Nkerejiwa
Senior Member
- Feb 25, 2014
- 146
- 214
MBOWE JIKAZE NA UYASIKILIZE HAYA YATAKUPONYA
Nimekaa nikasubiri kwanza kuona ni hatua Gani utachukua kamanda wangu Mwenyekiti wa CDM Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzai Bungeni Mh. Freeman Aikaeli Mbowe baada ya Tukio la Wananchi wa Wilaya ya Hai kuuliza Maswali Magumu na kupelekea Mkutano wako kuvunjika. Ni kweli inaumiza sana Mwenyekiti wa Chadema Taifa Kudhalilika namna ile. Inaonekana ni Tukio la kwanza na la aina yake ambalo limetokea katika Eneo ambalo unaamini ndio ufalme wako ulipo,
Jana katika Mkutano wako ulishtushwa na tukio lile na ukasema Wananchi wale wametoka Eneo jingine na sio wa kijiji kile. Lakini kumbuka wewe ni Mbunge wa Hai Jimbo lenye jumla ya vijiji 64, na Umefanya mikutano minne tu katika vijiji vinne. Inawezekana wananchi wa vijiji 60 ambavyo hujavifikia walikusubiri kwa Hamu sana ili wakwambie maneno hayo lakini walipogundua huo ni Mkutano wako wa Mwisho kwenye Ratiba wakaamua kukufuata hapo ulipo. Sababu tu Unapotangaza Mkutano wananchi wa Jimbo lako wana haki ya kuhudhuria bila kujali ni wa kijiji kipi.
Hoja ya picha za wananchi waliovaa mavazi ya ccm ni hoja dhaifu kuitumia katika utetezi. Hivi leo tukitaka picha ya Lema amevaa nguo ya TLP tutaipata, Au tukitafuta picha ya Muasisi wa chama cha chadema Ambaye ni Baba Mkwe wako Mzee Mtei akiwa kavaa nguo ya CCM tutaipata sababu tu tunaishi ndani ya uhuru wa kidokrasia unaweza amka Asubuhi na ukahama chama bila kuzuiwa. Ndio maana leo ukikutana na Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Vincent Mashinji utamkuta kavaa nguo ya CCM na sio Chadema.Hii hoja naiita dhaifu sababu hata hao wana CCM wanaoishi Hai wewe ni Mbunge wao.
Timu yako inayokusaidia kujibu hoja mitandaoni inazidi kukupoteza Muelekeo na kuonesha kuwa umeshindwa kuzijibu hoja za wananchi wako.
Ungejikita kusikiliza zile hoja zao na kuzijibu kwa Data na Ukweli ingeonekana hoja zao hazina maana na leo ningeendelea kukuona kama Mwanasiasa Makini wa Karne hii.
*MFANO*
*_Kuna mwananchi anaonekana kwenye Video akiuliza wewe umekua ukiwaeleza habari za Tundu lisu kupigwa Risasi, Kwani lini utakuja kuhusisha upigwaji wa Tundu lisu risasi na Zahanati ambayo uliahidi kuwaletea, Ungejibu tu hilo swali kweli ingeoneksna wale wananchi wametumwa._*
Unaposema kwamba Rais Magufuli anawanyanyasa watu wa kanda ya Kaskazini Mwananchi akakuuliza *_Rais huyo unayesema anawanyanyasa amewaletea Reli kutoka Dar mpaka Arusha na huyo mwananchi amepanda hiyo treni_* ulichopaswa ni kutoa Majibu Je ni sahihi huyo Mwananchi anachosema ni kweli au si kweli? Kisha Mwingine akauliza
*_Tuambie jambo Moja ambalo umefanya toka uchaguliwe kuwa mbunge wao_*
Majibu yalikua Rahisi sana kama kweli umefanya ungetoa Majibu tu.
Kitu ninachoamini Mbowe wewe ni Mwanasiasa ambaye uliamini Hai hakuna wa kukuuliza swali lolote linalopingana na wewe huku ukiwa umesahau kuwa Tupo katika kizazi cha kuhoji kuliko kile cha Mwanzo chenye ukimya. Tukio lililokutokea jana limekua kama Sindano ya Moto na sasa timu yako inataka kuaminisha watu kiwa wale watu wametengenezwa wakati kihalisia ukiwasikiliza walikua wanahoji Maswali ya Msingi na hoja zao zilikua na Maana.
Ni sawa kama wametengenezwa au hawajatengenezwa wale wananchi walikua na Maswali ya Msingi sana na Sura zao zilikua na ghadhabu huku zikimaanisha kile wanachozungumza ambacho kwa mtu wa kawaida aliyepangwa asingeweza kulifanya kwa jinsi walivyoonekana kwa uhalisia ule. Na Unapaswa ujitafakari zaidi kama wale watu wote walikua wanapiga kelele waliletwa kama unavyosema basi Mkutano wako ulikua na Idadi ndogo ya watu kiliko mikutano yako yote iliyopita.
