Mbowe ashikiwa bango kutafuna milioni 800 za ujenzi wa ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_8970.PNG


Gazeti la Fahari Yetu limeandika tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, likimhusisha na matumizi ya milioni 800 za ujenzi wa jengo la ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Gazeti hilo limedai kuwa, Mbowe alikiuka Azimio la Kikao cha Kamati Kuu ya Chama na kuamua kutumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi. Inaelezwa kuwa:
  • Mbowe alinunua nyumba Dubai kwa fedha za Chama.
  • Michango ya watu binafsi kwa Chama kama akina Mzee Sobodo haijulikani zilichukuliwa lini na kwa mfumo gani na hatimaye kutumikaje.
  • Fedha zilizopatikana kupitia "Fund Raising Events" mbalimbali kama za Dar na Mwanza hazijawahi kuonekana.
  • Malalamiko kwa Mbowe kujilipa fedha kwa mnadai ya kukikopesha milioni Chama milioni 700.
  • Malalamiko dhidi ya Mbowe kukiuzia Chama magari chakavu kwa zaidi ya milioni 600 ambapo kabla ya kuyauza kwa Chama, alikuwa akiyakodisha kwa Chama.
  • Malalamiko kwa Mbowe kununua LandCruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama na kisha kukiuzia Chama.
  • Ripoti ya CAG ya 2016/2017 imeonyesha namna fedha za CHADEMA zinavyotafunwa na wajanja wachache.
Kulingana na Gazeti la Fahari, kila anapojitokeza Kiongozi yeyote ndani ya CHADEMA kuhoji juu ya matumizi ya fedha za Chama, wanajitokeza wapambe wake wa kumtetea kwa kutumia hoja za nguvu badala ya nguvu ya hoja. Hivyo kwa mtaji huo wa kujichotea fedha bila kuhojiwa ama kuulizwa chochote, Mbowe hawezi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa Chama.

IMG_8968.JPG
 
View attachment 886186

Gazeti la Fahari Yetu limeandika tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, likimhusisha na matumizi ya milioni 800 za ujenzi wa jengo la ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Gazeti hilo limedai kuwa, Mbowe alikiuka Azimio la Kikao cha Kamati Kuu ya Chama na kuamua kutumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi. Inaelezwa kuwa:
  • Mbowe alinunua nyumba Dubai kwa fedha za Chama.
  • Michango ya watu binafsi kwa Chama kama akina Mzee Sobodo haijulikani zilichukuliwa lini na kwa mfumo gani na hatimaye kutumikaje.
  • Fedha zilizopatikana kupitia "Fund Raising Events" mbalimbali kama za Dar na Mwanza hazijawahi kuonekana.
  • Malalamiko kwa Mbowe kujilipa fedha kwa mnadai ya kukikopesha milioni Chama milioni 700.
  • Malalamiko dhidi ya Mbowe kukiuzia Chama magari chakavu kwa zaidi ya milioni 600 ambapo kabla ya kuyauza kwa Chama, alikuwa akiyakodisha kwa Chama.
  • Malalamiko kwa Mbowe kununua LandCruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama na kisha kukiuzia Chama.
  • Ripoti ya CAG ya 2016/2017 imeonyesha namna fedha za CHADEMA zinavyotafunwa na wajanja wachache.
Kulingana na Gazeti la Fahari, kila anapojitokeza Kiongozi yeyote ndani ya CHADEMA kuhoji juu ya matumizi ya fedha za Chama, wanajitokeza wapambe wake wa kumtetea kwa kutumia hoja za nguvu badala ya nguvu ya hoja. Hivyo kwa mtaji huo wa kujichotea fedha bila kuhojiwa ama kuulizwa chochote, Mbowe hawezi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa Chama.

View attachment 886175
Mtapata taabu sana na Mbowe
 
Ni dalili tosha kuwa wanamuogopa sana m/kiti Mbowe,ndiyo maana hawaishi kuzua mapya na yasiyo na tija,mbona kuna mengi ya kufanya hapa duniani yenye tija kuliko mambo haya ya kizushi,na haya magazeti mnalipwa kiasi gani kwa hii kazi ya kuwachafua watu,mtambue leo mnabebwa siku zaja mtakaposimama bila hao wanaowabeba mtawajibika kwa hizi taarifa za kupakana matope
 
CCM wanataka Mbowe afanane na kina Mrema, Lipumba ama Cheyo. Hivi vyama vya kama kina Dovutwa ama Mzee Rungwe viongozi wake hata Ishirini wanafika kweli?
 
Back
Top Bottom