Mbowe afanya mazungumzo na Chancellor wa Ujerumani

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Ziara ya CHADEMA, mbinyo mkubwa zaidi unakuja dhidi ya mafisadi wa ESCROW.
attachment.php

Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe mwanzoni mwa wiki hii alikutana na kufanya mazungumzo na Kansela wa Ujerumani Bibi Angela Markel.

Mbowe alikutana na Kiongozi huyo wa Taifa kubwa duniani pembeni ya Mkutano Mkuu wa chama cha CDU kinachotawala Ujerumani na kinachoongozwa na Bibi Markel.

Ingawa mazungumzo baina ya vigogo hao wawili hayajawekwa wazi lakini inatarajiwa kashfa ya wizi wa fedha wa Tegeta Escrow,Ukandamizaji wa demokrasia nchini na Katiba haramu ya CCM inayoitwa Katiba mpya ni kati ya mambo yaliyojadiliwa.

Katika ziara hiyo nchini Ujerumani mbali na Mbowe pia alifuatana na Makamu Mkiti Professor Abdallah Safari,Naibu Katibu Mkuu Salum Mwalim,Mkiti wa Bavicha Pascal Patrobas,Katibu Mkuu Bawacha Grace Tendega na Mkurugenzi wa Halmashauri wa chama hicho John Mrema.
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    43.3 KB · Views: 5,209
  • image.jpg
    image.jpg
    72 KB · Views: 8,430
  • mbowe.png
    mbowe.png
    17 KB · Views: 5,784
Juzi kuna kamkutano ka nyinyiem kata ya kisiwani-Rukwa huku akizomewa alisema "kufikia mwezi June mwakani tutakuwa tumefunga umeme kila kijiji' kumbe ndoto lol
 
Juzi kuna kamkutano ka nyinyiem kata ya kisiwani-Rukwa huku akizomewa alisema "kufikia mwezi June mwakani tutakuwa tumefunga umeme kila kijiji' kumbe ndoto lol
Alikuwa anaota......wana ukawa wakamwambia ww jamaa unaota hafu unaongea kwa sauti kubwa hadi tunasikia! teh teh
 
Ni vizuri hawa mafisadi wakafungwa ama kunyongwa kabisa! Tatizo kubwa la mafisadi wana mafungamano na ikulu yetu kwa namna moja ama nyingine!
 
Mbowe safi sana waeleze kila kitu wahisani ikibidi wakate misaada kabisa kushinikiza fedha za escrow zirudi.
 
UKAWA wameshakabidhiwa nchi kiaina. Ukiona mataifa makubwa yanaacha kushirikiana na sertikali iliyopo madarakani na kushirikiana na upinzani ujue walishasoma alama za nyakati na kuona dalili kubwa za upinzani kuchukua nchi, nawaonea huruma ccm kwani hawaliamini hili
 
Mbowe safi sana waeleze kila kitu wahisani ikibidi wakate misaada kabisa kushinikiza fedha za escrow zirudi.

Watanzania mpaka wafike mahali waone watoto wao wanawafia mikononi kwa njaa ndio yatazinduka na kuchana CCM, bila hivyo hayatazinduka
 
CCM wamebanwa kote kote..........hapo ndio tutaiona rangi halisi ya CCM, ama wananchi mufe kwa kukosa huduma baada ya misaada kuminywa au CCM wawatose wezi wenzao wananchi wapone........uamuzi mezani kwa JK.
 
Watanzania mpaka wafike mahali waone watoto wao wanawafia mikononi kwa njaa ndio yatazinduka na kuchana CCM, bila hivyo hayatazinduka

Kwani kuna chama kikiingia madalakani ndiyo kitakuwa kinagawa chakula bure majumbani?
 
Mbowe safi sana waeleze kila kitu wahisani ikibidi wakate misaada kabisa kushinikiza fedha za escrow zirudi.

Mimi nilidhani awaambie waache kutunyonya na kuiba maliasili zetu wewe unasema wakate misaada! Kumbe bado unaegemea misaada!
 
alaa kumbe ninyi mnakwenda kuzuia misaada kwa ajili ya wananchi??? tumewastukia na sisi tunawatangazia wananchi kuwa ninyi mnazuia misaada kwa kisingizio cha escrow halafu mnasababisha tupunguze huduma kwao....hukumu yenu kesho , april 30 2015 na oktoba 2015
Ziara ya Chadema , mbinyo mkubwa zaidi unakuja dhidi ya mafisadi wa escrow
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe mwanzoni mwa wiki hii alikutana na kufanya mazungumzo na Kansela wa Ujerumani Bibi Angela Markel.

Mbowe alikutana na Kiongozi huyo wa Taifa kubwa duniani pembeni ya Mkutano Mkuu wa chama cha CDU kinachotawala Ujerumani na kinachoongozwa na Bibi Markel.

Ingawa mazungumzo baina ya vigogo hao wawili hayajawekwa wazi lakini inatarajiwa kashfa ya wizi wa fedha wa Tegeta Escrow,Ukandamizaji wa demokrasia nchini na Katiba haramu ya CCM inayoitwa Katiba mpya ni kati ya mambo yaliyojadiliwa.

Katika ziara hiyo nchini Ujerumani mbali na Mbowe pia alifuatana na Makamu Mkiti Professor Abdallah Safari,Naibu Katibu Mkuu Salum Mwalim,Mkiti wa Bavicha Pascal Patrobas,Katibu Mkuu Bawacha Grace Tendega na Mkurugenzi wa Halmashauri wa chama hicho John Mrema.
 
Mimi nilidhani awaambie waache kutunyonya na kuiba maliasili zetu wewe unasema wakate misaada! Kumbe bado unaegemea misaada!

Kama kukata misaada itakuwa sababu ya watu kuwahibishana NA WARUKATIE TU...

Japo mwenyewe sipendi nchi inayotegemea misaada kiasi hiki
 
Ni nani anasikia harufu wa uharo wa Chama cha majambazi!!??? yameanza kuhara!!
 
Back
Top Bottom