Mbowe ana msongo mkubwa wa mawazo, ni baada ya kutoitwa Ikulu

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Sep 11, 2017
244
312
Nimemsikiliza mtani wangu Mbowe akijibu swali ni kwa nini hajaalikwa Ikulu ilihali yeye ndiye aliomba kwa maandishi lakini wamealikwa ambao hawajaomba kualikwa?

Ukimsikiliza utabaini ana kitu Wazungu na Wapare tunaita "psychological disorder". Yaani hitilafu itokanayo na matatizo ya kijamii na kiakili.

Huenda ni mjumuiko wa stress za kuulizwa maswali na wapiga kura, hofu ya uwezekano wa kufungwa au kupoteza ukuu wa kambi mwaka huu. Majibu ya Mbowe ni kiburudisho tosha!

Ikumbukwe mwaliko hauombwi. Huwezi kuomba mtu akualike! Ukishaomba mtu akualike unakuwa umejishusha thamani mno. Huna tofauti na ng'ombe anayetolewa bomani kwenda kuchinjwa. Hata ukialikwa unakuwa mgeni asiye na thamani! Ukifanya kosa la kuomba mwaliko na usialikwe ni busara ukae kimya kulinda hadhi yako.

Lakini pili huwezi kudai walioalikwa hawakuzungumzia hoja zako. Unajua kadi zao za mialiko zilisemaje?
Tatu, ili ualikwe lazima wewe unayetamani kualikwa uwe muungwana na mstaarabu. Usiwe unamzushia uongo unayetamani akualike. Mfano ni kauli ya Mbowe kuhusu Gwajima. Tayari polisi walishamuita kumhoji siku chache nyuma.

Leo Mbowe anamtuhumu anayetamani amualike kuwa ndiye aliyemtuma Gwajima. Anawapigisha ukunga wamama eti washike vichwa na kulia "keleuwiiiii" Mbowe hana hata punje ya ushahidi! Akiitwa polisi atabaki kudai polisi inatumika vibaya. Kwa akili tu ya mtaani, hivi Rais atamwalika mtu sampuli hii? Mtu anayemzushia kila uongo unaokuja kichwani?

Mbowe hapaswi kualikwa hata na DC Sabaya achilia mbali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na ukweli ni kuwa asipoalikwa hana chochote cha kufanya zaidi ya kupiga kelele BAWACHA na BAVICHA za keleuwiiiii!

Mbowe anaendelea kujidanganya na nguvu ya umma ambayo ni hewa. Angekuwa nayo asingesusa uchaguzi akaenda kusinzia. Asingekuwa anamuomba Rais uchaguzi urudiwe, angeitumia kulazimisha uchaguzi urudiwe. Ukweli ni huo Mbowe ni ombaomba, hana nguvu ya umma.

Ukichanganya na hoja kuhusu msajili kuvitaka vyama vihakikiwe kabla ya uchaguzi mkuu hutasita kubaini Mbowe ana msongo mkubwa wa mawazo! Hoja anayotoa kuwa vyama vimezuiwa kufanya kazi ni kichekesho. Mfano, Chama chake kimefanya uchaguzi wa viongozi hivi karibuni.

Hata juzi alianza mikutano jimboni mwake sema tu ukaingia mdudu. Hivi alitaka afanye nini kuimarisha Chama chake akazuiwa? Kuna aliyemzuia kusajili wanachama? Kujenga ofisi? Kutekeleza au kusimamia miradi ya maendeleo? Nadhani msajili aanze hili zoezi haraka. Kuna vyama vilishapoteza uhalali.

Vimebaki kuwa vyama vya BBC, DW, Twitter na Press conference tu. Hivi Mbowe ana hofu ya nini kuhakikiwa? Hana wanachama pande zote za muungano? Si huwa anajitapa Chadema imeenea hadi vijijini kupitia operesheni? Hofu ya nini?

Nimalizie kwa kumtakia hukumu njema mtani wangu hapo kesho.

Soma: Mbowe: CHADEMA haikupokea mwaliko wa kwenda Ikulu kuzungumza na Rais Magufuli
 
Kila zama na nyakati zake.

Alipowekwa ndani mara mbili na wafuasi wake wakala xmass na pasaka vizuri...ndio nilitambua hana huo umma

Umma alio nao wako mitandaoni kwa ID fake, wanaweza kutukana, kukejeli, kukuita msaliti, kamwe hawanaga muda wa kukifanya chama kikue
 
Kila zama na nyakati zake.

Alipowekwa ndani mara mbili na wafuasi wake wakala xmass na pasaka vizuri...ndio nilitambua hana huo umma

Umma alio nao wako mitandaoni kwa ID fake, wanaweza kutukana, kukejeli, kukuita msaliti, kamwe hawanaga muda wa kukifanya chama kikue
Unafikiri mwenyekiti yupi akiwekwa ndani wafuasi wake hawatakula xmass na na pasaka vizuri? Mtaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CalvinKimaro,
tunachojua ni kuwa Mbowe alimwelekeza rais afanye maridhiano na kambi ya upinzani na rais akatii bila ajizi.

tunajua Rais wetu ni egoistic, so hataki kuonekana amemtii Mbowe mbele ya mamilioni ya Watanzania tuliosikiliza ile speech ya Mbowe.

ndiyo maana rais ame mute mwaliko kwa Mbowe ambaye naye katoa condition kuwa hata akialikwa basi ni lazima aende na jopo lake lote la magwanda.

no drama!
 
