieleza kwamba katika utafiti huo, wataalamu hao waligundua kwamba katika jamii ya mbu, Anopheles gambiae; ambao wanajulikana tangu zamani kuwa ndio waenezao malaria, imezuka jamii nyingine inayotofautiana na hiyo kitabia, mfumo wa kibaiolojia na mazingira ya kuishi.
"Katika mbu wa kundi la Anopheles gambiae limezuka jingine linalotofautiana kitabia jambo linaloashiria kwamba wote sasa watasababisha ugumu wa kujikinga na malaria kwa njia zinazotumika sasa," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Utafiti huo ambao tayari umechapishwa kwenye jarida la kumbukumbu muhimu za kisayansi duniani, umetahadharisha kwamba tatizo hilo linazidi kuiweka katika hali mbaya zaidi Afrika kwa sababu ndiyo yenye kiwango kikubwa cha kuenea kwa ugonjwa huo, duniani.
"Anopheles gambiae ni mbu anayeeneza malaria katika nchi za Afrika zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara (Tanzania ni miongoni) ambazo zina kasi kubwa zaidi ya kuenea ugonjwa huo," inaeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inaeleza kwamba utafiti huo umegundua kuzuka kwa jamii hizo mbili ambazo zinawiana kimaumbo lakini zinatofautina kwa mfumo wa vinasaba (DNA) lakini wana uwezo wa kuzaliana.
Kuibuka kwa makundi hayo mawili ya mbu waenezao malaria, wanasayansi hao wanasema moja kwa moja yatakuwepo mabadiliko ya namna wadudu hao wanavyoeneza malaria.
"Hii inaelekea kusababisha ugumu wa kujikinga na malaria kwa kutumia njia ambazo tayari zimebuniwa na zinatumika sasa duniani kwa sababu mfumo wa kitabia wa mbu sasa umebadilika," taarifa hiyo inamnukuu mmoja wa wanasayansi walioshiriki katika utafiti huo, Profesa George Christophides.
"Ni wakati wa wataalamu wa afya duniani kukaa chini na kuchunguza zaidi jamii hizo ili kuibua njia mpya za kujikinga na ugonjwa huo." alisisitiza.
Kutofautiana huko kibaiolojia, wanasayansi hao wanasema hata dawa za kuua mbu pamoja na mazalia yake zinapaswa kufanyiwa marekebisho, ili ziweze kuua jamii zote.
Katika nchi nyingi za Afrika, Tanzania ikiwa miongoni, zimekuwa zikitumia dawa aina ya pyrethroids kwenye vyandarua ili kukabiliana na mbu waenezao malaria kwa maelezo kwamba wana tabia ya kuuma binadamu usiku wa manane.
Mbu hao wana tabia tofauti na wale ambao wataalamu wamekuwa wakielezea mara kwa mara ndio wanaoeneza malaria.
Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya kuambukiza na Mzio (Niaid) ya Marekani, imesema kundi la wanasayansi nchini Uingereza wamegundua aina hiyo mpya ya mbu na kutoa ripoti hiyo hadharani mwezi uliopita.
Taarifa iliyotolewa na Niaid kwa gazeti hili ilieleza kwamba katika utafiti huo, wataalamu hao waligundua kwamba katika jamii ya mbu, Anopheles gambiae; ambao wanajulikana tangu zamani kuwa ndio waenezao malaria, imezuka jamii nyingine inayotofautiana na hiyo kitabia, mfumo wa kibaiolojia na mazingira ya kuishi.
"Katika mbu wa kundi la Anopheles gambiae limezuka jingine linalotofautiana kitabia jambo linaloashiria kwamba wote sasa watasababisha ugumu wa kujikinga na malaria kwa njia zinazotumika sasa," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Utafiti huo ambao tayari umechapishwa kwenye jarida la kumbukumbu muhimu za kisayansi duniani, umetahadharisha kwamba tatizo hilo linazidi kuiweka katika hali mbaya zaidi Afrika kwa sababu ndiyo yenye kiwango kikubwa cha kuenea kwa ugonjwa huo, duniani.
"Anopheles gambiae ni mbu anayeeneza malaria katika nchi za Afrika zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara (Tanzania ni miongoni) ambazo zina kasi kubwa zaidi ya kuenea ugonjwa huo," inaeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inaeleza kwamba utafiti huo umegundua kuzuka kwa jamii hizo mbili ambazo zinawiana kimaumbo lakini zinatofautina kwa mfumo wa vinasaba (DNA) lakini wana uwezo wa kuzaliana.
Kuibuka kwa makundi hayo mawili ya mbu waenezao malaria, wanasayansi hao wanasema moja kwa moja yatakuwepo mabadiliko ya namna wadudu hao wanavyoeneza malaria.
"Hii inaelekea kusababisha ugumu wa kujikinga na malaria kwa kutumia njia ambazo tayari zimebuniwa na zinatumika sasa duniani kwa sababu mfumo wa kitabia wa mbu sasa umebadilika," taarifa hiyo inamnukuu mmoja wa wanasayansi walioshiriki katika utafiti huo, Profesa George Christophides.
"Ni wakati wa wataalamu wa afya duniani kukaa chini na kuchunguza zaidi jamii hizo ili kuibua njia mpya za kujikinga na ugonjwa huo." alisisitiza.
Kutofautiana huko kibaiolojia, wanasayansi hao wanasema hata dawa za kuua mbu pamoja na mazalia yake zinapaswa kufanyiwa marekebisho, ili ziweze kuua jamii zote.
Katika nchi nyingi za Afrika, Tanzania ikiwa miongoni, zimekuwa zikitumia dawa aina ya pyrethroids kwenye vyandarua ili kukabiliana na mbu waenezao malaria kwa maelezo kwamba wana tabia ya kuuma binadamu usiku wa manane.