Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Mbowe ataka siasa za amani, upendo zitawale
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesema siasa za amani, upendo, mshikamano na zenye hofu ya kumuogopa Mungu, ndizo zinazohitajika Tanzania. Mbowe aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Jimbo lake la Hai kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa Msikiti wa Lambo uliopo jimboni humo.
Aidha, alisisistiza suala la wananchi kujitoa katika shughuli za maendeleo ya kijamii pasipo kujali itikadi za kisiasa na kiimani.Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, alisema yeye kama kiongozi wa wananchi anapendezwa sana na siasa za amani na daima atahubiri amani na mshikamano. Alifafanua kuwa maendeleo ni suala muhimu linalomgusa kila mwananchi, hivyo inapofikia wakati wa kuangalia itikadi za kidini na vyama, itakuwa ni ngumu kuleta maendeleo ya wananchi pale inapohitajika suala la kuchangia au kushiriki katika shughuli za ujenzi wa taifa.
Katika harambee hiyo, Mbowe alichangia Shilingi milioni tano na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, aliahidi kukamilisha paa la msikiti huo pamoja na mazulia yenye thamani ya Sh. milioni 4.5 na kufanikisha kupatikana kiasi cha Sh. milioni 30 kiwango ambacho kilivuka lengo la kukusanya Sh. milioni 15. Awali, kabla ya harambee hiyo, Mbowe alifungua ofisi ya shirika lisilo la kiserikali la Hai Kilimanjaro Development Initiative (Hakidi) ambayo ilianzishwa kwa lengo la kutoa ajira kwa vijana kupitia sekta ya utalii.Akizungumza na wakazi wa mji huo wakati wa kupanda miti 10,000 na kufanya usafi katika maeneo hayo, Mbowe aliwataka wananchi hao kufanya usafi katika makazi yao na kupanda miti ili kusaidia upatikanaji wa maji.
Katika risala yake, Meneja wa shirika hilo, Mohamed Mbowe, alisema shirika lake linakusudia kuajiri vijana takribani 5,000 ambapo kwa kuanza watoa ajira kwa vijana 145 katika sekta ya utalii na wanakusudia kupanda miti milioni tatu kwa kipindi cha miaka minne ijayo.Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, alitakiwa kuwa mgeni rasmi, lakini hakutokea kutokana na kwenda kulipokea kundi lililoshuka kutoka Mlima Kilimanjaro.
Source: IPPMedia
Aidha, alisisistiza suala la wananchi kujitoa katika shughuli za maendeleo ya kijamii pasipo kujali itikadi za kisiasa na kiimani.Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, alisema yeye kama kiongozi wa wananchi anapendezwa sana na siasa za amani na daima atahubiri amani na mshikamano. Alifafanua kuwa maendeleo ni suala muhimu linalomgusa kila mwananchi, hivyo inapofikia wakati wa kuangalia itikadi za kidini na vyama, itakuwa ni ngumu kuleta maendeleo ya wananchi pale inapohitajika suala la kuchangia au kushiriki katika shughuli za ujenzi wa taifa.
Katika harambee hiyo, Mbowe alichangia Shilingi milioni tano na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, aliahidi kukamilisha paa la msikiti huo pamoja na mazulia yenye thamani ya Sh. milioni 4.5 na kufanikisha kupatikana kiasi cha Sh. milioni 30 kiwango ambacho kilivuka lengo la kukusanya Sh. milioni 15. Awali, kabla ya harambee hiyo, Mbowe alifungua ofisi ya shirika lisilo la kiserikali la Hai Kilimanjaro Development Initiative (Hakidi) ambayo ilianzishwa kwa lengo la kutoa ajira kwa vijana kupitia sekta ya utalii.Akizungumza na wakazi wa mji huo wakati wa kupanda miti 10,000 na kufanya usafi katika maeneo hayo, Mbowe aliwataka wananchi hao kufanya usafi katika makazi yao na kupanda miti ili kusaidia upatikanaji wa maji.
Katika risala yake, Meneja wa shirika hilo, Mohamed Mbowe, alisema shirika lake linakusudia kuajiri vijana takribani 5,000 ambapo kwa kuanza watoa ajira kwa vijana 145 katika sekta ya utalii na wanakusudia kupanda miti milioni tatu kwa kipindi cha miaka minne ijayo.Katika uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, alitakiwa kuwa mgeni rasmi, lakini hakutokea kutokana na kwenda kulipokea kundi lililoshuka kutoka Mlima Kilimanjaro.
Source: IPPMedia