Mbowe apokewa na umati Busanda; FFU yautawanya!

Habarindiyohiyo

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
263
13
FFU wamimina mabomu ya machozi Msafara wa Freeman Mbowe Busanda

2009-04-22 21:49:48
Na Joseph Mwendapole


Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wamefyatua mabomu ya machozi kuwatawanya mamia ya watu waliojitokeza kumlaki Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kwenye stendi ya mabasi ya Kataro, Jimbo la Busanda mkoani Mwanza.

Tukio hilo lilitokea majira ya 12:30 jioni juzi kilomita mbili kabla ya kufika eneo la stendi hiyo, ambako wakazi hao walisukuma gari la Mbowe, lakini mwenyewe alilazimika kuteremka na kutembea kwa miguu umbali wa kilomita moja.

Huku wakiimba kibwagizo cha `Mbowe, Mbowe,` umati mkubwa wa watu ulizidi kumiminika katika stendi hiyo, hali ambayo iliwafanya polisi kuwataka wakazi hao watawanyike huku wakifyatua mabomu ya machozi kwa lengo la kuwatawanya.

Polisi walikuwa wakiwataka wakazi hao kutawanyika kwa vile hapakuwa na mkutano wa hadhara ulioruhusiwa kufanyika.
Hata hivyo, wakazi hao waligoma kutawanyika, hadi watakapomwona Mbowe.

Akiwa jukwaani, Mbowe aliwaambia polisi kwamba hawakuwa na lengo la kufanya mkutano, isipokuwa walitaka kuwasalimia wananchi waliofurika kuwapokea.

Akiwasalimia wananchi hao, Mbowe alisema Jimbo la Busanda litakuwa kama lilivyokuwa Jimbo la Tarime, ambalo Chadema kilishinda katika uchaguzi mdogo wa ubunge na kukibwaga Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichokuwa mshindani wake mkubwa.

Wakati akitoa salamu hizo, mamia ya wananchi walikuwa wakiitikia kwa sauti kubwa ya ndiyo, ndiyo kama ishara ya kumuunga mkono, huku wengine wakiimba CCM imeuza jimbo hilo.

Mbowe alisema mchuano wa Chadema na CCM katika jimbo hilo ni kama timu za mpira za Manchester United na Liverpool za Uingereza.

Aidha, aliwataka polisi kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni za jeshi hilo na sio kuisaidia CCM katika harakati zake za kuwania ubunge katika jimbo hilo.

SOURCE: Nipashe
 
Last edited by a moderator:
FFU wamimina mabomu ya machozi Msafara wa Freeman Mbowe Busanda

2009-04-22 21:49:48
Na Joseph Mwendapole


Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wamefyatua mabomu ya machozi kuwatawanya mamia ya watu waliojitokeza kumlaki Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kwenye stendi ya mabasi ya Kataro, Jimbo la Busanda mkoani Mwanza.

Tukio hilo lilitokea majira ya 12:30 jioni juzi kilomita mbili kabla ya kufika eneo la stendi hiyo, ambako wakazi hao walisukuma gari la Mbowe, lakini mwenyewe alilazimika kuteremka na kutembea kwa miguu umbali wa kilomita moja.

Huku wakiimba kibwagizo cha `Mbowe, Mbowe,` umati mkubwa wa watu ulizidi kumiminika katika stendi hiyo, hali ambayo iliwafanya polisi kuwataka wakazi hao watawanyike huku wakifyatua mabomu ya machozi kwa lengo la kuwatawanya.

Polisi walikuwa wakiwataka wakazi hao kutawanyika kwa vile hapakuwa na mkutano wa hadhara ulioruhusiwa kufanyika.
Hata hivyo, wakazi hao waligoma kutawanyika, hadi watakapomwona Mbowe.

Akiwa jukwaani, Mbowe aliwaambia polisi kwamba hawakuwa na lengo la kufanya mkutano, isipokuwa walitaka kuwasalimia wananchi waliofurika kuwapokea.

Akiwasalimia wananchi hao, Mbowe alisema Jimbo la Busanda litakuwa kama lilivyokuwa Jimbo la Tarime, ambalo Chadema kilishinda katika uchaguzi mdogo wa ubunge na kukibwaga Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichokuwa mshindani wake mkubwa.

Wakati akitoa salamu hizo, mamia ya wananchi walikuwa wakiitikia kwa sauti kubwa ya ndiyo, ndiyo kama ishara ya kumuunga mkono, huku wengine wakiimba CCM imeuza jimbo hilo.

Mbowe alisema mchuano wa Chadema na CCM katika jimbo hilo ni kama timu za mpira za Manchester United na Liverpool za Uingereza.

Aidha, aliwataka polisi kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni za jeshi hilo na sio kuisaidia CCM katika harakati zake za kuwania ubunge katika jimbo hilo.

SOURCE: Nipashe

Kwanza nampa pole MH. Mbowe,
JE, WAZEE WA MAADILI mnatuambia nini kuhusiana na hili ? Je ni vyema kutupiana mabomu ya machozi bila ya sababu ?
Au maadili ni kukoseana heshima tu ? Maadili kwa upande wangu ni "tabia", aidha iwe nzuri au mbaya, na sasa naona tushakuwa na haka katabia "maadili" ka kurushiana mabomu ya machozi humu ndani ya taifa letu!

kaswali za uzushi tu, hivi ni lini mara ya mwisho tulisikia kiongozi wa ccm karushiwa mabomu ya machozi ??
 
FFU wamimina mabomu ya machozi Msafara wa Freeman Mbowe Busanda

HNH, naona kichwa cha habari hakibebi ujumbe wa habari yenyewe. Labda ungesema, "Kusanyiko la kuipokea chadema busanda lamiminiwa mabomu ya machozi".

Kuna haja ya kutafakari zaidi ni wakati gani nguvu za polisi zinahitajika kutumika katika harakati za siasa. Kwa mtindo huu wanafanya ionekane kuwa wanatumiwa na ccm, na hivyo kuendelea kuwajengea zaidi wanachi chuki dhidi ya ccm.
 
Kwanza nampa pole MH. Mbowe,
JE, WAZEE WA MAADILI mnatuambia nini kuhusiana na hili ? Je ni vyema kutupiana mabomu ya machozi bila ya sababu ?
Au maadili ni kukoseana heshima tu ? Maadili kwa upande wangu ni "tabia", aidha iwe nzuri au mbaya, na sasa naona tushakuwa na haka katabia "maadili" ka kurushiana mabomu ya machozi humu ndani ya taifa letu!

kaswali za uzushi tu, hivi ni lini mara ya mwisho tulisikia kiongozi wa ccm karushiwa mabomu ya machozi ??

Haya weee Kada mi yangu macho na masikio maana huu wokovu uliokushukia lazima kuna jambo. Ila wakuhurumiwa ni hawa polisi maana wanatumiwa kama mbwa awindaye sungura lakini anaishia kula mifupa pekee.
 
Wanazidi kumjenga na kuijenga CHADEMA. Inaonekana wazi kuwa kwa sasa tishio kubwa la CCM huku bara ni CHADEMA.Watatumia nguvu kubwa matokeo yake ni kuipandisha zaidi profile ya CHADEMA na Mbowe.
 
Wanazidi kumjenga na kuijenga CHADEMA. Inaonekana wazi kuwa kwa sasa tishio kubwa la CCM huku bara ni CHADEMA.Watatumia nguvu kubwa matokeo yake ni kuipandisha zaidi profile ya CHADEMA na Mbowe.

You are spot on!

Slowly watanzania wanaanza kutenganisha chuya na mchele, which is their basic right; yet wananyimwa kwa mabomu ya machozi. Hawa ndio mashujaa wetu wachache, ambao wako tayari kufia demokrasia ya vitendo. Tutaendelea kuona hivi hivi kama mchezo, I tell you tutashangazana 2010!

This is the so called 'kisiwa cha amani' kuwapumbaza mataifa ili kafiri aendeleze mradi wake. Tutakuwa free lini??
 
Hapo lazima kumkoma nyani; Mbowe andaa mipango ya uhakika kulichukua jimbo hilo; ita timu yote na msambae vijiji vyote hamna kulala mpaka CCM watoe machozi; na mkilichukua hilo jimbo ni kazi moja tu itabaki; kumuandaa Rais kutoka chadema wa Tz 2010; si lazima awe M/kiti yeyote aandaliwe ( Leaders are made not born) ; huku wao wakigombania vimeo; waTZ wasonga mbele na mabadiliko ya kweli
 
brother mbowe wory not, wanajaribu kufanya vihoja kwa sababu waona yaliyotokea mbeya vijijini na tarime yatajirudia huko pia.mpaka kieleweke kipindi hiki.
 
kicha cha habari hakiusiani kabisa na topic yenyewe, anyway wataalamu wanasema huwezi kushindana na wakati, muda ukifika hata wakitumia vifaru, kama hipo hipo tu, hakuna m2 aliyekuwa anategemea south africa ingepata uhuru pamoja na nguvu zote zile za makaburu, lakini muda ulipofika uhuru ukapatikana
cha muhimu ni kuwatoa mapema wa kina ZITTO ndani ya chama isije ikawa kama wakina lamwahi na NCCR
 
Mbowe nakupa pole, lakini hili ni jambo zuri wanalo lifanya hao mafisadi bila kujua, wanazidi kuipaisha chadema!

