Benson Mramba
JF-Expert Member
- Oct 29, 2013
- 644
- 1,482
Miaka yote tangu 2017 nimekuwa nikisema kuwa uwezo wa Mbowe kuiongoza CHADEMA ulikuwa umefikia mwisho kama kiongozi.
Nilisema sababu kubwa ni washauri wabovu, wenye uwezo mdogo wanamzunguka Freeman Mbowe. Niliwataja washauri hao kuwa ni Lema, Msigwa, John Mrema na Reggy Munisi. Nikasema CHADEMA inaharibiwa na kakikundi cha watu wasiozidi watano wakati ule. Watu hawakunielewa wakadhani nina chuki binafsi.
Jana yametokea makubwa kabisa kabisa ya kiongozi Mkuu kusema uongo hadharani kwa taifa, kulewa kupita kiasi mambo ambayo ni ukosefu wa maadili kwa kiwango cha juu kabisa kwa kiongozi wa ngazi yake.
Mimi nina maslahi makubwa na CHADEMA kama Mtanzania ninayependa upinzani na niliyepoteza muda wangu mwingi na rasilimali kuijenga CHADEMA na upinzani. Hivyo siwezi kumuacha Mbowe na kikundi chake wauvuruge upinzani nchini na CHADEMA.
Ninamtaka Mbowe, Kamati Kuu ya CHADEMA, Msajili wa vyama na kila anayehusika kumtaka Mbowe ajiuzulu kwasababu amekosa maadili na hana nia njema na CHADEMA wala Taifa letu la sivyo nitampeleka kwenye TUME YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA na ikilazimu Mahakamani.
Naomba kila Mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi hii aniunge mkono. Haya ni maamuzi yangu mwenyewe nikiwa na akili timamu bila kushinikizwa na mtu yoyote.
Naomba kuwasilisha
Nilisema sababu kubwa ni washauri wabovu, wenye uwezo mdogo wanamzunguka Freeman Mbowe. Niliwataja washauri hao kuwa ni Lema, Msigwa, John Mrema na Reggy Munisi. Nikasema CHADEMA inaharibiwa na kakikundi cha watu wasiozidi watano wakati ule. Watu hawakunielewa wakadhani nina chuki binafsi.
Jana yametokea makubwa kabisa kabisa ya kiongozi Mkuu kusema uongo hadharani kwa taifa, kulewa kupita kiasi mambo ambayo ni ukosefu wa maadili kwa kiwango cha juu kabisa kwa kiongozi wa ngazi yake.
Mimi nina maslahi makubwa na CHADEMA kama Mtanzania ninayependa upinzani na niliyepoteza muda wangu mwingi na rasilimali kuijenga CHADEMA na upinzani. Hivyo siwezi kumuacha Mbowe na kikundi chake wauvuruge upinzani nchini na CHADEMA.
Ninamtaka Mbowe, Kamati Kuu ya CHADEMA, Msajili wa vyama na kila anayehusika kumtaka Mbowe ajiuzulu kwasababu amekosa maadili na hana nia njema na CHADEMA wala Taifa letu la sivyo nitampeleka kwenye TUME YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA na ikilazimu Mahakamani.
Naomba kila Mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi hii aniunge mkono. Haya ni maamuzi yangu mwenyewe nikiwa na akili timamu bila kushinikizwa na mtu yoyote.
Naomba kuwasilisha