MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Amani iwe kwenu wajumbe!
Tunaposema upinzani katika nchi hii bado sana ieleweke kwamba bado mbichi kweli kweli hata uwezo wa kuendesha nchi bado.
Mbowe kama kiongozi Mkuu wa kambi Rasmi ya upinzani na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha upinzani ulitakiwa kukataa hila za wazi wazi za Bwana mdogo Sabaya kukupora ushindi kwa namna yeyote ile. Hukuwapanga wananchi wako vizuri kukataa upuuzi wa aina yeyote ile, ni bora mngegawana kesi kuliko kuporwa uchaguzi.
Ulitakiwa uwe mkali na jeuri pamoja na mbabe. Naamini njia zote za wizi ulikua unazijua ulitakiwa kuzizuia kila mahali. Kama kweli DC na timu yake ndio walikua wanahujumu uchaguzi basi ungeionyesha dunia kua hutaki Upumbavu hata kama ni kwenda jela. Wewe mtu anakuja kwako usiku usiku na watu wasiojielewa anabeba walinzi wako unalia lia,kwanini usingemalizana naye usiku huo huo?
Kule south Afrika na power yako ashinde Malema kwenye jimbo lake halafu upore ushindi wake uone, nenda pale Mombasa ashinde Hassan Joho halafu upore ushindi wake uone kitakachotokea.
Mbowe wewe ni business man huna uchungu wowote na maisha ya wananchi acha kupigia watu kelele. Ninyi watu wa fursa siyo wanasiasa.Kwa hali iliyotokea kabla ya matokeo kutoka mlitakiwa kuwa jela wote kwa kuukataa Upumbavu.
Eti mpo mtaani mnalia lia mnataka kuitisha maandamano? Muitishe maandamano wakati tayari mmeshashindwa na washindi wametangazwa ni ujinga. Mlitakiwa mzuie ushindi huo wa Magumashi kwa namna yoyote ile.
Endeleeni kulia lia CCM iwe inawapangia majimbo ya kushinda. Isipoamua kuwapa jimbo hata moja hapati kweli. Huu ni udhaifu mkubwa sana kwetu, hamna uchungu wowote na raia wote watu fursa tu.
Tunaposema upinzani katika nchi hii bado sana ieleweke kwamba bado mbichi kweli kweli hata uwezo wa kuendesha nchi bado.
Mbowe kama kiongozi Mkuu wa kambi Rasmi ya upinzani na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha upinzani ulitakiwa kukataa hila za wazi wazi za Bwana mdogo Sabaya kukupora ushindi kwa namna yeyote ile. Hukuwapanga wananchi wako vizuri kukataa upuuzi wa aina yeyote ile, ni bora mngegawana kesi kuliko kuporwa uchaguzi.
Ulitakiwa uwe mkali na jeuri pamoja na mbabe. Naamini njia zote za wizi ulikua unazijua ulitakiwa kuzizuia kila mahali. Kama kweli DC na timu yake ndio walikua wanahujumu uchaguzi basi ungeionyesha dunia kua hutaki Upumbavu hata kama ni kwenda jela. Wewe mtu anakuja kwako usiku usiku na watu wasiojielewa anabeba walinzi wako unalia lia,kwanini usingemalizana naye usiku huo huo?
Kule south Afrika na power yako ashinde Malema kwenye jimbo lake halafu upore ushindi wake uone, nenda pale Mombasa ashinde Hassan Joho halafu upore ushindi wake uone kitakachotokea.
Mbowe wewe ni business man huna uchungu wowote na maisha ya wananchi acha kupigia watu kelele. Ninyi watu wa fursa siyo wanasiasa.Kwa hali iliyotokea kabla ya matokeo kutoka mlitakiwa kuwa jela wote kwa kuukataa Upumbavu.
Eti mpo mtaani mnalia lia mnataka kuitisha maandamano? Muitishe maandamano wakati tayari mmeshashindwa na washindi wametangazwa ni ujinga. Mlitakiwa mzuie ushindi huo wa Magumashi kwa namna yoyote ile.
Endeleeni kulia lia CCM iwe inawapangia majimbo ya kushinda. Isipoamua kuwapa jimbo hata moja hapati kweli. Huu ni udhaifu mkubwa sana kwetu, hamna uchungu wowote na raia wote watu fursa tu.