Elections 2010 Mbowe: Tutashirikiana na Kambi ya Upinzani Bungeni

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA amesema, Chama chake kiko tayari kushirikiana na vyama vingine vya upinzani bungeni vyenye nia ya dhati ya kufanya hivyo.

Amesema, kwa maana hiyo CHADEMA imeacha milango wazi katika ushirikiano wa kumpata mgombea Uspika toka kambi ya Upinzani na pia kupata Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Kamanda Mbowe amesema, CHADEMA imedhamiria kutumia nafasi yake Bungeni kama official opposition party kuiwajibisha serikali kwa nguvu zaidi hasa katika suala zima la matumizi mabovu ya pesa na kuleta maendeleo. Amesema, kazi iliyofanywa na wabunge wa CHADEMA katika Bunge lililopita itaendelezwa kwa nguvu zote katika Bunge la sasa.

Kamanda Mbowe aliyasema hayo katika mahojiano na Elisha Elia mtangazaji wa TBC1 muda mfupi kabla ya yeye na Wabunge wengine wa CHADEMA kuelekea Dodoma tayari kwa shughuli zitakazoanza kesho.

Mbowe mesema Kamati kuu ya CHADEMA itakutana Dodoma na kujadili masuala muhimu kuhusiana na Bunge hili likiwepo suala la uteuzi wa Mgombea USpika na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani.

Baada ya mahojiano hayo Mh. Mbowe, Dr. Slaa na Wabunge wa CHADEMA waliongozana kwa magari kuelekea Dodoma huku Bendera za CHADEMA zikionekana zinapepea.

Mpiganaji Mkuu na Kamanda wa Majeshi ya Ardhini Dr. Wilbrod Slaa alionekana akiongea na Mzee wa Siku Mteule Ndesamburo huku wote wakionekana wenye afya njema na huku sura ya Dr. Slaa ikiwa na tabasamu lenye haiba.

Source: TBC1 News Bulletin ya Saa 2.00 Usiku.

Naomba kuwakilisha.
 
Ni jambo jema sana kwa afya ya upinzani kama CHADEMA wamwdhamiria kuvishirikisha vyama vingine vya upinzani katika nafasi yao kama "Official Opposition Camp". Upinzani imara utasaidia sana kuleta maendeleo ya kweli ya Nchi na kuifanya Serikali na Chama tawala visilale usingizi.
 
Kwa mantiki hii ngoma ya Marando kugombea Uspika na Zitto kugombea Uongozi wa Kambi ya Upinzani bado kitendawili. Kujulikana baada ya kikao cha Kamati Kuu.
 
Ni jambo jema sana kwa afya ya upinzani kama CHADEMA wamwdhamiria kuvishirikisha vyama vingine vya upinzani katika nafasi yao kama "Official Opposition Camp". Upinzani imara utasaidia sana kuleta maendeleo ya kweli ya Nchi na kuifanya Serikali na Chama tawala visilale usingizi.

Itapendeza kama Upinzani watamsimamisha candidate moja kogombea nafasi ya Uspika. Hamadi Rashid wa CUF au Marando could be ideally candidates.

Strategically CHADEMA watafanya vema wakimpitisha Hamadi Rashid kwani itatoa picha nzuri kwa upinzani kuwa CHADEMA wako serious kuunganisha opposition. Afterall, si rahisi kushinda unless miracle happens!
 
Itapendeza kama Upinzani watamsimamisha candidate moja kogombea nafasi ya Uspika. Hamadi Rashid wa CUF au Marando could be ideally candidates.

Strategically CHADEMA watafanya vema wakimpitisha Hamadi Rashid kwani itatoa picha nzuri kwa upinzani kuwa CHADEMA wako serious kuunganisha opposition. Afterall, si rahisi kushinda unless miracle happens!

What i m trying to count on ni kuwa, iwapo ccm watalazimisha kumpitisha chenge kama mgombea wao, kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wengi wa ccm kumpigia mgombea tofauti na wa kwao. (wana ccm wengi tu wamewapigia opposition candidates ktk uchaguzi ulioisha). Hivyo basi, CHADEMA wakimweka Marando, au wamsupport Rashid, anything may happen.
Angalizo tu, Rashid as an individual sina tatizo naye, hajawahi kuweka upinzani wake in doubt. kitendawili ni kitu gani kitakuja baada ya CUF kuuungana ccm hivi karibuni, can they be trused? wanaweza wakauza timu hawa. It's better for CHADEMA to go it alone, (kwenye uspika) kuliko kuwategemea CUF.
 
