Mbowe amshangaa Msajili wa Mahakama suala la ubunge wa jimbo la Loliondo

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
1,606
1,956
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema ameshangazwa na kauli ya Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Elizabeth Mkwizu kwamba hakuna rufaa ya uchaguzi wa Jimbo la Longido mahakamani hapo.

Elizabeth akizungumza na Mwananchi juzi alisema, “Hapa hatuna rufaa ya uchaguzi wa Jimbo la Longido, bali kuna maombi ya kuongezwa muda wa kuwasilisha ‘notice of appeal’ (taarifa ya kusudio la kukata rufaa). Walileta notice of appeal lakini ikatupiliwa mbali, sasa wanaomba muda ili waiwasilishe tena. Maombi si rufaa, kwa hiyo haya maombi yasingeweza kusimamisha shughuli za uchaguzi.”

Alikuwa akirejea uchaguzi mdogo uliofanyika Januari 13 baada ya aliyekuwa mbunge wa Longido kwa tiketi ya Chadema, Onesmo ole Nangole ushindi wake kutenguliwa na Mahakama Kuu.

Hata hivyo, Mbowe akizungumza na Mwananchi jana alisema kuna vitu vinaendelea kwa namna moja au nyingine katika Mahakama vinafikirisha na kuona wapinzani hawatendewi haki.

“Kama wanakiri maombi yalipelekwa na wanayo, kufungua kesi si ni ‘process’ (mchakato), zote za kwenda kukata rufaa sasa kama maombi yatakubaliwa na tukakata rufaa, huo uchaguzi ulioitishwa na kufanyika inakuwaje?” alihoji;

“Hakuna mtu anayetaka kukata rufaa bila sababu, maombi hayo ni sehemu ya kesi. Lakini kwa nini wasingesikiliza haraka hayo maombi ili kama yanakataliwa uchaguzi ufanyike.”

Mbowe, ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni alisema, “Kuna mambo ambayo yafanyika katika Mahakama zetu baadhi yanatia doa na ndilo tatizo la nchi yetu.”

Katika ufafanuzi wake, Mkwizu alisema kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya Mahakama ya Rufaa, maombi hayo yamepangwa kusikilizwa na Jaji Jacob Mwambegele, Februari 5.

Wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo, mwombaji kupitia kwa mawakili wake atalazimika kutoa sababu za kuiridhisha Mahakama ni kwa nini alichelewa kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa.

Ikiwa Mahakama haitaridhika na sababu zake, itatupilia mbali maombi hayo lakini ikiridhika nazo itamruhusu kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa.

Baada ya kuwasilisha taarifa hiyo, atasubiri kupata kumbukumbu za rufaa, yaani nyaraka zitakazohusika kwenye rufaa yake, ikiwamo hukumu anayoilalamikia, mwenendo wa kesi ya msingi na vielelezo vilivyotumika.

Akipata nyaraka hizo, ndipo atakapowasilisha rufaa kamili, yaani sababu za kwa nini anapinga hukumu iliyomvua ubunge wa jimbo hilo, na upande wa pili (wajibu rufaa) nao utawasilisha hoja zake na baada ya Mahakama kusikiliza hoja za pande zote ndipo itatoa hukumu.

Ole Nangole alivuliwa ubunge na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Juni 29, 2016 kutokana na kesi ya uchaguzi iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa kiti hicho kwa tiketi ya CCM, Dk Steven Kiruswa akipinga ushindi wake.

Baada ya Mahakama kumvua ubunge, Ole Nangole kupitia mawakili John Materu na Dancan Oola aliwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa kupinga hukumu hiyo.

Hata hivyo, taarifa hiyo ya kusudio la kukata rufaa ilitupiliwa mbali kwa kuwa muda wa kisheria wa siku 14 za kuwasilisha kusudio la kukata rufaa ulikuwa umeshaisha ndipo alipoomba kuongezewa muda wa kuwasilisha taarifa hiyo.

Maombi hayo pia yalitupiliwa mbali na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, ndipo wakapeleka maombi Mahakama ya Rufani

Chanzo: Mwananchi
 
Mbowe amechanganyikiwa,hiyo fani angewaachia akina kibatala,mambo ya kisheria ni tofauti na kuchezesha santuri na div 0 yake
 
Wamuulize Wasira kesi za uchaguzi huchukua muda gani mahakamani. Hakuna sheria inayozifanya ziwe of top priority. Yaani mahakama kuu ziahirishe ratiba ya shughuli zake kwa sababu kuna mwanasiasa anafikiria kadhulumiwa haki yake kwenye uchaguzi.

Kesi za malalmiko ya uchaguzi mkuu hupangiwa mwaka mmoja ziwe zimetolewa hukumu, kitu ambacho kilitekelezwa katika jimbo hilo la Longido na mbunge mwingine kaishapatikana. Mbunge huyo mpya anatakiwa kuendelea na kazi hata kama kuna kesi ya rufaa. Hakuna utaratibu wa kisheria kuwa rufaa hizo ziwe zimekamilika ndani ya kipindi gani. Hivyo Mbowe awe na subira. Kama atashinda hiyo rufaa hata baada ya mwaka mmoja, uchaguzi mwingine mdogo utafanyika kwenye jimbo hilo na mbunge atakayeshindwa rufaa naye atakata rufaa nyingine kwani ni haki yake and the circle continues!
 
Mbowe amechanganyikiwa,hiyo fani angewaachia akina kibatala,mambo ya kisheria ni tofauti na kuchezesha santuri na div 0 yake
Wewe ni mtoto mdogo!!!? Kwani akili zako zinaonekana ni za kitoto. Kwani kuelezea makosa yanayofanywa na mahakama lazima uwe mwanasheria? Yeye ni mwenyekiti wa chama. Wanasheria wa chadema wameshamuejezea makosa ya ya kisheria yaliyofanywa na msajili wa mahakama.
 
Wewe ni mtoto mdogo!!!? Kwani akili zako zinaonekana ni za kitoto. Kwani kuelezea makosa yanayofanywa na mahakama lazima uwe mwanasheria? Yeye ni mwenyekiti wa chama. Wanasheria wa chadema wameshamuejezea makosa ya ya kisheria yaliyofanywa na msajili wa mahakama.
Ndio tatizo la makarai,mnapenda kulazimisha yaliokuwa kwenye ubongo wenu yawe ya kweli
Hoja hii ilipaswa iongelewe na mwamsheria sio mwanasiasa,wewe unajaribu tu kuremba,mbona tunawaona akina kibatala wanaongelea mambo ya kesi za chadema?
Tatizo mmezoea kudanganywa na hakuna anaehoji
Lowassa alitukanwa na kina tundu lissu na lema kwa kumpongeza magufuli mpaka leo imezimwa kimya kimya,wakati kamati kuu iltuambia itatoa tamko
 
Kauli ya Mahakama in maana kuwa hiyo rufaa itatupwa tu. Sasa hiyo tarehe 5/2/2018 mahakama itasikiliza nini wakati tayari imeruhusu uchaguzi ufanyike? kwa nini mahakama haikusubiri shauri la msingi liishe kwanza ili kuona upande gani una haki?
 
Wamuulize Wasira kesi za uchaguzi huchukua muda gani mahakamani. Hakuna sheria inayozifanya ziwe of top priority. Yaani mahakama kuu ziahirishe ratiba ya shughuli zake kwa sababu kuna mwanasiasa anafikiria kadhulumiwa haki yake kwenye uchaguzi.

Kesi za malalmiko ya uchaguzi mkuu hupangiwa mwaka mmoja ziwe zimetolewa hukumu, kitu ambacho kilitekelezwa katika jimbo hilo la Longido na mbunge mwingine kaishapatikana. Mbunge huyo mpya anatakiwa kuendelea na kazi hata kama kuna kesi ya rufaa. Hakuna utaratibu wa kisheria kuwa rufaa hizo ziwe zimekamilika ndani ya kipindi gani. Hivyo Mbowe awe na subira. Kama atashinda hiyo rufaa hata baada ya mwaka mmoja, uchaguzi mwingine mdogo utafanyika kwenye jimbo hilo na mbunge atakayeshindwa rufaa naye atakata rufaa nyingine kwani ni haki yake and the circle continues!

Mkuu kenya linafanyika hilo na lipo kikatiba kuwa kesi zote lazima ziishe faster nadhani ndani ya miezi sita.
 
Back
Top Bottom