Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Huu ndiyo ukweli na haihitaji kufanya utafiti wa ndani kujuwa hili kwa Mh.Freeman Mbowe, Mwenyekiti m-babe wa chadema, kiongozi wa upinzani bungeni na mfanyabiashra wa kibepari Tanzania akiwa ni Mkwe wa muasisi wa chadema, mzee E.Mtei ni mbumbumbu wa historia ya nchi yake ama mkaidi tu .
Mbowe ni mbumbumbu wa historia ya Tanzania au mbishi tu, kusema la haki sina hakika na elimu yake siwezi kusema chochote katika hilo lakini kwa kauli yake mwenyewe kathibitisha kuwa hana uelewa wa kutosha wa baadhi ya mambo ya msingi ya historia ya nchi hii ua ubishi tu.
Kwa kauli yake Mh. Mbowe amesema au amenukuliwa kusema kuwa " ... Mh. Idriss Abdulwakyl Nombe (late), alikuwa na elimu ya darasa la saba...".
Marehemu Mzee Wakyl alikuwa rais wa Zanzibar wa awamu ya nne na makamo wa rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania 1985-90.
Awali nilidhani kuwa Mh. Mbowe ameghafilika,hivyo waungwana wakamkumbusha Mh. Mbowe kuwa kauli yake aliikosea na kiungwana tu awaombe radhi familia ya marehemu kwa kauli yake hiyo ya bahati mbaya. Kwakuwa ukweli ni kuwa Mzee Idriss Abudulwakyl alikuwa ni msomi wa ngazi ya chuo kikuu Makerere Uganda, chuo kile kile alichosoma Nyerere na wasomi wengine wa Tanzania,hilo Mh. Mbowe halijuwi wala hajawahi kulisikia na akadai kuwa anataka kufanya utafiti ndiyo aombe radhi.
Mbowe ameenda mbali zaidi kwa kukataa kuwa amekosea na kushikilia msimamo wake wa kukataa kuomba radhi wanafamilia ya mzee wakyl na hata taasisi alizotumikia.
Mh. Mbowe amesahau kuwa Wakyl alikuwa kiongozi wa kitaifa, ambaye anastahili heshima na hadhi kama viongozi wengine wa kitaifa waliotangulia mbele ya haki.
Anaposhikilia kauli yake ya kumbeza, kumdharau na kumtoa thamani kwa kauli kama hiyo ajuwe kuwa anawatukana na kuwatoa thamani wananchi ambao walimuamini kuwa kiongozi wao na kumuheshimu wakati na baada ya uongozi wake.
Ushauri wa bure kwa Mbowe, kuwa ukaidi wake hauwezi kumfanya masikini wa fedha kusema kweli, lakini heshima yake kama kiongozi wa kitaifa asiyeheshimu viongozi wenzake wa kitaifa itapotea na wananchi watamdharau.
Namkumbusha kuwa kutafuta uaduwi na watu si vyema, asisahau jinsi Mh Mizengo Pinda alivyoivua heshima yake kwa wazanzibari kama nyoka anavyovuwa kanzu yake, kwa Zanzibar Pinda si chochote si lolote hata viongozi wa chama chake huku wanamuona "kojoz" tu.
Hivyo, mbowe asitake hayo yamkute, chama chake hakijuulikani huku, naye anahitaji kishike dola, akubali kuwa amekosea na kuwaomba radhi si CCM bali wanafamilia wa Mzee Idriss na wananchi wa Zanzibar na Tanzania ambao wanawaenzi na kuwaheshimu viongzi wao wa kitaifa.
Mbowe ni mbumbumbu wa historia ya Tanzania au mbishi tu, kusema la haki sina hakika na elimu yake siwezi kusema chochote katika hilo lakini kwa kauli yake mwenyewe kathibitisha kuwa hana uelewa wa kutosha wa baadhi ya mambo ya msingi ya historia ya nchi hii ua ubishi tu.
Kwa kauli yake Mh. Mbowe amesema au amenukuliwa kusema kuwa " ... Mh. Idriss Abdulwakyl Nombe (late), alikuwa na elimu ya darasa la saba...".
Marehemu Mzee Wakyl alikuwa rais wa Zanzibar wa awamu ya nne na makamo wa rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania 1985-90.
Awali nilidhani kuwa Mh. Mbowe ameghafilika,hivyo waungwana wakamkumbusha Mh. Mbowe kuwa kauli yake aliikosea na kiungwana tu awaombe radhi familia ya marehemu kwa kauli yake hiyo ya bahati mbaya. Kwakuwa ukweli ni kuwa Mzee Idriss Abudulwakyl alikuwa ni msomi wa ngazi ya chuo kikuu Makerere Uganda, chuo kile kile alichosoma Nyerere na wasomi wengine wa Tanzania,hilo Mh. Mbowe halijuwi wala hajawahi kulisikia na akadai kuwa anataka kufanya utafiti ndiyo aombe radhi.
Mbowe ameenda mbali zaidi kwa kukataa kuwa amekosea na kushikilia msimamo wake wa kukataa kuomba radhi wanafamilia ya mzee wakyl na hata taasisi alizotumikia.
Mh. Mbowe amesahau kuwa Wakyl alikuwa kiongozi wa kitaifa, ambaye anastahili heshima na hadhi kama viongozi wengine wa kitaifa waliotangulia mbele ya haki.
Anaposhikilia kauli yake ya kumbeza, kumdharau na kumtoa thamani kwa kauli kama hiyo ajuwe kuwa anawatukana na kuwatoa thamani wananchi ambao walimuamini kuwa kiongozi wao na kumuheshimu wakati na baada ya uongozi wake.
Ushauri wa bure kwa Mbowe, kuwa ukaidi wake hauwezi kumfanya masikini wa fedha kusema kweli, lakini heshima yake kama kiongozi wa kitaifa asiyeheshimu viongozi wenzake wa kitaifa itapotea na wananchi watamdharau.
Namkumbusha kuwa kutafuta uaduwi na watu si vyema, asisahau jinsi Mh Mizengo Pinda alivyoivua heshima yake kwa wazanzibari kama nyoka anavyovuwa kanzu yake, kwa Zanzibar Pinda si chochote si lolote hata viongozi wa chama chake huku wanamuona "kojoz" tu.
Hivyo, mbowe asitake hayo yamkute, chama chake hakijuulikani huku, naye anahitaji kishike dola, akubali kuwa amekosea na kuwaomba radhi si CCM bali wanafamilia wa Mzee Idriss na wananchi wa Zanzibar na Tanzania ambao wanawaenzi na kuwaheshimu viongzi wao wa kitaifa.