Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,495
- 9,275
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema yeye na wenzake walianzisha chama hicho ili kupinga sera za ujamaa na kujitegemea zinazotumiwa na Chama cha Mapinduzi.
Akizungumza katika mwendelezo wa mahojiano yanayoitwa ‘Speaking with Tundu Lissu’ yaliyorushwa na Podcast ya Nadj Khamis, Mbowe amesema chama hicho kilianzishwa na watu wenye mtazamo wa soko huria waliopinga ukandamizwaji kiuchumi na kijamii uliokuwa umeshika kasi.
Alisema vuguvugu la mabadiliko lilikuja wakati wa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi, aliyerejesha uhuru wa kibiashara na hivyo watu wakatamani kuwa na mabadiliko kwenye nyanja ya kisiasa.
“Wakati biashara zimeruhusiwa kukawa na vuguvugu la kisiasa. Kukawa na harakati za kina Mzee Fundikira (Abdallah), harakati za Mzee Mapalala (James), kule Chuo kikuu, harakati za kina Marando (Mabere) na wengineo,” alianza kueleza Mbowe, ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa kinara kwenye siasa za Tanzania.
Ametaja makundi matatu ya mageuzi yaliyoibuka kuwa pamoja na kundi la wasomi na waliofanya kazi serikalini, akiwataja aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Naibu Gavana, Bob Makani na wengineo.
“Kundi la pili lilikuwa na wafanyabiashara ambao waliona kasi za kufanya baishara haziendani na sera za ujamaa. Kwa hiyo tulitaka kujadili sera za uchumi wa soko. Kundi la tatu lilikuwa ni la wasomi wazuri, wengine wako vyuoni, mashirika ya umma na serikalini,” alisema.
Alisema katika kundi la kwanza ndilo lililoanzisha Chadema na walimwomba Mzee Mtei kuwa Mwenyekiti wake mwaka 1991.
“Baadaye ile sheria ya vyama vingi ikapitishwa Julai 1992, wakati huo tumeshaanza kukutana. Wengi walioanzisha Chadema walikuwa watu wazima,” alisema.
“Kwa hiyo sisi tulianzisha chama tukiwa na clear policy (sera mahsusi) tunataka nini. Tulikuwa kabisa hatutaki siasa ya ujamaa. Waasisi wengine walirudi CCM, lakini kilichotuunganisha sisi tulikuwa hatukubali sera za kijamaa.
“Kwa upande mwingine, vyama vingi vilivyoanzishwa vilikuwa na sera za kijamaa, ikiwamo NCCR -Mageuzi. Ila walikuwa wanatofautiana na CCM ilikuwa ni utekelezaji wa sera,” alisema.
Chanzo: Mwananchi
Akizungumza katika mwendelezo wa mahojiano yanayoitwa ‘Speaking with Tundu Lissu’ yaliyorushwa na Podcast ya Nadj Khamis, Mbowe amesema chama hicho kilianzishwa na watu wenye mtazamo wa soko huria waliopinga ukandamizwaji kiuchumi na kijamii uliokuwa umeshika kasi.
Alisema vuguvugu la mabadiliko lilikuja wakati wa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi, aliyerejesha uhuru wa kibiashara na hivyo watu wakatamani kuwa na mabadiliko kwenye nyanja ya kisiasa.
“Wakati biashara zimeruhusiwa kukawa na vuguvugu la kisiasa. Kukawa na harakati za kina Mzee Fundikira (Abdallah), harakati za Mzee Mapalala (James), kule Chuo kikuu, harakati za kina Marando (Mabere) na wengineo,” alianza kueleza Mbowe, ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa kinara kwenye siasa za Tanzania.
Ametaja makundi matatu ya mageuzi yaliyoibuka kuwa pamoja na kundi la wasomi na waliofanya kazi serikalini, akiwataja aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Naibu Gavana, Bob Makani na wengineo.
“Kundi la pili lilikuwa na wafanyabiashara ambao waliona kasi za kufanya baishara haziendani na sera za ujamaa. Kwa hiyo tulitaka kujadili sera za uchumi wa soko. Kundi la tatu lilikuwa ni la wasomi wazuri, wengine wako vyuoni, mashirika ya umma na serikalini,” alisema.
Alisema katika kundi la kwanza ndilo lililoanzisha Chadema na walimwomba Mzee Mtei kuwa Mwenyekiti wake mwaka 1991.
“Baadaye ile sheria ya vyama vingi ikapitishwa Julai 1992, wakati huo tumeshaanza kukutana. Wengi walioanzisha Chadema walikuwa watu wazima,” alisema.
“Kwa hiyo sisi tulianzisha chama tukiwa na clear policy (sera mahsusi) tunataka nini. Tulikuwa kabisa hatutaki siasa ya ujamaa. Waasisi wengine walirudi CCM, lakini kilichotuunganisha sisi tulikuwa hatukubali sera za kijamaa.
“Kwa upande mwingine, vyama vingi vilivyoanzishwa vilikuwa na sera za kijamaa, ikiwamo NCCR -Mageuzi. Ila walikuwa wanatofautiana na CCM ilikuwa ni utekelezaji wa sera,” alisema.
Chanzo: Mwananchi