CalvinKimaro
JF-Expert Member
- Sep 11, 2017
- 244
- 312
Nimemsikiliza mtani wangu Mbowe akijibu swali ni kwa nini hajaalikwa Ikulu ilihali yeye ndiye aliomba kwa maandishi lakini wamealikwa ambao hawajaomba kualikwa?
Ukimsikiliza utabaini ana kitu Wazungu na Wapare tunaita "psychological disorder". Yaani hitilafu itokanayo na matatizo ya kijamii na kiakili.
Huenda ni mjumuiko wa stress za kuulizwa maswali na wapiga kura, hofu ya uwezekano wa kufungwa au kupoteza ukuu wa kambi mwaka huu. Majibu ya Mbowe ni kiburudisho tosha!
Ikumbukwe mwaliko hauombwi. Huwezi kuomba mtu akualike! Ukishaomba mtu akualike unakuwa umejishusha thamani mno. Huna tofauti na ng'ombe anayetolewa bomani kwenda kuchinjwa. Hata ukialikwa unakuwa mgeni asiye na thamani! Ukifanya kosa la kuomba mwaliko na usialikwe ni busara ukae kimya kulinda hadhi yako.
Lakini pili huwezi kudai walioalikwa hawakuzungumzia hoja zako. Unajua kadi zao za mialiko zilisemaje?
Tatu, ili ualikwe lazima wewe unayetamani kualikwa uwe muungwana na mstaarabu. Usiwe unamzushia uongo unayetamani akualike. Mfano ni kauli ya Mbowe kuhusu Gwajima. Tayari polisi walishamuita kumhoji siku chache nyuma.
Leo Mbowe anamtuhumu anayetamani amualike kuwa ndiye aliyemtuma Gwajima. Anawapigisha ukunga wamama eti washike vichwa na kulia "keleuwiiiii" Mbowe hana hata punje ya ushahidi! Akiitwa polisi atabaki kudai polisi inatumika vibaya. Kwa akili tu ya mtaani, hivi Rais atamwalika mtu sampuli hii? Mtu anayemzushia kila uongo unaokuja kichwani?
Mbowe hapaswi kualikwa hata na DC Sabaya achilia mbali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na ukweli ni kuwa asipoalikwa hana chochote cha kufanya zaidi ya kupiga kelele BAWACHA na BAVICHA za keleuwiiiii!
Mbowe anaendelea kujidanganya na nguvu ya umma ambayo ni hewa. Angekuwa nayo asingesusa uchaguzi akaenda kusinzia. Asingekuwa anamuomba Rais uchaguzi urudiwe, angeitumia kulazimisha uchaguzi urudiwe. Ukweli ni huo Mbowe ni ombaomba, hana nguvu ya umma.
Ukichanganya na hoja kuhusu msajili kuvitaka vyama vihakikiwe kabla ya uchaguzi mkuu hutasita kubaini Mbowe ana msongo mkubwa wa mawazo! Hoja anayotoa kuwa vyama vimezuiwa kufanya kazi ni kichekesho. Mfano, Chama chake kimefanya uchaguzi wa viongozi hivi karibuni.
Hata juzi alianza mikutano jimboni mwake sema tu ukaingia mdudu. Hivi alitaka afanye nini kuimarisha Chama chake akazuiwa? Kuna aliyemzuia kusajili wanachama? Kujenga ofisi? Kutekeleza au kusimamia miradi ya maendeleo? Nadhani msajili aanze hili zoezi haraka. Kuna vyama vilishapoteza uhalali.
Vimebaki kuwa vyama vya BBC, DW, Twitter na Press conference tu. Hivi Mbowe ana hofu ya nini kuhakikiwa? Hana wanachama pande zote za muungano? Si huwa anajitapa Chadema imeenea hadi vijijini kupitia operesheni? Hofu ya nini?
Nimalizie kwa kumtakia hukumu njema mtani wangu hapo kesho.
Soma: Mbowe: CHADEMA haikupokea mwaliko wa kwenda Ikulu kuzungumza na Rais Magufuli
Ukimsikiliza utabaini ana kitu Wazungu na Wapare tunaita "psychological disorder". Yaani hitilafu itokanayo na matatizo ya kijamii na kiakili.
Huenda ni mjumuiko wa stress za kuulizwa maswali na wapiga kura, hofu ya uwezekano wa kufungwa au kupoteza ukuu wa kambi mwaka huu. Majibu ya Mbowe ni kiburudisho tosha!
Ikumbukwe mwaliko hauombwi. Huwezi kuomba mtu akualike! Ukishaomba mtu akualike unakuwa umejishusha thamani mno. Huna tofauti na ng'ombe anayetolewa bomani kwenda kuchinjwa. Hata ukialikwa unakuwa mgeni asiye na thamani! Ukifanya kosa la kuomba mwaliko na usialikwe ni busara ukae kimya kulinda hadhi yako.
Lakini pili huwezi kudai walioalikwa hawakuzungumzia hoja zako. Unajua kadi zao za mialiko zilisemaje?
Tatu, ili ualikwe lazima wewe unayetamani kualikwa uwe muungwana na mstaarabu. Usiwe unamzushia uongo unayetamani akualike. Mfano ni kauli ya Mbowe kuhusu Gwajima. Tayari polisi walishamuita kumhoji siku chache nyuma.
Leo Mbowe anamtuhumu anayetamani amualike kuwa ndiye aliyemtuma Gwajima. Anawapigisha ukunga wamama eti washike vichwa na kulia "keleuwiiiii" Mbowe hana hata punje ya ushahidi! Akiitwa polisi atabaki kudai polisi inatumika vibaya. Kwa akili tu ya mtaani, hivi Rais atamwalika mtu sampuli hii? Mtu anayemzushia kila uongo unaokuja kichwani?
Mbowe hapaswi kualikwa hata na DC Sabaya achilia mbali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na ukweli ni kuwa asipoalikwa hana chochote cha kufanya zaidi ya kupiga kelele BAWACHA na BAVICHA za keleuwiiiii!
Mbowe anaendelea kujidanganya na nguvu ya umma ambayo ni hewa. Angekuwa nayo asingesusa uchaguzi akaenda kusinzia. Asingekuwa anamuomba Rais uchaguzi urudiwe, angeitumia kulazimisha uchaguzi urudiwe. Ukweli ni huo Mbowe ni ombaomba, hana nguvu ya umma.
Ukichanganya na hoja kuhusu msajili kuvitaka vyama vihakikiwe kabla ya uchaguzi mkuu hutasita kubaini Mbowe ana msongo mkubwa wa mawazo! Hoja anayotoa kuwa vyama vimezuiwa kufanya kazi ni kichekesho. Mfano, Chama chake kimefanya uchaguzi wa viongozi hivi karibuni.
Hata juzi alianza mikutano jimboni mwake sema tu ukaingia mdudu. Hivi alitaka afanye nini kuimarisha Chama chake akazuiwa? Kuna aliyemzuia kusajili wanachama? Kujenga ofisi? Kutekeleza au kusimamia miradi ya maendeleo? Nadhani msajili aanze hili zoezi haraka. Kuna vyama vilishapoteza uhalali.
Vimebaki kuwa vyama vya BBC, DW, Twitter na Press conference tu. Hivi Mbowe ana hofu ya nini kuhakikiwa? Hana wanachama pande zote za muungano? Si huwa anajitapa Chadema imeenea hadi vijijini kupitia operesheni? Hofu ya nini?
Nimalizie kwa kumtakia hukumu njema mtani wangu hapo kesho.
Soma: Mbowe: CHADEMA haikupokea mwaliko wa kwenda Ikulu kuzungumza na Rais Magufuli