Uchaguzi 2020 Mbowe, Mnyika, Tundu nje ya Bunge CHADEMA patachimbika

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

Kutokana na hali ilivyo huenda CHADEMA ikakosa Mbunge ambaye ni kiongozi Mkuu katika chama kwani Mbowe ambaye ni Mwenyekiti nafasi yake kurudi bungeni ni finyu mno kwani Wananchi wa Hai wameshamtaka akabidhi Jimbo.

Kwa upande wa Mnyika yeye alishasoma alama za nyakati akaamua kujitoa kugombea ubunge, Tundu ambaye ni makamu mwenyekiti yeye amechagua kushiriki kugombea urais huku akijua hashindi. Salum Mwalim ambaye ni kiongozi kwa upande wa Zanzibar anashiriki kwenye uchaguzi kama mgombea mwenza wa Tundu Lissu.

Ni dhahiri hao wote baada ya uchaguzi wataishi kwa kutegemea posho kutoka chamani hapa ndipo patachimbika na ukizingatia ruzuku inaenda kupungua.

Wasipo kuwa wavumilivu tutegemee watu kugawana mbao.
 
Mkuu@wakudadavua hivi pale ufipa walikufanya nini? Naona uko desperate sana na chadema.
Nyuzi zako nyingi zinahusu chadema kuliko huko uliko ccm.
Tueleze tu usitufiche
 
Jikite kwenye hoja kamanda acha kuweweseka
Mkuu@wakudadavua hivi pale ufipa walikufanya nini? Naona uko desperate sana na chadema.
Nyuzi zako nyingi zinahusu chadema kuliko huko uliko ccm.
Tueleze tu usitufiche
 
Sasa wewe ikitokea CCM tukashinda wote wabunge, wewe utafaidika nini?

Hatuombei ivo ila sasa na nyie jitahidini kuongeza ushawishi kwa wananchi basi, mambo ya sjui spana, mara matusi watu wanasubiri kuskia mtawafanyia nn, ongezeni jitahada
 
Hawa vijana hali yao ya uelewa wa masuala ni ndogo mno ndio maana wanaishia kutukana
hatuombei ivo ila sasa na nyie jitahidini kuongeza ushawishi kwa wananchi basi, mambo ya sjui spana, mara matusi watu wanasubiri kuskia mtawafanyia nn, ongezeni jitahada
 
Hakiki details za majina kwanza.
Ni vema kwa sasa kila mgombea wa udiwani afanye uhakiki wa vituo katika kata yake ili kubaini vituo hewa. Ni vema kuhakiki wapiga kura kubaini walioongezwa na kuhakikisha kuwa mawakala wanatambua vituo vyao kabla ya siku ya uchaguzi. Kila mgombea ubunge hali kadhalika afanye hivyo kwa jimbo lake. Tume imehalalisha kuingiza karatasi nyingi za kupigia kura na kudai kuwa mtu anaweza kuomba karatasi nyingine kama akibadilisha uamuzi au kuharibu ya awali. Huku ni kuhalalisha kuingiza balot papers nyingi vituoni kwa nia ya wizi. Si kuna kura zinazoharibika ambazo nazo huhesabiwa? Kuna kila dalili kuwa tume inaratibu wizi wa kura badala ya kuzuia. Kwa kusema mtu hata anaweza kutumia leseni ya udereva kupigia kura hiyo nsyo ni nini kama sio kuruhusu mwanya wa wizi wa kura???
 
Back
Top Bottom