Calamity
JF-Expert Member
- May 28, 2013
- 856
- 47
...alisema pia unaweza ukawa na pesa lakini ukanunuliwa au usiwe na pesa lakini usinunuliwe....vilevile aliongeza kuwa yeye(mbowe) hana pesa lakini HANA NJAA!Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa ambaye pia ni Kiongozi Wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge Wa Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, akiwahutubia Wakazi zaidi ya Elfu Kumi na Mbili wa Jiji la Mwanza na Kanda ya Ziwa Magharibi Katika Uwanja wa Shule ya Msingi Nyamalango, Chuo Kikuu Cha SAUT Malimbe, Mh. Mbowe aliwakumbusha Watanzania Kote Nchini Kuwa, Kitendo cha CCM Kukosa Mbinu za Kumnunua ili aimalize Chadema Kama Walivyofanya Kwa Baadhi ya Watu ndani ya Chama Kinazidi Kuwaumizia Akili na Kuwafanya Wazidi Kukata tamaa Kila Kukicha. Hapa anasema "Ndg. zangu Makamanda, napenda Kuwadhibitishia Kwamba Mbowe hafiki bei na Mbowe
hanunuliki Kwa Bei yoyote, Kitendo cha Mbowe Kutofika Bei Kinawaumizi akili na Kuwafanya Waendelee Kukata tamaa Kila Kukicha, Isipokuwa anayefika Bei yao aende huko Kwetu ni aibu Kuwa naye ndani ya Taasisi hii ya Umma Watanzania, Safari hii Ilianza Zamani Kabla yetu Sote, hivyo Wapo Watakaopanda na Wapo Watakaoshuka Kwa Sababu tofauti tofauti, Kilichopo hivi sasa ni Kuufikia Mwisho Wake"
vipi mkuu ulikuwepo ktk maadamano kutoka nyamalango hadi hotelini????mimi nilikomea butimba kona aisee si unajua tena uzee unatunyemelea.....
Yule mzee aliyetoa kiwanja chake mkuyuni ili Chadema W(nyamagana) wajenge ofisi unamkumbuka??ni ndungu yangu aisee,nitafunguka siku nyingine
Chadema ni mpango wa MUNGU