What i m trying to count on ni kuwa, iwapo ccm watalazimisha kumpitisha chenge kama mgombea wao, kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wengi wa ccm kumpigia mgombea tofauti na wa kwao. (wana ccm wengi tu wamewapigia opposition candidates ktk uchaguzi ulioisha). Hivyo basi, CHADEMA wakimweka Marando, au wamsupport Rashid, anything may happen.

Angalizo tu, Rashid as an individual sina tatizo naye, hajawahi kuweka upinzani wake in doubt. kitendawili ni kitu gani kitakuja baada ya CUF kuuungana ccm hivi karibuni, can they be trused? wanaweza wakauza timu hawa. It's better for CHADEMA to go it alone, (kwenye uspika) kuliko kuwategemea CUF.

Kuna ukweli katika maneno uliyoyasema.

Let us wait and see. TIME. TIME will tell.
 
What i m trying to count on ni kuwa, iwapo ccm watalazimisha kumpitisha chenge kama mgombea wao, kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wengi wa ccm kumpigia mgombea tofauti na wa kwao. (wana ccm wengi tu wamewapigia opposition candidates ktk uchaguzi ulioisha). Hivyo basi, CHADEMA wakimweka Marando, au wamsupport Rashid, anything may happen.
Angalizo tu, Rashid as an individual sina tatizo naye, hajawahi kuweka upinzani wake in doubt. kitendawili ni kitu gani kitakuja baada ya CUF kuuungana ccm hivi karibuni, can they be trused? wanaweza wakauza timu hawa. It's better for CHADEMA to go it alone, (kwenye uspika) kuliko kuwategemea CUF.

No Mesterdennis, Chadema to go it alone would be a big mistake, it will be the loser? Kwanini Hamad ana nafasi kubwa ya kushinda. Kwanza endepo CCM watamsimamisha Chenge basi wategemee baadhi ya wabunge wa CCm watampigia candidate wa opposition, pili, Ubara v's Uzanzibari ni jambo ambalo ndani ya CCM bado lipo na hivyo kunauwezekano mkubwa wazanzibari wakampigia Hamad, Udini kwa sasa una nafasi kubwa katika politics za Tanzania, huu ni ukweli tu na mwisho, zikipatikan kura kutoka CCM na CUF ukijumlisha na Chadema, NCCR na TLP UDP candidate wa CCM atakua ameshindwa! We have to out smart CCM in their own game! Masterdennis , you should know in politics there is no permanent enemy! Politics its about strategies.
 
Kamanda Mbowe hii ni nafasi nzuri kujenga mazingira ya nguvu kubwa ya upinzani bungeni. Lengeni kupata uspika ili pamoja na nguvu ya upinzani ya Chadema sauti yenu ilete haraka tume huru na katiba mpya. Mtu asiwatishe, wananchi ndiyo wenye kauli ya mwisho. Nguvu kubwa tuko nyuma yenu. Tumieni dhana ya nguvu ya upinzani bungeni.
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA amesema, Chama chake kiko tayari kushirikiana na vyama vingine vya upinzani bungeni vyenye nia ya dhati ya kufanya hivyo.

Amesema, kwa maana hiyo CHADEMA imeacha milango wazi katika ushirikiano wa kumpata mgombea Uspika toka kambi ya Upinzani na pia kupata Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Kamanda Mbowe amesema, CHADEMA imedhamiria kutumia nafasi yake Bungeni kama official opposition party kuiwajibisha serikali kwa nguvu zaidi hasa katika suala zima la matumizi mabovu ya pesa na kuleta maendeleo. Amesema, kazi iliyofanywa na wabunge wa CHADEMA katika Bunge lililopita itaendelezwa kwa nguvu zote katika Bunge la sasa.

Kamanda Mbowe aliyasema hayo katika mahojiano na Elisha Elia mtangazaji wa TBC1 muda mfupi kabla ya yeye na Wabunge wengine wa CHADEMA kuelekea Dodoma tayari kwa shughuli zitakazoanza kesho.

Mbowe mesema Kamati kuu ya CHADEMA itakutana Dodoma na kujadili masuala muhimu kuhusiana na Bunge hili likiwepo suala la uteuzi wa Mgombea USpika na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani.

Baada ya mahojiano hayo Mh. Mbowe, Dr. Slaa na Wabunge wa CHADEMA waliongozana kwa magari kuelekea Dodoma huku Bendera za CHADEMA zikionekana zinapepea.

