Mbongo akinunua soda na kuziweka kwenye jokofu, hatatulia mpaka atakapozimaliza zote ndipo atapata amani

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_9148.JPG


Kwa sasa tunaishi maisha ya kizungu, ya kuwa na vyakula na vinywaji kwenye majokofu. Huu ni ustaarabu ulioletwa na wazungu na umeenea maeneo yote duniani. Kwa Nchi masikini kama Tanzania, majokofu yanatumika sana mijini kutokana na kipato mikubwa cha wakazi wa mijini.

Imeshafikia kama ni kitu cha aibu kwa mkazi wa Dar kukosa jokofu nyumbani. Watu wenye uwezo hununua kreti ya soda ha kuiweka nyumbani lakini wasio na uwezo hununua kuanzia moja na kuendelea.

Je, ulishawahi kujiuliza kuwa, majokofu ya familia nyingi za Bongo, ukitoa wale wa nafasi ya juu huwa hayana vinywaji muda mwingi?

Kwa kawaida, mara moja moja utaona familia inanunua soda labda mbili, tatu ama tano lakini changamoto inayowapata kama hawajazinywa soda hizo, watasumbuka sana siku nzima watazifikiria tu hizo soda. Yaani wasipozinywa wataendelea kuteseka kuwa wanakumbuka tu kuwa, kuna soda kwenye jokofu. Utashangaa kwa siku hiyo hiyo moja watajikuta wamezinywa soda zote.

Yaani wasipozinywa basi watapata tabu sana.

Wadau naomba kupata mwazo yenu, hili suala likoje kwako ama nyumbani kwenu: je, huwa na nyie kuna ka kitu kanakuwa kanawakereketa kuwa kuna soda kwenye jokofu?

Najua wazee wa gambe hawasumbukiagi visoda so siyo issue kwao.
 
Mi nafikiri ni mazoea na ugeni wa hivi vitu.

Tukiwa wadogo wakati mzee kanunua friji, alikuwa analeta matunda fuko zima ya aina tofauti.

Kipindi cha mwanzoni yale matunda yalikuwa tuna yamaliza yote. Lkn ilifikia kipindi tuka anza kuyachoka ikafikia hali matunda hatuyali mpk yanaharibika yakiwa kwenye friji.

Mimi nilikuwa addicted na Pepsi, yani haipiti siku sijagonga mbili.
Ikanilazimu niwe nanunua katoni naweka kwenye friji.

Lkn cha kushangaza kitendo cha kuwa nazo nikawa hata sizimwi.

Ukiona familia watoto roho hazitulii kwa vilivyo kwenye friji, jua hivyo vitu ni vigeni au vinapatikana kwa nadra sanaa!!
 
Ninavyojua mm unapokua na pirika nyingi sana unakua haukumbuki kama nimeeka kinywaji changu kwenye jokofu au chakula, sometimes unaweza kuweka kinywaji kizuri tu au chakula but kikaa mda mref adi wiki coz umesahau kama kuna kitu flan nimeweka ndani, but mara nyingi watoto ndio wanakunywa ama kutumia ulivyoviweka ndani ya jokofu, ndio maana unakuta havikai.
 
Hahahahah,dah hapa ngoja nijitege kesho najua patakuwa na burudani ya bure kabisa hapa!
 
Hii picha ni ya lini mkuu?

Mara ya mwisho uliona Fanta,Sprite ya kwny chupa za hivo lini mkuu?
 
Achana na friji,nikiwa boarding siku za wali nilikuwa natenga mara mbili ili jioni nisile ugali lakini kila mara nilikuwa napita na kupiga tonge hadi inafika saa 11 jioni wali wote umeisha unaenda kupokea ugali kwa unyonge huku unamulaumu shetani
Ulikuwa mroho Kama Kiranja wa zamu na kiranja wa chakula :cku za wali huwa wanajaza ndoo nzima na kupeleka bwenini

anyway ukiona una uroho na kitu ujue ktu hcho ni adim kwako ngawa sometimes kuna uroho wa kudumu kwa baadh ya watu
 
Achana na friji,nikiwa boarding siku za wali nilikuwa natenga mara mbili ili jioni nisile ugali lakini kila mara nilikuwa napita na kupiga tonge hadi inafika saa 11 jioni wali wote umeisha unaenda kupokea ugali kwa unyonge huku unamulaumu shetani
Dah!!! We ni balaa nimekuaminia. Of course umenikumbusha na mimi huko tukiwa A-level siku ya wali hupati sahani ya pile lakini siku ya makande ilikuwa at least rahisi kurudia. Mimi mwenyewe nilichukia sana ugali na maharage, so nilikuwa nikipata chance lazima nizame nao.
 
View attachment 891229

Kwa sasa tunaishi maisha ya kizungu, ya kuwa na vyakula na vinywaji kwenye majokofu. Huu ni ustaarabu ulioletwa na wazungu na umeenea maeneo yote duniani. Kwa Nchi masikini kama Tanzania, majokofu yanatumika sana mijini kutokana na kipato mikubwa cha wakazi wa mijini. Imeshafikia kama ni kitu cha aibu kwa mkazi wa Dar kukosa jokofu nyumbani. Watu wenye uwezo hununua kreti ya soda ha kuiweka nyumbani lakini wasio na uwezo hununua kuanzia moja na kuendelea.
Je, ulishawahi kujiuliza kuwa, majokofu ya familia nyingi za Bongo, ukitoa wale wa nafasi ya juu huwa hayana vinywaji muda mwingi?
Kwa kawaida, mara moja moja utaona familia inanunua soda labda mbili, tatu ama tano lakini changamoto inayowapata kama hawajazinywa soda hizo, watasumbuka sana siku nzima wakazi fikiria tu hizo soda. Yaani wasipozinywa wataendelea kuteseka kuwa wanakumbuka tu kuwa, kuna soda kwenye jokofu. Utashangaa kwa siku hiyo hiyo moja watajikuta wamezinywa soda zote. Yaani wasipozinywa basi watapata tabu sana.
Wadau naomba kupata mwazo yenu, hili suala likoje kwako ama nyumani kwenu: je, huwa na nyie kuna ka kitu kanakuwa kawakereketa kuwa kuna soda kwenye jokofu?

Najua wazee wa gambe hawasumbukiagi visoda so siyo issue kwao.


Kwa nini kila kitu ni lazima mlinganishe 1-1? Hivi na wao Wazungu hufanya hivyo? Kama wote tulipaswa kuwa sawa basi si wote tungekuwa Waafrika/Wazungu/Wachina/Waarabu?
 
Mi nafikiri ni mazoea na ugeni wa hivi vitu.

Tukiwa wadogo wakati mzee kanunua friji, alikuwa analeta matunda fuko zima ya aina tofauti.

Kipindi cha mwanzoni yale matunda yalikuwa tuna yamaliza yote. Lkn ilifikia kipindi tuka anza kuyachoka ikafikia hali matunda hatuyali mpk yanaharibika yakiwa kwenye friji.

Mimi nilikuwa addicted na Pepsi, yani haipiti siku sijagonga mbili.
Ikanilazimu niwe nanunua katoni naweka kwenye friji.

Lkn cha kushangaza kitendo cha kuwa nazo nikawa hata sizimwi.

Ukiona familia watoto roho hazitulii kwa vilivyo kwenye friji, jua hivyo vitu ni vigeni au vinapatikana kwa nadra sanaa!!
mangi umefunga mjadala
 
Hii inahusiana vipi na mimi kutokunywa soda?
Naona alihisi kuwa wewe unazipenda sana soda ila unavunga tu but mimi nimekuelewa kuwa, soda kwako zimeshakuwa kitu cha kawaida sana na haziwezi kusumbua kichwa chako unapokuwa nyumbani eti kuwa una soda ndani ya jokofu.
 
Umenikumbusha mbali sana kitambo Mkuu, tukiwa wadogo kijijini huko, mchele ukinunuliwa usipopikwa siku hiyo mtu unakosa aman kabisa unamuona mama mtu mbaya sana ,, ukipikwa unaoga mapema kabisa kuepusha shari na mama ,
Pia tulikuwa tunazunguka jiko eti uumuke uwe mwingi,, nikikumbukaga nacheka sana,,

Nimekulia mazingira ambayo mpunga haulimwi ndo maana nmeona mpunga ukiwa shamban nkiwa na miaka 20,, Chakula kulikuwa ni ndizi kwa kwenda mbele


Hyo tabia ya kuwaza kitu hivo inatokana na kitu kuwa nadra sana au kutokuwa na mazoea nacho,,
 
Back
Top Bottom