Kuna Mwananchi alikuuliza *_Kwa miaka minne kwanini hujawahi kuja jimboni_* Sio kuwambia ulikua unaenda Mahakamani sababu kwenda mahakamani hakuna mahusiano na Sababu za wao kukuchagua kuwa mbunge wao.Na walikuuliza *_Kati ya hayo unayoenda Mahakamani ni yapi yanahusiana na jimbo la hai?_*
Hizi hoja zao zilipaswa kupata Majibu ya Msingi kutoka kwa watu wanaokujibia mtandaoni kuliko kuanza kutukana na kudhalilisha wapiga kura wako kwa kuwaita Walevi wakati hao ndio walipanga Mstari kukupigia kura Mwezi Oktoba 2015.
Nakushauri ukae kwa utulivu na kutafakari kwa Makini hoja za wananchi wako iwe ni wana CCM, wana CHADEMA, TLP, CHAUMA, UDP, CUF, ACT au wasio na chama na kuzipatia majibu ili kuweza kurudisha imani na heshima yako pale Hai.
Hoja za kazi ya Kitaifa na kuacha jimbo ni majibu ambayo wanaonekana wameyachoka na sasa wanahitaji kukuona ukitekeleza wajibu wako.
Nimalize kuwa kukung'ata sikio
_Inawezekana kama unavyosema Sabaya ndiye MasterMind wa hili tukio au asiwe yeye, Lakini jambo kubwa unatakiwa uwe tahadhari nalo kuhusu huyo Sabaya ni kwamba hizi ndio ligi zake, Kwahiyo wewe uachopaswa kufanya ni kuwa Makini kwa Siasa unazopeleka Hai sababu huyu Ole Sabaya kwa hulka na tabia hatokubali kazi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli na anazozifanya yeye mwenyewe hai zipotoshwe kwa siasa za bei rahisi, Athari zake ni kuzuia zile siasa za Zamani za Kikamanda na siasa za kihuni ziingie Wilayani Mwake na huyo Atakuchonganisha na wananchi maana yeye kwa hulka na Tabia ni muumini wa siasa tata na ngumu. Nakushauri Badilisha Muelekeo na Aina ya Siasa zako unapokua Jimboni._
Si unajua usemi unaosema
*UKIMUAMSHA ALIYE LALA?.…..*
Jitafakari
Ni Mimi
Mwanaharakati Huru
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekaa nikasubiri kwanza kuona ni hatua Gani utachukua kamanda wangu Mwenyekiti wa CDM Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzai Bungeni Mh. Freeman Aikaeli Mbowe baada ya Tukio la Wananchi wa Wilaya ya Hai kuuliza Maswali Magumu na kupelekea Mkutano wako kuvunjika. Ni kweli inaumiza sana Mwenyekiti wa Chadema Taifa Kudhalilika namna ile. Inaonekana ni Tukio la kwanza na la aina yake ambalo limetokea katika Eneo ambalo unaamini ndio ufalme wako ulipo,
Jana katika Mkutano wako ulishtushwa na tukio lile na ukasema Wananchi wale wametoka Eneo jingine na sio wa kijiji kile. Lakini kumbuka wewe ni Mbunge wa Hai Jimbo lenye jumla ya vijiji 64, na Umefanya mikutano minne tu katika vijiji vinne. Inawezekana wananchi wa vijiji 60 ambavyo hujavifikia walikusubiri kwa Hamu sana ili wakwambie maneno hayo lakini walipogundua huo ni Mkutano wako wa Mwisho kwenye Ratiba wakaamua kukufuata hapo ulipo. Sababu tu Unapotangaza Mkutano wananchi wa Jimbo lako wana haki ya kuhudhuria bila kujali ni wa kijiji kipi.
Hoja ya picha za wananchi waliovaa mavazi ya ccm ni hoja dhaifu kuitumia katika utetezi. Hivi leo tukitaka picha ya Lema amevaa nguo ya TLP tutaipata, Au tukitafuta picha ya Muasisi wa chama cha chadema Ambaye ni Baba Mkwe wako Mzee Mtei akiwa kavaa nguo ya CCM tutaipata sababu tu tunaishi ndani ya uhuru wa kidokrasia unaweza amka Asubuhi na ukahama chama bila kuzuiwa. Ndio maana leo ukikutana na Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Vincent Mashinji utamkuta kavaa nguo ya CCM na sio Chadema.Hii hoja naiita dhaifu sababu hata hao wana CCM wanaoishi Hai wewe ni Mbunge wao.
Timu yako inayokusaidia kujibu hoja mitandaoni inazidi kukupoteza Muelekeo na kuonesha kuwa umeshindwa kuzijibu hoja za wananchi wako.
Ungejikita kusikiliza zile hoja zao na kuzijibu kwa Data na Ukweli ingeonekana hoja zao hazina maana na leo ningeendelea kukuona kama Mwanasiasa Makini wa Karne hii.
*MFANO*
*_Kuna mwananchi anaonekana kwenye Video akiuliza wewe umekua ukiwaeleza habari za Tundu lisu kupigwa Risasi, Kwani lini utakuja kuhusisha upigwaji wa Tundu lisu risasi na Zahanati ambayo uliahidi kuwaletea, Ungejibu tu hilo swali kweli ingeoneksna wale wananchi wametumwa._*
Unaposema kwamba Rais Magufuli anawanyanyasa watu wa kanda ya Kaskazini Mwananchi akakuuliza *_Rais huyo unayesema anawanyanyasa amewaletea Reli kutoka Dar mpaka Arusha na huyo mwananchi amepanda hiyo treni_* ulichopaswa ni kutoa Majibu Je ni sahihi huyo Mwananchi anachosema ni kweli au si kweli? Kisha Mwingine akauliza
*_Tuambie jambo Moja ambalo umefanya toka uchaguliwe kuwa mbunge wao_*
Majibu yalikua Rahisi sana kama kweli umefanya ungetoa Majibu tu.
Kitu ninachoamini Mbowe wewe ni Mwanasiasa ambaye uliamini Hai hakuna wa kukuuliza swali lolote linalopingana na wewe huku ukiwa umesahau kuwa Tupo katika kizazi cha kuhoji kuliko kile cha Mwanzo chenye ukimya. Tukio lililokutokea jana limekua kama Sindano ya Moto na sasa timu yako inataka kuaminisha watu kiwa wale watu wametengenezwa wakati kihalisia ukiwasikiliza walikua wanahoji Maswali ya Msingi na hoja zao zilikua na Maana.
Ni sawa kama wametengenezwa au hawajatengenezwa wale wananchi walikua na Maswali ya Msingi sana na Sura zao zilikua na ghadhabu huku zikimaanisha kile wanachozungumza ambacho kwa mtu wa kawaida aliyepangwa asingeweza kulifanya kwa jinsi walivyoonekana kwa uhalisia ule. Na Unapaswa ujitafakari zaidi kama wale watu wote walikua wanapiga kelele waliletwa kama unavyosema basi Mkutano wako ulikua na Idadi ndogo ya watu kiliko mikutano yako yote iliyopita.
Kuna Mwananchi alikuuliza *_Kwa miaka minne kwanini hujawahi kuja jimboni_* Sio kuwambia ulikua unaenda Mahakamani sababu kwenda mahakamani hakuna mahusiano na Sababu za wao kukuchagua kuwa mbunge wao.Na walikuuliza *_Kati ya hayo unayoenda Mahakamani ni yapi yanahusiana na jimbo la hai?_*
Hizi hoja zao zilipaswa kupata Majibu ya Msingi kutoka kwa watu wanaokujibia mtandaoni kuliko kuanza kutukana na kudhalilisha wapiga kura wako kwa kuwaita Walevi wakati hao ndio walipanga Mstari kukupigia kura Mwezi Oktoba 2015.
Nakushauri ukae kwa utulivu na kutafakari kwa Makini hoja za wananchi wako iwe ni wana CCM, wana CHADEMA, TLP, CHAUMA, UDP, CUF, ACT au wasio na chama na kuzipatia majibu ili kuweza kurudisha imani na heshima yako pale Hai.
Hoja za kazi ya Kitaifa na kuacha jimbo ni majibu ambayo wanaonekana wameyachoka na sasa wanahitaji kukuona ukitekeleza wajibu wako.
Nimalize kuwa kukung'ata sikio
_Inawezekana kama unavyosema Sabaya ndiye MasterMind wa hili tukio au asiwe yeye, Lakini jambo kubwa unatakiwa uwe tahadhari nalo kuhusu huyo Sabaya ni kwamba hizi ndio ligi zake, Kwahiyo wewe uachopaswa kufanya ni kuwa Makini kwa Siasa unazopeleka Hai sababu huyu Ole Sabaya kwa hulka na tabia hatokubali kazi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli na anazozifanya yeye mwenyewe hai zipotoshwe kwa siasa za bei rahisi, Athari zake ni kuzuia zile siasa za Zamani za Kikamanda na siasa za kihuni ziingie Wilayani Mwake na huyo Atakuchonganisha na wananchi maana yeye kwa hulka na Tabia ni muumini wa siasa tata na ngumu. Nakushauri Badilisha Muelekeo na Aina ya Siasa zako unapokua Jimboni._
Si unajua usemi unaosema
*UKIMUAMSHA ALIYE LALA?.…..*
Jitafakari
Ni Mimi
Mwanaharakati Huru
Sent using Jamii Forums mobile app