Mpiganaji Mkuu na Kamanda wa Majeshi ya Ardhini Dr. Wilbrod Slaa alionekana akiongea na Mzee wa Siku Mteule Ndesamburo huku wote wakionekana wenye afya njema na huku sura ya Dr. Slaa ikiwa na tabasamu lenye haiba.

Source: TBC1 News Bulletin ya Saa 2.00 Usiku.

Naomba kuwakilisha.

Thank you very much. That is good news. Bado tunasubili statement ya Dr. Slaa (Rais wa walala hoi)
 
hembu nifahamisheni, dr. Slaa anakwenda dodoma kama nani? Kwani yeye ni mbunge? Na inamaana sasa slaa amekubali matokeo na kuitambua serikali ya ccm? Kama hajaitambua bado inakuaje chadema waende dodoma? Unapohudhuria vikao vya bunge ni lazima ujadili bajeti ya serikali na kama huitambui serikali yenyewe hapo ni kichekesho!!!

chadema ni lazima wawe na msimamo ili wananchi tusiyumbe! Kama slaa hajakubali matokeo mbona anaelekea dodoma kwenye bunge?

naomba ufafanuzi hapa!!
 
What i m trying to count on ni kuwa, iwapo ccm watalazimisha kumpitisha chenge kama mgombea wao, kuna uwezekano mkubwa wa wabunge wengi wa ccm kumpigia mgombea tofauti na wa kwao. (wana ccm wengi tu wamewapigia opposition candidates ktk uchaguzi ulioisha). Hivyo basi, CHADEMA wakimweka Marando, au wamsupport Rashid, anything may happen.
Angalizo tu, Rashid as an individual sina tatizo naye, hajawahi kuweka upinzani wake in doubt. kitendawili ni kitu gani kitakuja baada ya CUF kuuungana ccm hivi karibuni, can they be trused? wanaweza wakauza timu hawa. It's better for CHADEMA to go it alone, (kwenye uspika) kuliko kuwategemea CUF.
Ni kweli Chadema needs to be so cautious in this matter,vinginevyo italeta matokeo yasiyotarajiwa.Nafikiri itakuwa vizuri watathmini upepo ukoje pia kwa hao wabunge wa ccm ili waweze kujua kama mpango wao unaweza kufanikiwa vinginevyo bora wao wasiweke mgombea wakaweka support kwa mgombea wa ccm aliye bora zaidi.Mfano kwa wagombea wa ccm waliojitokeza ni bora six akarudi hao wengine hawana maana kabisa.
 
hembu nifahamisheni, dr. Slaa anakwenda dodoma kama nani? Kwani yeye ni mbunge? Na inamaana sasa slaa amekubali matokeo na kuitambua serikali ya ccm? Kama hajaitambua bado inakuaje chadema waende dodoma? Unapohudhuria vikao vya bunge ni lazima ujadili bajeti ya serikali na kama huitambui serikali yenyewe hapo ni kichekesho!!!

chadema ni lazima wawe na msimamo ili wananchi tusiyumbe! Kama slaa hajakubali matokeo mbona anaelekea dodoma kwenye bunge?

naomba ufafanuzi hapa!!

take time to read brother uliposoma Slaa anaenda Dodoma pia imeandikwa "Mbowe mesema Kamati kuu ya CHADEMA itakutana Dodoma na kujadili masuala muhimu kuhusiana na Bunge hili likiwepo suala la uteuzi wa Mgombea USpika na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani" So nadhani unajua kuwa Slaa ni sehemu ya kamati kuu
 
Mbunge anawajibu wa kuwawakilisha walio mchagua. Kuto kwenda bungeni ni kuwasaliti waliokupigia kura. Slaa kwenda bungeni haimaanishi kakubali matokeo Kwani kura ya raisi ilipigwa tofauti na ya mbunge. Katiba ya Tanzania hairuhusu kwenda mahakamani kurekebisha matokeo ya raisi. Ila waweza rekebisha matokeo ya ubunge kwenda bungeni haimaanishi umekubali matokeo ya baadhi ya viti Vya ubunge
 
Ni kweli Chadema needs to be so cautious in this matter,vinginevyo italeta matokeo yasiyotarajiwa.Nafikiri itakuwa vizuri watathmini upepo ukoje pia kwa hao wabunge wa ccm ili waweze kujua kama mpango wao unaweza kufanikiwa vinginevyo bora wao wasiweke mgombea wakaweka support kwa mgombea wa ccm aliye bora zaidi.Mfano kwa wagombea wa ccm waliojitokeza ni bora six akarudi hao wengine hawana maana kabisa.