Ila hao askari nawaonea huruma, hivi ukiwa askari manake unaambiwa uache kufikilia kutumia ubongo wako badala yake mtu awe anafikiria kwa ajili yako na lolote utakalo ambiwa bila kufikilia unaswaga tu?

Nyie askari, ebu tumieni akili zenu mlizo jaliwa na Muumba wacheni kuwa kama roboti! Siyo kila ukiambiwa piga unapiga ua, una ua bila kujiuliza kwanini unafanya hivyo? sasa mabomu ya machozi yanini? kwa vurugu zipi hadi muwarushie raia wenzenu mabomu? mwe!
 
Polisi wana haki ya kutuliza ghasia. Freeman kakubali walikuwa hawana kibali cha kufanya mkutano hapo. Kumetokea mkusanyiko wa watu na basi polisi wana haki ya kufanya kazi yao. Mwenye kosa ni mtoa vibali vya mikutano au Chadema. Wangeomba kibali in anticipating such a turn-out.
 
Mazingaombwe tu! Watu wanajitafutia umaarufu hapa!

My general take regarding Mh. Mbowe my friend and my brother!!!

Sina shaka na Uzalendo wa Mh. Mbowe kama nilivyosina shaka na Uzalendo wa Mzee wa Kiraracha aka. Lyatonga Mrema.

Lakini nina mashaka makubwa sana ya:-

Mh. Mbowe kama kiongozi wa nchi kama nilivyokuwa na Mashaka makubwa sana kwa Mheshimiwa Lyatonga kuwa Kiongozi wa Nchi.

Ahsanteni kwa kunisoma.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Mazingaombwe tu! Watu wanajitafutia umaarufu hapa!

My general take regarding Mh. Mbowe my friend and my brother!!!

Sina shaka na Uzalendo wa Mh. Mbowe kama nilivyosina shaka na Uzalendo wa Mzee wa Kiraracha aka. Lyatonga Mrema.

Lakini nina mashaka makubwa sana ya:-

Mh. Mbowe kama kiongozi wa nchi kama nilivyokuwa na Mashaka makubwa sana kwa Mheshimiwa Lyatonga kuwa Kiongozi wa Nchi.

Ahsanteni kwa kunisoma.

Mungu Ibariki Tanzania


samahani Kasheshe, unaweza fafanua ukatusaidia na sisi? inawezekana mashaka yako yakanisaidia mimi binafsi.
 
Ila wakuhurumiwa ni hawa polisi maana wanatumiwa kama mbwa awindaye sungura lakini anaishia kula mifupa pekee.

Mkuu nimeipenda sana hii! Polisi wetu naona hata elimu ya uraia hawana sijui huko Moshi huwa wanaijifunza nini!

Hivi, ingelikuwa wananchi wamekusanyika hivyo (bila kibali) kwa ajili ya kumpokea say Makamba, je, hawa Polisi wangeliwarushia mabomu hivi? Je, kulikuwa na risk gani ya kiusalam ambayo wananchi wale walikuwa wanaipose pale?

Very tired na huu uonevu!
 
Kumetokea mkusanyiko wa watu na basi polisi wana haki ya kufanya kazi yao. Mwenye kosa ni mtoa vibali vya mikutano au Chadema. Wangeomba kibali in anticipating such a turn-out.

Wananchi ambao hukusanyika informally barabarani na kuzuia mIsafara wa JK mara nyingi ili kumshinikiza asimame wampe hi na kusikiliza kero zao, mbona hao Polisi huwa hawafanyi ''kazi yao'' unayoirefer hapo? why, kama sio upendeleo na double standards & lack of consistency in dealing with securty issues kwa hawa polisi?
 
Hao polisi wanatoka Zenji nini ? Maana polisi wa kule wana uzoefu na utumwa huo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom