Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,441
- 7,778
Mwenyekiti wa kambi ya upinzani bungeni, Freeman Mbowe amemuuliza waziri mkuu juu matukio mengi ya siku za karibuni yanayovunja amani, usalama na yanayojenga chuki miongoni mwa vyama vya siasa na kuharibu utengamano wa kitaifa.
Amesema tukio la kushambuliwa kwa risasi kwa dhamira ya kuua kwa mbunge Tundu Lissu imezua hofu kubwa kwa Taifa, bara zima la Afrika na jumuiya ya kimataifa na taharuki hiyo imeharibu taswira na heshima ya Taifa.
Amesema hawajaona kama serikali imechukua hatua yoyote kujaribu suala hilo kutoendelea kuharibu taswira ya Taifa. Amesema hapo nyuma vilitokea vifo vya kisiasa na hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa.
Akijibu swali hilo, waziri mkuu amesema yapo matukio yanajitokeza na japokuwa mheshimiwa Mbowe ameongelea upande wa siasa, yapo matukio kwa ujumla wake nchini kwenye maeneo kadhaa. Amesema wapo watu hawana nia njia wamejitokeza ikiwemo wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji kupoteza watu wengi pia kamanda wa JWTZ kupigwa risasi hiyo wayazungumze yote kwa ujumla wake.
Amesema vyombo vya dola vinaendelea kufanya uchunguzi na hauwezi ukawa uchunguzi wa leo na ufumbuzi ukatoka leo. Amesema vyombo vya dola vina uwezo na suala la muda tu kwani wahusika walitumia mbinu nyingi kuhakikisha wanajificha. Amesema uchunguzi ukikamilika watatoa taarifa na waendelee kujenga imani kwa vyombo vya dola.
Mbowe akiuliza swali la nyongeza alisema anajua ya kila mtanzania yana thamani kubwalakini swali lake lilikuwa specific kwa siasa, amesema kushambuliwa Lissu sio la kawaida na uonevu dhidi ya vyama vya siasa nchini na leo ni siku ya tatu tangu mbunge akamatwe Mtwara. Je, Serikali inaona shida gani kuruhusu vyombo vya kimataifa vya kiuchunguzi kuja kufanya uchunguzi kwa sababu sio mara ya kwanza serikali kuomba msaada kutoka nchi za nje akitolea mfano benki kuu ilipoungua hivyo ni jambo la kawaida. Amesema vyombo vya dola hawavidharau bali havina dhamira.
Waziri mkuu amesema hakuna aliefurahishwa na matukio yanayojitokeza ya mauaji au ya shambulio kwa mbunge mwenzao lakini vyombo vya dola vimepewa jukumu la kusimamia na kulinda na pia ikitokea vina wajibu wa kufanya uchunguzi.
Amesema tukio la kushambuliwa kwa risasi kwa dhamira ya kuua kwa mbunge Tundu Lissu imezua hofu kubwa kwa Taifa, bara zima la Afrika na jumuiya ya kimataifa na taharuki hiyo imeharibu taswira na heshima ya Taifa.
Amesema hawajaona kama serikali imechukua hatua yoyote kujaribu suala hilo kutoendelea kuharibu taswira ya Taifa. Amesema hapo nyuma vilitokea vifo vya kisiasa na hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa.
Akijibu swali hilo, waziri mkuu amesema yapo matukio yanajitokeza na japokuwa mheshimiwa Mbowe ameongelea upande wa siasa, yapo matukio kwa ujumla wake nchini kwenye maeneo kadhaa. Amesema wapo watu hawana nia njia wamejitokeza ikiwemo wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji kupoteza watu wengi pia kamanda wa JWTZ kupigwa risasi hiyo wayazungumze yote kwa ujumla wake.
Amesema vyombo vya dola vinaendelea kufanya uchunguzi na hauwezi ukawa uchunguzi wa leo na ufumbuzi ukatoka leo. Amesema vyombo vya dola vina uwezo na suala la muda tu kwani wahusika walitumia mbinu nyingi kuhakikisha wanajificha. Amesema uchunguzi ukikamilika watatoa taarifa na waendelee kujenga imani kwa vyombo vya dola.
Mbowe akiuliza swali la nyongeza alisema anajua ya kila mtanzania yana thamani kubwalakini swali lake lilikuwa specific kwa siasa, amesema kushambuliwa Lissu sio la kawaida na uonevu dhidi ya vyama vya siasa nchini na leo ni siku ya tatu tangu mbunge akamatwe Mtwara. Je, Serikali inaona shida gani kuruhusu vyombo vya kimataifa vya kiuchunguzi kuja kufanya uchunguzi kwa sababu sio mara ya kwanza serikali kuomba msaada kutoka nchi za nje akitolea mfano benki kuu ilipoungua hivyo ni jambo la kawaida. Amesema vyombo vya dola hawavidharau bali havina dhamira.
Waziri mkuu amesema hakuna aliefurahishwa na matukio yanayojitokeza ya mauaji au ya shambulio kwa mbunge mwenzao lakini vyombo vya dola vimepewa jukumu la kusimamia na kulinda na pia ikitokea vina wajibu wa kufanya uchunguzi.