Thanks. You said it all.
 
Thank you very much. That is good news. Bado tunasubili statement ya Dr. Slaa (Rais wa walala hoi)

Seems like this time Tanzania ina Ma-Ris wawili:

1. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na
2, Rais wa Watu wa Tanzania

Usishange kuona no.2 anakuwa more popular hasa pale no.1 atakapokuwa anfanya blunders.

Wachangiaji wengi JF wamekuwa wanam-refer Dr. Slaa kama "Rais wangu", "Rais wa ukweli", "Rais wa watu", nk.
 
While it's a good idea for opposition in the union parliament to join hands and fight for the common cause, the political atmosphere in Zanzibar at present leaves one with a lot of questions on reliability of CUF as credible opposition.

Sote tunajua kuwa CUF ina nguvu zaidi Zanzibar na hivyo ingawa Lipumba ni m/kiti, ushawishi wa viongozi kutoka ZNZ ndani ya CUF ni mkubwa zaidi hasa ukizingatia kuwa wao sasa ni sehemu ya dola wakiwa na nguvu zaidi ya kisiasa na hata kiuchumi

Itakuwaje inapotakiwa kutoa msimamo wa upinzani ktk jambo ambalo serikali ya muungano CCM na serikali mseto CCM na CUF zina maslahi?

Niliwahi kusoma kwenye MWANAHALISI, ilielezwa kuwa CHADEMA waliomba CUF itoe mgombea mwenza na CHADEMA itoe mgombea urais ili washirikiane, lakini wakati hilo linajadiliwa, Kikwete aliwapigia simu viongozi CUF zanzbr na kuwaambia kama wanataka kweli kuunda serikali ya pamoja visiwani na CCM, waondoe wazo la kuungana na CHADEMA bara vinginevyo watakosa kote. Akina Maalim Seif kwa kulinda "kitumbua chao" wakafuta wazo la kuungana na CHADEMA. Je, hili la mgongano wa maslahi haliwezi kujirudia ndani ya bunge?

Isitoshe,wapinzani wengine kama Mrema, Cheyo, Mbatia "wameshachakachuliwa". Hawa badala ya kuunga mkono wapinzani wenzao, wamekuwa wakiwasakama na huku wakiisifia CCM na Kikwete. Je? Hawa ni wa kuungana nao? Au mnataka bora wingi,muonekane mnafika 100 huku mamluki kibao kati yenu?
 
Well well well, ni sentensi chache alizoongea Mbowe, lakini zilizojaa busara na hekima. Thats why I like that man...
 
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA amesema, Chama chake kiko tayari kushirikiana na vyama vingine vya upinzani bungeni vyenye nia ya dhati ya kufanya hivyo.

Amesema, kwa maana hiyo CHADEMA imeacha milango wazi katika ushirikiano wa kumpata mgombea Uspika toka kambi ya Upinzani na pia kupata Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Kamanda Mbowe amesema, CHADEMA imedhamiria kutumia nafasi yake Bungeni kama official opposition party kuiwajibisha serikali kwa nguvu zaidi hasa katika suala zima la matumizi mabovu ya pesa na kuleta maendeleo. Amesema, kazi iliyofanywa na wabunge wa CHADEMA katika Bunge lililopita itaendelezwa kwa nguvu zote katika Bunge la sasa.

Kamanda Mbowe aliyasema hayo katika mahojiano na Elisha Elia mtangazaji wa TBC1 muda mfupi kabla ya yeye na Wabunge wengine wa CHADEMA kuelekea Dodoma tayari kwa shughuli zitakazoanza kesho.

Mbowe mesema Kamati kuu ya CHADEMA itakutana Dodoma na kujadili masuala muhimu kuhusiana na Bunge hili likiwepo suala la uteuzi wa Mgombea USpika na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani.

Baada ya mahojiano hayo Mh. Mbowe, Dr. Slaa na Wabunge wa CHADEMA waliongozana kwa magari kuelekea Dodoma huku Bendera za CHADEMA zikionekana zinapepea.

Mpiganaji Mkuu na Kamanda wa Majeshi ya Ardhini Dr. Wilbrod Slaa alionekana akiongea na Mzee wa Siku Mteule Ndesamburo huku wote wakionekana wenye afya njema na huku sura ya Dr. Slaa ikiwa na tabasamu lenye haiba.

Source: TBC1 News Bulletin ya Saa 2.00 Usiku.

Naomba kuwakilisha.


I wish to read that again and again and again and again... Kwa kweli tuna Mwenyekiti...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom