Mbozi vs Kongwa, analysis by Malisa GJ

Inside10

JF-Expert Member
May 20, 2011
25,792
23,273
MBOZI vs KONGWA.!
Katika "uteuzi na utenguzi" wa wakuu wa wilaya unaoendelea, kuna baadhi ya vitu nimevinote kwny wilaya hizi mbili ambavyo vimeniacha na maswali kadhaa.

# MBOZI ;
Tuanze na Mbozi. Jana DC wa wilaya hiyo Ndg.Ally Maswanya aliamua kujiuzulu nafasi hiyo aliyoteuliwa siku chache zilizopita. Maswanywa anakuwa DC wa pili wa Mbozi kujiuzulu ndani ya kipindi cha miaka minne. Mwaka 2012 aliyekua DC wa Mbozi Ndg.Gabriel Kimolo nae alijiuzulu nafasi hiyo. Mwaka 2013, Tarehe 9 December Kimolo
alitangaza kujiunga na CHADEMA, katika kongamano liliofanyika Riverside
Ubungo jijini Dar. So alianza Kimollo sasa Maswanya.

Wote Mbozi. Kwanini? Watu wengi wanahoji kwanini Maswanya hakujiuzulu kabla ya kula kiapo? Lakini mimi nahoji kwanini Rais amhamishe DC wa Kongwa kwenda Mbozi halafu Kongwa isubiri uteuzi mpya, kwanini Mbozi ndio isingesubiri uteuzi mpya? Sio kwamba nakosoa mamlaka ya uteuzi ila nawaza tu katika "ujinga" wangu.!

# KONGWA
Kongwa nako kumetokea "the posibility of imposibility". Ktk kura za maoni Kongwa (CCM) Mhe.Job Ndugai alichuana vikali na Dr.John Chilongani, John Palingo (na wengine). Yapo madai kuwa hakukuwa na maelewano mazuri kati ya mahasimu hawa watatu kisiasa.

Japo ni jambo la kawaida ktk siasa kutofautiana kidogo hasa kama mnatafuta nafasi moja lakini Kongwa ilikua tofauti kdg maana Mhe.Spika alimtandika bakora Dr.Chilongani hadi kuzirai kwa muda. Kinacholeta maswali ni wapinzani wawili wa Mhe.Ndugai (Palingo naChilongani) wote kuteuliwa ukuu wa wilaya.

Chilongani ameteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Meatu mkoani Simiyu na Palingo aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya Kongwa kabla ya kuhamishwa jana kwenda Mbozi kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Ndg.Maswanya. Mpinzani mwingine wa kisiasa wa Ndugai anadaiwa kuwa Ndg.Simon Ngatunga. Hata sababu za Ndugai kumtandika Chilongani, ni mzozo kati ya Ndugai na Ngatunga.

Dr.Chilongani alimua kuwarekodi (kwa simu yake) wakizozana ndipo Ndugai akakasirishwa na kitendo hicho, hivyo kuahirisha mzozo wake na Ngatunga na kwenda kumvaa Chilongani.

Ndugu Ngatunga ambaye alikua mtumishi wa Halmashauri ya
Kongwa kwa sasa amepandishwa cheo kuwa Afisa Biashara Mkoa wa
Dodoma. Mwingine ni Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kongwa Bi.Lilian Matinga. Huyu nae inadaiwa kuwa waliwahi kutofautiana na Mhe.Ndugai, na ilifikia hatua ya kumtisha kwamba atamuondoa Kongwa. Huyu nae ameteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Mpanda huko mkoani Katavi.

# Swali; Kwanini watu wote waliojaribu "kumsumbua" Mhe.Spika pale Kongwa wamepewa "ulaji?". Is somebody seeking for sympathy orsomething?

Karibu tujadili.!
 
MBOZI vs KONGWA.!
Katika "uteuzi na utenguzi" wa wakuu wa wilaya unaoendelea, kuna baadhi ya vitu nimevinote kwny wilaya hizi mbili ambavyo vimeniacha na maswali kadhaa.
# MBOZI ;
Tuanze na Mbozi. Jana DC wa wilaya hiyo Ndg.Ally Maswanya aliamua kujiuzulu nafasi hiyo aliyoteuliwa siku chache zilizopita. Maswanywa anakuwa DC wa pili wa Mbozi kujiuzulu ndani ya kipindi cha miaka minne. Mwaka 2012 aliyekua DC wa Mbozi Ndg.Gabriel Kimolo nae alijiuzulu nafasi hiyo. Mwaka 2013, Tarehe 9 December Kimolo
alitangaza kujiunga na CHADEMA, katika kongamano liliofanyika Riverside
Ubungo jijini Dar. So alianza Kimollo sasa Maswanya.
Wote Mbozi. Kwanini? Watu wengi wanahoji kwanini Maswanya hakujiuzulu kabla ya kula kiapo? Lakini mimi nahoji kwanini Rais amhamishe DC wa Kongwa kwenda Mbozi halafu Kongwa isubiri uteuzi mpya, kwanini Mbozi ndio isingesubiri uteuzi mpya? Sio kwamba nakosoa mamlaka ya uteuzi ila nawaza tu katika "ujinga" wangu.!
# KONGWA
Kongwa nako kumetokea "the posibility of imposibility". Ktk kura za maoni Kongwa (CCM) Mhe.Job Ndugai alichuana vikali na Dr.John Chilongani, John Palingo (na wengine). Yapo madai kuwa hakukuwa na maelewano mazuri kati ya mahasimu hawa watatu kisiasa. Japo ni jambo la kawaida ktk siasa kutofautiana kidogo hasa kama mnatafuta nafasi moja lakini Kongwa ilikua tofauti kdg maana Mhe.Spika alimtandika bakora Dr.Chilongani hadi kuzirai kwa muda. Kinacholeta maswali ni wapinzani wawili wa Mhe.Ndugai (Palingo na
Chilongani) wote kuteuliwa ukuu wa wilaya. Chilongani ameteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Meatu mkoani Simiyu na Palingo aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya Kongwa kabla ya
kuhamishwa jana kwenda Mbozi kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Ndg.Maswanya. Mpinzani mwingine wa kisiasa wa Ndugai anadaiwa kuwa Ndg.Simon
Ngatunga. Hata sababu za Ndugai kumtandika Chilongani, ni mzozo kati ya Ndugai na Ngatunga. Dr.Chilongani alimua kuwarekodi (kwa simu yake) wakizozana ndipo Ndugai akakasirishwa na kitendo hicho, hivyo kuahirisha mzozo wake na Ngatunga na kwenda kumvaa Chilongani. Ndugu Ngatunga ambaye alikua mtumishi wa Halmashauri ya
Kongwa kwa sasa amepandishwa cheo kuwa Afisa Biashara Mkoa wa
Dodoma. Mwingine ni Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kongwa Bi.Lilian Matinga. Huyu nae inadaiwa kuwa waliwahi kutofautiana na Mhe.Ndugai, na ilifikia hatua ya kumtisha kwamba atamuondoa Kongwa. Huyu nae ameteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Mpanda huko mkoani Katavi.
# Swali; Kwanini watu wote waliojaribu "kumsumbua" Mhe.Spika pale Kongwa wamepewa "ulaji?". Is somebody seeking for sympathy orsomething?

Karibu tujadili.!
Mkuu kwa mbozi ni ma dc wengi wata wachia ngazi au kutumbuliwa, mbozi ipo chini ya cdm na wananchi wake wamejielewa kupita maelezo
 
Mkuu kwa mbozi ni ma dc wengi wata wachia ngazi au kutumbuliwa, mbozi ipo chini ya cdm na wananchi wake wamejielewa kupita maelezo
Kwa kweli mkuu na ukizingatia wanyiha kule hawataki ubabaishaji na kuendeshwa hovyo.

Naona Maswanya aliligundua hilo mapema.
 
Hivi nini sababu hasa ya huyu jamaa kujiuzulu mapema hivi,ingawa namsifu kwa ujasiri na msimamo wake
 
  • Thanks
Reactions: cmp
Mk
Nasubiri speaker wangu ndugai ambaye apone[/QUOTE
Mkuu kuna kupona tena kweli.kwa hizi figisu inaonekana ni mpango mahsusi. Ee Mungu mwepushe na balaa lolote. Tangu wakati wa sakata la Seth na Rugemalira bungeni, huyu bwana afya yake inazorota kila uchao. Mungu mpiganie Ndungai
 
Tatizo anapata matibabu yasiyo sahihi, badala ya kwenda kwa babu wa Loliondo yeye kaenda India, huko wanaharibu akili tu, akirudi atakuwa kama yule daktari wa sheri ya a.
Angeenda kwa Prophet T B Joshua, yote yangekwishne na siyo babu wa Loliondo, no charges ila ni nauli yako tu na anarudi nzima!! when Servants of God speak forth, the wise listen!
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom