iron finger
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 358
- 220
Habari za jioni wakuu,
nimeona nidondoke upya tena hapa jukwaani kueleza kwa kina hasa yale yaliyo moyoni na pia yanayokisibu chama changu pendwa CHADEMA
Kama ni mtafiti huru wa siasa za nchi yetu utaweka fikra zako juu ya mustakabali wa CHADEMA na kama ni mkweli na huru wa fikra hutakawia kujua anguko zito ambalo CHADEMA wasipobadilika litawakumba
Tukianzia bungeni wabunge wengi wa CHADEMA wameanza kujisahau na hasa kusahau kilichowapeleka bungeni na kushindwa kutetea maslahi na maendeleo ya majimbo yao,wengi sasa wamejikita katika kuendesha hoja zao binasfi na sio za chama tena hapa nawazungumzia wale machachari kama Zitto, Mnyika, Wenje, Sugu na wasemaji wengine. Kazi ya kubeba chama imebaki kwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mh. Mbowe ambaye peke yake ndio anapigania maslahi ya chama, pia wapo wabunge wa chama ambao hawana msaada wowote katika kazi na hata hoja za chama bungeni wao wameshashindwa na wanasubiri tu mwaka ujao wa uchaguzi wakabidhi majimbo kwa CCM hawa ni kama kina Machemli, Kasulumabayi, Dr Mbasa na profesa Kahigi wakiwepo pia wengi wa viti maalum ambao hawabebi ajenda yeyote ya chama bungeni hivyo kuifanya sasa CHADEMA ionekane ya kawaida sana bungeni kwa hiyo kwa upande wa bunge ni kama wabunge wote wa CHADEMA wamemsusia Mbowe na kumfanya yeye peke yake abebe chama akisaidiwa kidogo na Mh Lissu
Katika kazi za nje za chama napo kuna mgomo baridi kwa mtazamo wangu kawa sasa kurugenzi zote za chama zimelala pono nahisi ni hangover za uchaguzi uliopita wakuregenzi wengi hasa baada ya kukabidhiwa mashangingi wapo busy kuandaa majimbo ya uchaguzi na kusahau shughuli za kujenga chama hali ambayo inamfanya katibu mkuu Dr Slaa awe peke yake katika kubeba ajenda za chama hapa wakurugenzi walio kwenye mgomo ni kama kina Kigaila, Lwakatare, Mrema na Komu, wote sasa hawafikirii chama na badala yake wanawaza hatma zao kisiasa.
Nasema hayo kwa uchungu mkubwa na ndio maana nikaleta utafiti huu hapa jamvini ili wajitekebishe na kuokoa chama chetu pendwa dhidi ya anguko linalokuja na tuache kuwasusia Mbowe na Slaa wao peke yao ndio wabebe ajenda za chama
Nitasema ukweli daima
nimeona nidondoke upya tena hapa jukwaani kueleza kwa kina hasa yale yaliyo moyoni na pia yanayokisibu chama changu pendwa CHADEMA
Kama ni mtafiti huru wa siasa za nchi yetu utaweka fikra zako juu ya mustakabali wa CHADEMA na kama ni mkweli na huru wa fikra hutakawia kujua anguko zito ambalo CHADEMA wasipobadilika litawakumba
Tukianzia bungeni wabunge wengi wa CHADEMA wameanza kujisahau na hasa kusahau kilichowapeleka bungeni na kushindwa kutetea maslahi na maendeleo ya majimbo yao,wengi sasa wamejikita katika kuendesha hoja zao binasfi na sio za chama tena hapa nawazungumzia wale machachari kama Zitto, Mnyika, Wenje, Sugu na wasemaji wengine. Kazi ya kubeba chama imebaki kwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mh. Mbowe ambaye peke yake ndio anapigania maslahi ya chama, pia wapo wabunge wa chama ambao hawana msaada wowote katika kazi na hata hoja za chama bungeni wao wameshashindwa na wanasubiri tu mwaka ujao wa uchaguzi wakabidhi majimbo kwa CCM hawa ni kama kina Machemli, Kasulumabayi, Dr Mbasa na profesa Kahigi wakiwepo pia wengi wa viti maalum ambao hawabebi ajenda yeyote ya chama bungeni hivyo kuifanya sasa CHADEMA ionekane ya kawaida sana bungeni kwa hiyo kwa upande wa bunge ni kama wabunge wote wa CHADEMA wamemsusia Mbowe na kumfanya yeye peke yake abebe chama akisaidiwa kidogo na Mh Lissu
Katika kazi za nje za chama napo kuna mgomo baridi kwa mtazamo wangu kawa sasa kurugenzi zote za chama zimelala pono nahisi ni hangover za uchaguzi uliopita wakuregenzi wengi hasa baada ya kukabidhiwa mashangingi wapo busy kuandaa majimbo ya uchaguzi na kusahau shughuli za kujenga chama hali ambayo inamfanya katibu mkuu Dr Slaa awe peke yake katika kubeba ajenda za chama hapa wakurugenzi walio kwenye mgomo ni kama kina Kigaila, Lwakatare, Mrema na Komu, wote sasa hawafikirii chama na badala yake wanawaza hatma zao kisiasa.
Nasema hayo kwa uchungu mkubwa na ndio maana nikaleta utafiti huu hapa jamvini ili wajitekebishe na kuokoa chama chetu pendwa dhidi ya anguko linalokuja na tuache kuwasusia Mbowe na Slaa wao peke yao ndio wabebe ajenda za chama
Nitasema ukweli daima