Kila zama na nyakati zake.

Alipowekwa ndani mara mbili na wafuasi wake wakala xmass na pasaka vizuri...ndio nilitambua hana huo umma

Umma alio nao wako mitandaoni kwa ID fake, wanaweza kutukana, kukejeli, kukuita msaliti, kamwe hawanaga muda wa kukifanya chama kikue
Wanapost na kujicoment wao wenyewe mchana kutwa,
Wakitoka JF,wanaenda twitter then Instagram.

Ukiwajibu hoja za msingi wao wanaishi kukukejeli buku saba wa lumumba.

Wenzao CCM wanafanya siasa usiku na mchana huko kwa wananchi lakini hawa wenzetu hata ofisi za kata haziko wazi.

Wakishindwa.....
Tumeibiwa khe.....


Sent using Jamii Forums mobile app
 
tunachojua ni kuwa Mbowe alimwelekeza rais afanye maridhiano na kambi ya upinzani na rais akatii bila ajizi.

tunajua Rais wetu ni egoistic, so hataki kuonekana amemtii Mbowe mbele ya mamilioni ya Watanzania tuliosikiliza ile speech ya Mbowe.
ndiyo maana rais ame mute mwaliko kwa Mbowe ambaye naye katoa condition kuwa hata akialikwa basi ni lazima aende na jopo lake lote la magwanda.

no drama!
Haya asubiri huo mwaliko mwaka 2021

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CalvinKimaro,
Mkuu ulichoandika hapa ni ukweli asilimia miamoja! Tatizo la Mbowe na CHADEMA ni ulema lema, uheche heche, yaani wanadhani watanzania zaidi ya ml.50 wte wanaweza kuturagai kwa viroba vya pombe na misokoto ya bangi ambayo waliitumia kugawa kwa vijana na kuwaingiza barabarani.

Mbowe na genge lake tangu aingie magufuri madarakani na kutekeleza vyema irani ya ccm pamoja na hoja zote za wapinzani akiwemo Babu seya , ufisadi, rushwa, nidham, na maendereo ya wazi na yanayoonekana! Chadema wakaanza sera za vurugu ,uzushi, na uchonganishi.

Lakini hata walivyoshindwa kuwaaminisha watanzania hawajataka kurudi kwenye mstari! Wanachadema wenyewe wanataka kujua matumizi ya fedha za michango yao, fedha za rudhuku, lakini yeye amebaki kuwakodishia ndege, kuwakodishia kumbi za gharama na kuwashonea wakina mama wa Bavicha vitenge!
Kuhusu hukumu yaleo!

Kiukweli wasipokula mvua basi nitajua mahakama inawaogopa wanasiasa.
Maana ukisikiliza ile crip ya kinondoni hata kama ningekuwa mm hakim mtu wakutoka hapo labda salum mwalim.
 
Kila zama na nyakati zake.

Alipowekwa ndani mara mbili na wafuasi wake wakala xmass na pasaka vizuri...ndio nilitambua hana huo umma

Umma alio nao wako mitandaoni kwa ID fake, wanaweza kutukana, kukejeli, kukuita msaliti, kamwe hawanaga muda wa kukifanya chama kikue
Umewapiga mshale wa goti. Hawasimami wala hawakai.
 
Haya ndio mawazo ya middle class wa kitanzania,ambaye anajiona amesoma na ana uelewa wa kusoma to understand,kwa taarifa yako mtoa hoja ;ni kweli Mh.Mbowe aliandika barua ikulu kwa ajili ya kukutana na our no 1(ni haki yake ambayo hata mimi na wewe tunayo,ili mradi tufuate sheria)kukubaliwa kwa ombi ni HAKI ya yule anayeombwa(kumbuka hili mkuu).

Kwa taarifa yako mh.Shariff Hamad alishaandika barua muda mrefu ya kuomba kukutana na president Magufuli na hili alituthibitishia kuwa wakati wa uzinduzi wa kitabu cha President Mkapa,Rais Magufuli alimjibu kuwa anajua anamtafuta na atatafuta muda waonane,kwa hiyo ni ufinyu wa akili yako mtoa hoja kuwa Mh.Hamad hakuomba mwaliko.next time unapotoa hoja ni vema usipindishe ukweli pamoja na mapenzi yako (ambayo nayo ni haki yako).
 
Eti ana msongo.Kwani Ikulu ni mbinguni?

Mbona Mbowe alishakanyaga hapo Ikulu enzi za JK mara kadhaa,halafu leo ndo aone ni mahala pa pekee sana? Mbona alishakanyaga Ikulu nyingine kadhaa hapa duniani ambazo ni nzuri zaidi ya hiyo ya Magogoni?
 
Mbowe ameanza kwenda ikulu enzi za baba wa taifa wakati huo huyo mshamba wenu alikuwa bado ana matongotongo huko bush
 
Nadhani utakuwa Msangi vile na upo karibu sana na yule mzee pale tambarare. Pole sana ila CCM haina rafiki wa kudumu. Ka Mbowe ana huo ugonjwa uliouona nadhani weye ndo umesha komaa kabisa ndo maana ukaweza kumtambua mgonjwa mpya Mbowe.
shetwani hajawahi kuwa na urafiki wa kudumu na binadamu hata siku moja tambua hilo.
 
Back
Top Bottom