Mbowe acha kujikaanga kwa mafuta yako

JINOME

JF-Expert Member
May 29, 2017
958
1,424
Kwenye gazeti la Nipashe Leo Alhamis Novemba 16, 2017 katika ukurasa wa Mbele limeandika nukuu ya maneno ya Mbowe ambapo amesema “Masha hakuwa na msaada wowote ule Chadema”. Lahaula!!

Leo hii Mbowe huyu huyu ndio anaibuka na maneno ya kumtuhumu Masha kuwa hakuwa na msaada wowote ule Chadema? Mbowe anasahau kuwa:-

1. Ni Chadema ndio walimteua Masha kugombea Ubunge Afrika Mashariki (EAC). Utawezaje kumteua mtu asiye na msaada nanyi wowote ule?

2. Ni Chadema hao hao walikuwa wakimpandisha Masha kwenye majukwaa ya kisiasa ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na majukwaa mengineyo ya kisiasa. Huyu ndio ambaye Mbowe anasema hakuwa na msaada wowote ule?

3. Ni Masha huyu huyu alijitoa kwenye uchaguzi wa TLS uliosaidia kuongeza ushindi kwa Tundu Lissu wa Chadema na kunyakua Urais wa TLS. Utasemaje Masha hakuwa na msaada wowote ule? Maneno mengine ni heri Mbowe ngekaa kimya tu kuliko kuamua kuongea pumba tupu.

4. Ni Masha huyu huyu aliingia matatani na vyombo vya kisheria kutokana na uamui wake wa kwenda kituo cha Polisi cha Oysterbay kwenda kutoa dhamana kwa wanafunzi waliokusanyika bila kibali. Nakumbuka Chadema walimsifia sana Masha kutokana na kitendo hiki. Leo hii Mbowe atasemaje Masha hakuwa na msaada wowote ule Chadema?

5. Masha huyu huyu alikuwa anaiwakilisha Chadema kwenye mikutano, midahalo mbalimbali. Mbowe atasemaje Masha hakuwa na msaada wowote ule? Watampaje uwakilishi mtu asiye na msaada kwao?

Anachokifanya Mbowe ni ubabaishaji, ni mwendelezo wa kutokuthamini michango ya Watu ndani ya Chadema. Ni kama ilivyofanyika kwa Zitto Kabwe, Dk. Willbroad Slaa na wengineo. Ipo siku hata wengineo nao pia kuambiwa ni mizigo, ni suala la wakati tu.

Chadema wako hivyo, mtu akitoka Chadema kwao humwita msaliti, hana msaada, amehongwa na CCM, na majina ya ovyo ovyo hupewa. Akienda Chadema huyo hutafasiriwa kuwa shujaa, Mzalendo na kamanda. Huu ni ushahidi tosha kuwa nchini hakuna upinzani bali pamejaa wababaishaji mithili ya Mbowe
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kauli na vitendo vya Mh.Mbowe na majibu(Reactions) za wanachama na viongozi wenzake pamoja na wakereketwa/wafurukutwa, majibu yao huwa ni ndiyoooooo. Angalia mifano hii hapa chini;

1. Madai ya kuwa ana ushahidi wa CD mtu aliyepiga bomu kwenye mkutano wake, hadi leo hatujaiona na wafuasi walisema ndiyooooo.

2.Mbowe alimponda sana Lowasa na kumdhalilisha, wafuasi wakasema ndiyooooo

3.Mbowe aliwahi kusema Lowasa anakuja yaanu anahamia CHADEMA na ma -Dc 82, wenyeviti CCM wilaya na mikoa wa kutosha, wafuasi ndiyoooooo, na hadi leo hakuna kitu.

4.Mbowe aliwahi kusema anabadirisha gia angani- Wafuasi ndiyoooooo, madhara yake tunayaona.

5.Aliwahi kusema 2015 wakati wa kampeni kwamba 25 Okt. Saa 4 tu tayari ushindi lakini hadi leo, na wafuasi ndiyoooooo.

Je tuamini kwamba Wafuasi hawa wanamuogopa m/kiti? Au hawana uwezo wa kutumia akili yao vizuri? Au ni kwa sababu ya kuzoea kutukana matusi? Maana hata humu kwenye hoja hii watatukana.

Na mtawajua kwa urahisi sana kwani hawakosi kutumia naneno ya matusi. Ukiona mtu kaandika sentesi mbili tatu au 4 na kutumia matusi , moja kwa moja huyo huna haja ya kupoteza mda kwani ni Li-Chadema.
 
Baada ya kukamilisha uloyataja item 1 to 5 aliifanyia nini chadema baadae?? Namaanisha Baada ya kushindwa eac, kupandishwa majukwaan etc..

Mikutano ya hadhara imezuiwa.. masha km wakili amefanya nn zaidi ya labda kucheka tu kijino pembe,
Hakuweza kutoka hadharani kulaunu au kutuongoza kwa lolote hata chadema inapokuwa legally in trouble. Mawakili wa chadema akina kibatala et al tunawaona jitihada zao.
Mwisho ivi km angeshinda EAC vp hangejitoa pia??
nyie UVCCM please vacate from our chadema
 
Ni haki yake kusema hayo kwa kua anajua mapuruzai ,anayo yaongoza hayana uwezo wa kuhoji!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom