Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Baada ya wananchi wa jimbo la Hai kutaka majibu kutoka kwa Mbunge wao kwa njia ya kuhoji mkutanoni kumetokea propaganda mfu kuwa wametumwa. Hata kama wametumwa, je siyo wananchi wa Hai? Kwanini wasijibiwe kwa hoja na badala yake Mbowe na wafuasi wake wanalialia? Kwa haraka haraka nimesikia maswali yao kama ifuatavyo wakiyaelekeza kwa Mbowe:
Mh. Mbowe tuambie umetufanyia nini miaka mitano (5) jimboni kwetu?
Mh. Mbowe tangu mwaka 2015 hujawahi kufanya mkutano tukueleze kero zetu, kwanini leo?
Mh. Mbowe hatujawahi kukusikia bungeni ukiongelea chochote kuhusu wilaya ya Hai, kwanini?
Mh. Mbowe kwanini kila siku kwenye mikutano yako hapa jimboni unazungumzia Akwilina badala ya mambo yahusuyo watu wa Hai?
Hizi hoja zingepatiwa majibu ili kuwanyamazisha wananchi wa jimbo la Hai na sio kulialia na kutafuta mchawi. Kumbukeni Mbowe amekuwa Mbunge wa Hai kwa miaka kumi mfululizo kuanzia 2010 ukiacha mwaka 2000-2005. Je, maswali ya hapo juu si sawa kuulizwa?
Baada ya wananchi wa jimbo la Hai kutaka majibu kutoka kwa Mbunge wao kwa njia ya kuhoji mkutanoni kumetokea propaganda mfu kuwa wametumwa. Hata kama wametumwa, je siyo wananchi wa Hai? Kwanini wasijibiwe kwa hoja na badala yake Mbowe na wafuasi wake wanalialia? Kwa haraka haraka nimesikia maswali yao kama ifuatavyo wakiyaelekeza kwa Mbowe:
Mh. Mbowe tuambie umetufanyia nini miaka mitano (5) jimboni kwetu?
Mh. Mbowe tangu mwaka 2015 hujawahi kufanya mkutano tukueleze kero zetu, kwanini leo?
Mh. Mbowe hatujawahi kukusikia bungeni ukiongelea chochote kuhusu wilaya ya Hai, kwanini?
Mh. Mbowe kwanini kila siku kwenye mikutano yako hapa jimboni unazungumzia Akwilina badala ya mambo yahusuyo watu wa Hai?
Hizi hoja zingepatiwa majibu ili kuwanyamazisha wananchi wa jimbo la Hai na sio kulialia na kutafuta mchawi. Kumbukeni Mbowe amekuwa Mbunge wa Hai kwa miaka kumi mfululizo kuanzia 2010 ukiacha mwaka 2000-2005. Je, maswali ya hapo juu si sawa kuulizwa?